Naombeni ushauri,namempenda binti mlokole

Naombeni ushauri,namempenda binti mlokole

Habari wana MMU,

Kwanza napenda kuwapa pongezi members wa hili jukwaa ambao mmekuwa mkitoa mchango wa Mawazo katika mijadala mbali mbali ambayo imekuwa inaletwa mbele yenu! Kwa namna moja au nyingine imekuwa ikitusaidia sana, hususan kwenye swala zima la mapenz ambalo linaumiza akil na mioyo ya wengi wetu!

Mimi nina swala moja ambalo limekuwa likinisumbua, nimetokea kumpenda msichana mmoja ambae tumasoma nae hapa chuo, Ud. Ni binti ambae amesimama kiroho, anamisimamo yake ya kimaisha ikiwamo kumtanguliza mungu katika kila kitu!

Ni takriban mwaka mmoja sasa tangu nimeanza mazoea nae na kujaribu kujenga urafik lakin tatizo ni kwamba huwa harespond mesege, hapend kuchat, hata muda wa maongez na watu wengine huwa hana.,

Mara zote yupo bize na mambo yake, in shotly hapend mazoea na mtu yeyote! Nmejaribu kutumia kila njia na bidii ili kujenga hata mazoea nae imeshindikana!

Wadau ,naombeni ushauri wenu kwa wale wenye uzoefu na watu wa aina hii,

Nampenda sana na napenda aje kuwa mke wangu wa ndoa,
Nb. Mimi pia nampenda mungu...,


Hekima na busara itawaleee

Asanten,

Mmeonana kwa muda gani.
If just for a short time,mpe nafasi.Talk about other stuff:-family,hobbies,likes n dislikes,future life and mostly life-challenges based on the Bible.Usikurupuke kujadili kuhusu ndoa na sex.Kumbuka,ukaribu wako na yeye unampa naye nafasi yake yeye kukusoma.So don't rush. Give her your time,energy,emotions and who knows,labda ni yeye atakayesema anaku-feel.
Kila la heri.
 
Km kweli huyo dada ameokoka nakushauri usipoteze muda maana maisha ya kuokoka yana muongozo wake na taratibu zake ambazo sasa anazifuata ndo maana anakuvutia. Unawezza jitahidi kumpata but upande wa pili yaani yeye atakuwa ameasi ulokole wake ndipo atakuwa mtu wa kawaida kama wadada wengine. Mungu amekataza mtu mwenye imani fulani kuoana na mwenye imani nyingine viko vitu vingi vinaweza wasumbueni baadaye hata wewe utakuwa bored sana pale yeye yuko church wewe utapenda disco,..... Ushauri tafuta mtu mwenye the same interest you will a good chemistry
 
Mlokole waachie walokole wenzake waje wafaidi umeona faida ya kuokoka eeeeh!
Wacha uhuni wewe ....Aliyekuambia mapenzi yanahitaji dini ni nani...??? Attraction inatokea pasipo na dini....Mambo ya dini yatakuja baadaye....

Mwambie mwenzako akaze buti atapata....Ameshindwa tuu kum-fece directly...

Binafsi walokole wengi nimelamba sana...
 
mke mwema mtu hupewa na Mungu na sio JF! invest in prayers. muda huu unaouliza hapa jf ungekuwa unaomba ili upate mke mwema. labda umeshindwa tu kusema unataka utembee naye then usepe maana kama sio hivyo usingeongelea misimamo ya huyo binti ungejua tu hiyo ndo imani yake! spoils I dint mean kuchafua rather a reward or share!!

Hivi unaomba halafu Mungu anakupeperushia huyo mke...???

Kazima utafute, lazina uone, lazima upate intimate attraction kwanza, lazima ujichanganye,.....Ukishakuwa na circle ya kutosha ya marafiki hapo ndo utaomba Mungu kati ya hao marafi akuoneshe atakaye kuwa wako...

Imani bila vitendo ni mfu...
 
Nakumbuka mkakammmoja alianza hadi kuja kanisani kwetu ili tu ampate mdada hahahaha
 
Inakubidi na wewe uokoke kama kweli wamuitaji
 
Kumpata binti aliyeshikilia Imani inakuwa ngumu sana,cha kufanya usiwe na haraka ya kumpata kimapenzi.

Anza kwa kumpata kiroho kwanza na muaminishe kuwa huna nia mbaya nae.Ikiwezekana mfatane kila anapoenda ibada na sala za jioni muwe wote.

Kama mnasoma darasa moja jaribu kuwa unafanya naye discussion na hata muda wa msosi basi muwe wote.

Taratibu anza kumsoma hisia zake kama kweli anaingilika na anaweza kuwa katika mahusiano,kama utaona yupo tayari basi mwaga verses za maana zenye malengo na sio zile, oohh kwetu tuna pesa blah blah kibao weka pembeni.Na kama haingiliki basi jombaa chapa lapa usije hadhirika maana atakukataa na urafiki wenu ndo utakuwa mwisho.

pia kama ni binti mcha mungu kweli ujue kila hatua anayopiga lazima amshirikishe pastor wake huwa ni kama baba au mama wa kiroho
 
nilikuwa namjibu jamaa kutokana na alicho andika. wewe umejibu kutokana na jibu nililo toa. kama unataka tuwe sawa ungeuliza je Mungu anakushushia huyo mke bila kutafuta? hapo tungeelewana.
 
Hivi unaomba halafu Mungu anakupeperushia huyo mke...???

Kazima utafute, lazina uone, lazima upate intimate attraction kwanza, lazima ujichanganye,.....Ukishakuwa na circle ya kutosha ya marafiki hapo ndo utaomba Mungu kati ya hao marafi akuoneshe atakaye kuwa wako...

Imani bila vitendo ni mfu...

huwezi kumwomba mungu mke mwema huku unae kichwani tayari
 
Km kweli huyo dada ameokoka nakushauri usipoteze muda maana maisha ya kuokoka yana muongozo wake na taratibu zake ambazo sasa anazifuata ndo maana anakuvutia. Unawezza jitahidi kumpata but upande wa pili yaani yeye atakuwa ameasi ulokole wake ndipo atakuwa mtu wa kawaida kama wadada wengine. Mungu amekataza mtu mwenye imani fulani kuoana na mwenye imani nyingine viko vitu vingi vinaweza wasumbueni baadaye hata wewe utakuwa bored sana pale yeye yuko church wewe utapenda disco,..... Ushauri tafuta mtu mwenye the same interest you will a good chemistry

kweli kabisa
 
huwezi kumwomba mungu mke mwema huku unae kichwani tayari

Soma nilichoandika between the lines.......Au ukishakuwa mcha Mungu hutongozi.....?? Hiyo ni process ndugu katika maisha na lazima upitie...

Sasa wewe jifungie ndani au kanisani halafu usubiri Mungu akuteremshie......You must have something to show....

Hata Yesu alipo fanya muujiza wa samaki wawili na mikate mitano...Hakushusha muujiza...kulikuwa kuna kitu kidogo ndo maana akaongeza....

Rejea kitabu cha Wafalme uone Eliya alivyomfanyie muujiza yule mama mjane na mwanaye waliokiwa wanasubiri kufa......Walikuwa na kitu cha kuonesha....

Muoneshe Mungu marafiki zako hata 20...halafu msihi akuchagulie....

Imani bila matendo ni mfuuuuu!!!! Shauri yako..
 
kweli kabisa

Kizazi cha Ibilisi hiki.....Nyinyi watu nani kawalogaaaaa......Hivi Yesu alikuja kwa wema tuuu.....?? Yesu alikuja duniani kwa watu wote ili waokoke......

Ni wapi Biblia imesema oaneni watu wa dini moja.. ??? Ukitaka kumvuta mtu kwako lazima uwe naye...Lazima umuoneshe uzuri wa unacho kiabudu....
Sijui nani kawapumbaza akili zenu nyie kizazi cha ibilisi..

fool
 
ongea kwanza na Mungu, kisha Mungu ataenda mpelekea ujumbe wake, pindi binti atakapoomba Mungu ampe Mume mwema, namaanisha ingia nkiroho, kinyume na hapo subiria ukemewe kama kashetani kadogo kadogo.

Sawa mkuu, hata mimi pia nampenda na kumtumikia mungu
 
Mmeonana kwa muda gani.
If just for a short time,mpe nafasi.Talk about other stuff:-family,hobbies,likes n dislikes,future life and mostly life-challenges based on the Bible.Usikurupuke kujadili kuhusu ndoa na sex.Kumbuka,ukaribu wako na yeye unampa naye nafasi yake yeye kukusoma.So don't rush. Give her your time,energy,emotions and who knows,labda ni yeye atakayesema anaku-feel.
Kila la heri.

Thanx, we have been friend almost a year now!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom