The Senetor
Member
- Aug 23, 2014
- 41
- 23
Wakuu poleni kwa majukumu, mimi si mwenyeji sana humu ila ndugu yenu nina jambo linanitatiza sana. Niliwahi kuwa na uhusiano wa kimapenzi na binti mmoja ambaye nilidumu nae kwa miaka 3 nilimsaidia hadi akafika chuo kikuu na nilipotaka kumwoa familia yake waliomba nimsubiri amalize masomo basi nilichofanya niliamua kumvisha pete ya uchumba kuonyesha upendo wangu kwake.
Baadae alibadilika sana na nikaja gundua ananisaliti kwa kuwa na uhusiano na mwanaume mwingine kwa muda wa mwaka mmoja.Niliumia sana na nikajitoa kwenye msururu baadae waliachana na jamaa na mimi baada ya miezi 6 nikatafuta mwanamke mwingine, julai mwaka huu akaanza kunitafuta kwa bidii nilimzuia asinipigie wala kunitumia sms lengo likiwa ni kumsahau kirahisi.
Huyu niliyenae ni mwelewa,ananiheshimu sana na kunipenda sana pia kimapenzi anajiweza mno yaani sijawahi kupata mwanamke anayenipa utamu kama yeye na sasa hivi ana mimba yangu ya miezi minne. Tatizo nililonalo ni mimi kumkumbuka sana yule ex kiasi natamani kumpigia simu na bado nampenda sana kweli moyo wangu unanirudisha sana nyuma nimejaribu kumsahau ili nimpende huyu lakini muda mwingi namwaza yule mwingine.
Wakuu samahani sana kama nitawakera nishaurini nifanyeje ili nimsahau na nimpende shemeji/wifi yenu mwenye mimba yangu au niwe nawasiliana nae kama rafiki tu.Samahanini sana kwa maneno mengi..
Baadae alibadilika sana na nikaja gundua ananisaliti kwa kuwa na uhusiano na mwanaume mwingine kwa muda wa mwaka mmoja.Niliumia sana na nikajitoa kwenye msururu baadae waliachana na jamaa na mimi baada ya miezi 6 nikatafuta mwanamke mwingine, julai mwaka huu akaanza kunitafuta kwa bidii nilimzuia asinipigie wala kunitumia sms lengo likiwa ni kumsahau kirahisi.
Huyu niliyenae ni mwelewa,ananiheshimu sana na kunipenda sana pia kimapenzi anajiweza mno yaani sijawahi kupata mwanamke anayenipa utamu kama yeye na sasa hivi ana mimba yangu ya miezi minne. Tatizo nililonalo ni mimi kumkumbuka sana yule ex kiasi natamani kumpigia simu na bado nampenda sana kweli moyo wangu unanirudisha sana nyuma nimejaribu kumsahau ili nimpende huyu lakini muda mwingi namwaza yule mwingine.
Wakuu samahani sana kama nitawakera nishaurini nifanyeje ili nimsahau na nimpende shemeji/wifi yenu mwenye mimba yangu au niwe nawasiliana nae kama rafiki tu.Samahanini sana kwa maneno mengi..