Eamon Jacky
New Member
- Feb 7, 2017
- 4
- 2
Nina mpenzi, huu ni mwaka wa pili sasa tupo kwenye mahusiano. Ila kwa bahati mbaya au nzuri, hatuishi pamoja kwa sasa mimi nipo Manyara kikazi na yeye yupo Songea kikazi. Kuna ugomvi ulitokea kati yetu hivi karibuni, alinikuta nawasiliana na ex wangu japo kuwa yalikua ni mazungumzo ya kawaida tu na wala hatukua na lengo baya ni basi tu kujuliana hali.
Ila kilichomkasirisha yeye sio kuwasiliana nae bali ni kukuta ile namba ya ex wangu kwemye simu yangu tena na tunawasaliana wakati yeye mwenyewe ndio aliifutaga kwenye simu yangu kipindi cha nyuma. Ameniblock kila sehemu mpaka instagram ameniunfollow leo ni siku ya nne.
Bado nampenda sana na nina malengo nae. Naombeni ushauri, nifanyaje?
Ila kilichomkasirisha yeye sio kuwasiliana nae bali ni kukuta ile namba ya ex wangu kwemye simu yangu tena na tunawasaliana wakati yeye mwenyewe ndio aliifutaga kwenye simu yangu kipindi cha nyuma. Ameniblock kila sehemu mpaka instagram ameniunfollow leo ni siku ya nne.
Bado nampenda sana na nina malengo nae. Naombeni ushauri, nifanyaje?