Song of Solomon
JF-Expert Member
- Aug 5, 2021
- 2,733
- 5,490
Mke wangu alichukua simu yangu na kufuta namba ya mpenzi wangu mwingine, namba ya Magreth na kuhifadhi namba yake ya kuwa anaitwa Magreth.
Sikujua kuwa kuna mtu alimwambia mke wangu kuhusu Magreth, kisha nikapokea SMS kutoka kwa Magreth akiomba pesa Sh.250,000.
Nilimkimbilia mke wangu kwa kuwa sikuwa na hiyo hela wakati huo na kumdanganya kuwa nahitaji Sh. 250,000 kwa dharura. Nilimwambia kuwa mdogo wangu Rutta anaumwa na anahitaji pesa haraka.
Mke wangu alinipa zile pesa na nikakimbilia kutuma kwenye akaunti namba iliyoandikwa kwenye ule ujumbe.
Nikiwa nimejipumzisha nyumbani baada ya kutoka kazini, niliendelea kuwaza iwapo Magreth alipokea pesa hizo.
Nilimtumia SMS ili kujua kama alikuwa amepokea pesa. Jibu lake lilikuwa, "Nipigie sasa."
Nilitoka nje nyuma ya nyumba kupiga simu.
Weeeeeeh!
Unaweza kufikiria uso wangu wa kutisha ulivyokuwa niliposikia sauti ya mke wangu badala ya Magreth!
Leo ni siku ya tatu bado nimesimama nje.
Sijui jinsi ya kurudi nyumbani kwangu !!!
Ushauri wowote tafadhali ...
Sikujua kuwa kuna mtu alimwambia mke wangu kuhusu Magreth, kisha nikapokea SMS kutoka kwa Magreth akiomba pesa Sh.250,000.
Nilimkimbilia mke wangu kwa kuwa sikuwa na hiyo hela wakati huo na kumdanganya kuwa nahitaji Sh. 250,000 kwa dharura. Nilimwambia kuwa mdogo wangu Rutta anaumwa na anahitaji pesa haraka.
Mke wangu alinipa zile pesa na nikakimbilia kutuma kwenye akaunti namba iliyoandikwa kwenye ule ujumbe.
Nikiwa nimejipumzisha nyumbani baada ya kutoka kazini, niliendelea kuwaza iwapo Magreth alipokea pesa hizo.
Nilimtumia SMS ili kujua kama alikuwa amepokea pesa. Jibu lake lilikuwa, "Nipigie sasa."
Nilitoka nje nyuma ya nyumba kupiga simu.
Weeeeeeh!
Unaweza kufikiria uso wangu wa kutisha ulivyokuwa niliposikia sauti ya mke wangu badala ya Magreth!
Leo ni siku ya tatu bado nimesimama nje.
Sijui jinsi ya kurudi nyumbani kwangu !!!
Ushauri wowote tafadhali ...