Naombeni ushahuri kwa hili

Naombeni ushahuri kwa hili

Playboy

JF-Expert Member
Joined
Aug 11, 2011
Posts
1,170
Reaction score
945
Habari zenu wana JF wenzangu poleni na majukumu ya hapa na pale ya ujenzi wa taifa hili.Baada ya kutakia kheri,pia napenda kuishukuru jamii forum kwa kuwa moja ya msaada kwangu hasa kujua mambo mengi hasa nyanja za kisiasa,kitamaduni pia kijamii nimeweza kujua mengi kupata ushauri mwingi na baadhi ya vitu nilivyovikuta huku nimeviapply katika maisha yangu vikanisaidia sana..Aksanteni sana kwa hilo.
Dhumuni la kuleta uzi huu ni kuomba ushauri juu la swala hili.
Mimi ni kijana wa kiume niliyezaliwa miaka 25 iliyopita nimeanza kuwa katika mahusiano hasa ya kimapenzi tangu nikiwa na miaka 15 nimepitia changamoto nyingi kama mjuavyo MAPENZI yalivyo na changamoto zake.
Kuomba ushauri hasa ni juu ya hili swala,miezi miwili iliyopita kabla sijamaliza masomo yangu ya degree ya kwanza kwenye chuo kimojawapo jijini Dar es Salaam,nilikutana na mwanamke mmoja ambaye ni rika langu,basi katika harakati za hapa na pale yule mwanamke akavutiwa na mimi akaomba tuwe wapenzi basi mie na moyo wa hurumaa nikamkubalia binti yule tukawa wapenzi ,mpaka sasa tupi naye for two months;

Suala lililokuja kujitokeza sasa ambalo ndo naomba ushauri kwenu,Mimi nilikuwa tayari nina mwanamke ambaye pia ni mwanafunzi tuliye maliza nae chuo ngazi ya degree ya kwanza ambaye tumewekeana malengo sana ya maisha baadaye.Sasa mwanamke huyu niliyeanza naye mapenzi miezi miwili iliyopita amegundua nina mwanamke mwingine na kikubwa zaidi ana mimba yangu ya miezi mitatu na wiki mbili na mwanamke wa sasa kujua yotee baada yakupata mawasiliano na mwanamke wangu wa kwanza wakasimuliana yoteeee,ilikuwa mtitiii acheni tuuu.

Suala lililokuja mezani kwa huyu mwanamke wa pili kanufuata getoo na kuniekeza hayaaa
"Mimi nakupenda sanaaaaa tena sanaaa hapa nilipo nilifunga kizazi,akanioneshea alama hiyo ambayo ipo mkononi chini ya kwapa ukigusa kuna kama kakamba iviii (sijui kama ndo kweli ndo ufungaji wa kizazi uo au laaah)..basi akaendelea tiririka..nilifunga kizazi baada ya kupewa mimba na mwanaume nimpendaye akaikataa mimba ilee ajasema sio yake bahati nzurii nilijifungua salamaa mtoto wa kiume kwa kuwachukia wabaume wote duniani nikaamua kufunga kizazi, sasa basi hapa nipo tayari kufungua kizazi kwa sababy ww tayari una mwanamke wako nataka unipe MIMBA tu uka suala la kulea niachie mimi nitalea sita taka hata senti tano yako then nikuachue uendelee na mwanamke wako lasi ivyo nitahakikisha huta kuwa na huyo mwanamke wako uliyena mimba yako mimi nataja unipe mimba tuu basi nimeamua kufanya hivi sababu nakupenda na napenda hata nisipo kuwa na wewe niwe na damu yako"...akamaliza....

Jamani wana jamii forum nimebaki njia panda sijui nifanyajeeh na amenipa siku tatu kufikiri; naombeni ushauri jamani naombeni nipo njia panda ni hayo tu.
 
subiri mpnz wako wa kwanza ajifungue uvae majukumu ya baba, acha kuhangaika,
unadhani kama ameomba mimba atashindwa kuomba hela?
 
Hiyo njia panda ya kujitakia, kwani unavyomkubalia hukujua una mwanamke?
 
Si unajua tamaa za kimwili ambazo humpata mtu yoyote nao ndo naona madhara yake.shida ni huyu mwanamke wa pili kaleta headache
 
Ushauri wako now mzuriiiii wa kuchezea libolo fc ila mi naomba ushauri wa kuokoa penzi langu
 
Simama kama mwanaume, unatishiwa nyau, km utaka kujuta ktk misha yako fanya kosa la kumpa mimba huyo kichenchede, angalia mbele tulia na huyo mwenye mimba yako, umeona wapi mimba inadaiwa kwa vtisho?
 
Mimi naona hii elimu yetu bongo inashuka kweli,yaani watu wanamaliza vyuo uwezo wao wa kufikiri ni mdogo mno kama mtu wa form 4,janga kwa taifa.
 
Japo umetudanganya tutakushauri,maana haiwezekani mwanamke akutongoze halafu ushindwe kumwambia kuwa una mtu tena ukizingatia mtu wako ni mjamzito.Pole kwa kulikoroga.

Lakini pole pia kwa kunasa kwenye mtego wa huyo wa pili wa kutaka umpe mimba.Kitendo cha wewe kuja kuomba ushauri kina onyesha kuwa kwa namna moja unataka kumkubalia ombi lake.

Pia pole kwa kuwa muoga maana inaonekana kitisho chake cha kusambaratisha uhusiano wako kimekuingia,kwa hili pia pole kwa kutokuwa mwanaume shababi maana ningekuwa mimi hicho kitisho ndio ingekuwa tiketi yake

Ushauri: Ukitaka uje kuishi maisha magumu hapa duniani basi wewe mpe huo ujauzito anaotaka.
 
Kama ndio mambo watanzania tunayoyafanya na kuyafikiria haya..basi ccm itatawala milele.
 
Wee mpe tuu hy mimba, sioni shida iko wapi sii kataka mwenyewe? Kwani unaenda kununua dukani hadi uone ugumu wa hili.
 
mkuu mtoto angekuwa ni mdoli wa kumnunua karume na kumpa basi sawa ungempa mtoto... ila mtoto ni damu yako pia... so angalia isje ikawa shida katika maisha yako ya baadae maana damu nzito kuliko maji.... ukawa unataka upaweke sawa kwa huyu kumbe kwa mwengine unaharibu... tulia watoto wakiwa na mama tofaut tofaut huwa sio sana....
 
Njia panda ya kujitakia hiyo,subiri utaona wanaanza kupasua Nazi na mayai
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom