Naombeni mwongozo

Fixed Point

JF-Expert Member
Joined
Sep 30, 2009
Posts
11,304
Reaction score
12,753
Nawasalimu wana MMU.

Jamani tuna hawa wadada wanatusaidia kukaa na nyumba zetu.

Kama tujuavyo maisha ya siku hizi bila simu inakuwa patashika kidogo.

Huwa mdada akija kama hana simu huwa nampa simu ambayo nimeinunua kwa ajili ya nyumbani ili niweze kuwasiliana naye naye awasiliane nami ambapo sipo nyumbani.

Na kama inatokea mdada kaja na simu yake basi simlazimishi atumie ile yangu, huwa natumia tu ile namba yake kwa mawasiliano.

Kinachotokea mpaka naomba mwongozo hapa ni kwamba; Huwa nampa sh. 1000 kila wiki kwa ajili ya simu, ili akipata dharura basi aweze kunitaarifu. Mara nyingi mimi huwa napiga simu nyumbani mara kwa mara kwa hiyo inatokea mara nyingi tu ndani ya wiki hajanipigia wala kutuma sms hata moja, na yaweza kuwa hivyo hata mwezi mzima.

Kinachonichosha, siku ikitokea kapata dharura wala hapigi, nikiuliza naambiwa simu haina hela.

Wenzangu pia mnakumbwa na hili tatizo?

Nifanyeje sasa ili hili tatizo liishe?

sababu wakati mwingine ni jambo la maana kabisa linatokea lakini hawezi kuniambia kisa hela kwenye simu kamaliza zoote kupigia watu wake, sasa maana yoooteee ya mimi kumpa hela ya simu inakuwa haipo.

Nimepata mdada mpya sasa nataka nianze naye tangu mwanzo sheria ya hela yangu ya simu iweje........
 
Usimpe hela weka tu utaratibu wa kupiga kila siku mara mbili au tatu..au weka hela simu ya nyumbani sio yake
simu ya nyumbani ndo ambayo anaitumia, in case hana yake, na tatizo bado ni lile lile.
Ukweli kati ya watu wanaopiga simu nyumbani mara kwa mara ni mimi, na ndo maana anaweza kukaa wiki nzima hajanipigia. lakini sasa inatokea umepiga tu baada ya muda kukatokea dharura, labda mgeni kaja au chochote kile ambapo dada inabidi anitaarifu; sheshe ndo linaanzia hapo.
 
Reactions: BAK
Muelimishe atakuelewa na umuambie wala haitaji kukupigia akubeep tu kunapokuwa na dharura, au umuonganishie kifurushi cha wiki hata kama atamaliza muda wa maongezi bado atakuwa na msg za kutosha hivyo kunapokuwa na dharura atakutumia msg.


Sent from my iPhone using JamiiForums mobile app
 

Karibu airtel yatosha package..but Tafuta wataalam simu ifanyiwe settings ipige namba fulani tu...namba zingine haipigi
 
Hapo hamna usuluhishi zaid ya kukata huduma ya kumuwekea vocha,hata mm wife alilalamika anampa vocha bt inaishia kupigia ndg zake sasa hv huduma tumekata kbs tunapiga sisi kama akitaka vocha anunue mwnyw apige atakavyo....mabeki 3 akili zao wote ni moja.
 
Nunua bundle ya wiki nzima. Asipate sababu. Je anajua jinsi ya kutumia hizi bundles au...?
anajua kutumia bundle ila sasa hela yooote inaishia kupiga simu zake anazozijua
 
Reactions: BAK
Ukweli kati ya kitu sikitaki ni kuni-beep, ndo maana nampa hela ya airtime, sitaki kabisa huo mchezo
 
Reactions: BAK
Karibu airtel yatosha package..but Tafuta wataalam simu ifanyiwe settings ipige namba fulani tu...namba zingine haipigi
Asante rafiki.
Ila sasa nikiiblock kupiga namba nyingine si nitakuwa namwonea? akitaka kuongea na wazazi wake au ndugu wengine itakuwaje?
 
Reactions: BAK
Wadada wanachosha sana nahis IQ ndogo
Kikubwa weka masharti kuwa pesa unayoweka isitumike kinyume na mashart

Ila kuwa mtu wa kupiga simu home hta mara 3 kuepusha matatizo.
 
nakuambia, hawa watu ni majanga.
Yaani siku mwanangu wa mwisho anaenda boarding school nitapumua sana, yaani sitathubutu kuendelea kukaa na hawa watu hata kwa siku moja, nakaa nao tu sababu ya watoto
 
Ukweli kati ya kitu sikitaki ni kuni-beep, ndo maana nampa hela ya airtime, sitaki kabisa huo mchezo

Basi muunganushie bando la wiki na umuambie ni kwa ajili ya dharura hapo nyumbani kama anataka kuwasiliana na ndugu au rafiki zake awatumie msg period.


Sent from my iPhone using JamiiForums mobile app
 
Wadada wanachosha sana nahis IQ ndogo
Kikubwa weka masharti kuwa pesa unayoweka isitumike kinyume na mashart

Ila kuwa mtu wa kupiga simu home hta mara 3 kuepusha matatizo.
home napiga sana simu, yaani hata mara 5 kwa siku, lakini hiyo haizuii kutokea dharura inayohitaji simu ya haraka.
sasa sijui nimuingize kwenye zile sms za wiki bila kupiga ili awe anatuma sms. ingawa sasa sms kwangu huwa siyo dharura, naweza soma jioni kama mchana nimebanwa sana, au nikaisoma baada ya masaa 2
 
Reactions: BAK
nakuambia, hawa watu ni majanga.
Yaani siku mwanangu wa mwisho anaenda boarding school nitapumua sana, yaani sitathubutu kuendelea kukaa na hawa watu hata kwa siku moja, nakaa nao tu sababu ya watoto

Mwanangu ananifurahisha tukirudi jioni anatoa taarifa ya kila kitu ambacho sio cha kawaida kilichotokea home
 
Una block simu ya home unayoweka pesa..yake huigusi
umenipa akili nyingine hapa rafiki.
huwa sitenganishi simu ya home na yake. kama ana yake basi ile ya home naihifadhi na natumia yake kwa mawasiliano, kwa hiyo hata hela nampa aweke kwenye hiyo yake. sasa labda nimpe tu na yangu, ila kupiga niwe naipiga ile yake, hela niweke kwenye yangu na niiblock. akipata dharura atatumia ile yangu kunipigia.
WAZO ZURI HILI
 
Basi muunganushie bando la wiki na umuambie ni kwa ajili ya dharura hapo nyumbani kama anataka kuwasiliana na ndugu au rafiki zake awatumie msg period.


Sent from my iPhone using JamiiForums mobile app
ha haaa, atanielewa unafikiri?
 
Reactions: BAK
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…