Naombeni ushauri kuhusu jambo hili

Naombeni ushauri kuhusu jambo hili

Kuboja A

Member
Joined
Sep 16, 2018
Posts
9
Reaction score
13
Habari ndugu zangu?,

Naomba mnisaidie ushauri maana nina jambo gumu hapa. Mimi ni mtumishi, nilipata shida ya kifedha nikamtafuta mdada mmoja akaniazimia pesa kwa mtu laki mbili na nusu, nilitakiwa kurudisha kwa riba.

Nilimrudisha riba mara mbili baada ya hapo mambo yakagoma kabisa, yule Dada aliyeniazimia pesa kwa mtu akawa aelewi kabisa, akanibadlilishia kibao kuwa ile pesa aliniazimia kwa mume wake ambaye ni askari, huku mwanzoni alisema aliniazimia kwa mfanyakazi mwenzie, yeye anafanya kazi hospital. Sasa huyo askari Kesi kaichukua yeye anadai pesa zilikua zake, ananitishia kweli, siku moja akaja na defender kazini kwangu ili anikamate ila sikuwepo.

Sasa mwisho wa week iliyopita nikakutana nae akiwa na mkewe, akaoneshwa ndio Mimi,akakomaa twende kituoni au nimpe kitu chochote akae nacho, mie nikamuomba mwisho wa mwezi ujao ntaanza kumlipa nikamwambia changamoto nilizokua nazo lakini akuelewa, akanipeleka kituoni anachofanyia kazi akani harass na askari wenzie, nikawasiliana na mfanyakazi mwenzangu akaja akaongea nae lkn aelewi akamuomba ifikapo jumanne yaani juzi atampa laki moja.

Yule askari akamwambia niache sim au aniwake lokapu,nikaacha sim kwa yule mfanyakazi mwenzangu ili abaki nayo hadi nitakapomaliza Deni ndio anipe,nikamwachia sim.Sasa hiyo jumanne ikapita yule mwenzangu akupata pesa.

Jana jumatano wakamfuata kazini awape ile sim yangu, yeye akawaambia IPO nyumbani maana walikuja watatu, ikabidi waende hadi kwake kufika kwake mkewe akuwepo,chumbani kumefungwa,bado awakuelewa wakachukua sim yake, wakampa kazi akirudi mkewe aipeleke hiyo sim yangu kwa huyo askari ndio wampe yake.

Sasa jamani nisaidieni nifanyeje? Nia yangu ni kumlipa kuanzia mwezi ujao, nilipata misukosuko ya kimaisha na nikamweleza ila aelewi,yaani ananikosesha amani na pesa akunipa yeye.

Nisaidieni wana jf
 
Umefanya makosa makubwa kukubali kwenda kituoni,bora ungekubali wakuue hapohapo walipokuchukulia....

Huyo usimlipe endelea kumsumbua hivyo hivyo labda ukamlipie mahakamani,tena akija kukudai mwambie me saizi sina hela kama hutaki niuwe...

KAWAIDA YA DENI,MDAI WAKO AKIKUTANGAZA ANAKUA AMESHAJILIPA...

Halafu kama mliandikishiana juujuu,mwambie sikujui
 
Mwambie huyo jamaa yako akawafungulie kesi mahakamani.

Na wewe mkatae jamaa mwambie yeye haumtambui sababu haukufanya biashara nae kama vipi na akupeleke mahakamani.

Ukifika mahakamani kubali kosa lakini ukubali kwamba utalipa taratibu kutokana na changamoto ulizopata.

Pia siku nyingine usije ukakubali akupeleke kituoni na kama noma acha iwe noma (jifunze ukakamavu jamaa)
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom