Mfalme_wa_Nyika
JF-Expert Member
- May 24, 2023
- 684
- 1,541
Wadau kila mtu ana siri za maisha yake. Mimi kifupi ni mtu mzima nina maisha nimeenda shule na nina njia zakujipatia kipato.
Kifupi nina rafiki yangu daktari alinionesha kwa simu hii kamari ya hili game - Aviator siku moja tukiwa tumepumzika mahali.
Kuanzia siku ile mwaka 2022 mpaka leo maisha yangu yamebadilika. Yaani ni mimi na aviator tu kila pesa nikipata naweka huko na ninaliwa yaani kuna kipindi kwa wiki naliwa si chini ya 3M...
Imagine, yaani najitahidi kuacha lakini siwezi ile uchungu wakupoteza napata kiu kila ninaposhika pesa a naongeza dau na mpaka moyo wangu umekuwa siku hizi kama hauna hisia tena, naweza eka leo 250K ikaliwa ndani ya dakika kumi, nabaki mtupu kuombaomba.
Imefika hatua nataka kuuza mpaka magari yangu ili nicheze Aviator, thanks kea girlfriend wangu anayenishaurigi nisiuze gari ingawa hajui mimi nacheza kamari, yaani hii siri natoa hapa kwenu sijawahi mwambia mtu yeyote.
Kuna saa nawaza nikate eneo a shamba langu niuze ili niweze kurudisha pesa niliyopigwa na mhindi kwenye Aviator maana kwa mwaka toka 2022 napoteza si chini ya milioni 25-35 kwa hesabu za juu juu nilizofanya.
Nawaza kama Aviator ningeijua kabla sijafanya chochote kwenye maisha leo nisingekuwa na kitu chochote, ila hatari iliyopo ni kuwa sasa yaani kwa siku naweza kupata laki tatu nne ila yote inaisha kwa Aviator,
Hakuna hela inakaa mkononi, mpaka inataka kuharibu mahusiano, girlfriend wangu anajua nina uwezo wa kuwa na hela ila kuna wakati anasema inakuwaje nashindwa kumhudumia pesa napeleka wapi ila kumwambia mimi ni teja wa kamari ya Aviator nashindwa naona aibu nazidi kujichimbia kaburi la umasikini mfarakaniko na self denial...
Naombeni maana imenibidi niandike hili baada ya uchungu nimeweka leo jumla ya 400K na mhindi kala yote yaani asubuhi nilikua na 400K mda huu sina hata mia na kuna saa nilipata mpaka 3.6M ila mhindi akairudisha yoooote.
Mazee nimechoka haya maisha naomba mtu aniambie jamani niachaje kamari hiii!? Sitaki haya maisha....
Kuna saa napata hasira balaa ataka mpaka kujidhuru naniuliza nina pepo gani!?
Naomba msaada wa hali na mawazo niweze kuachana na hii kamari ya mchezo wa Aviator.
Kifupi nina rafiki yangu daktari alinionesha kwa simu hii kamari ya hili game - Aviator siku moja tukiwa tumepumzika mahali.
Kuanzia siku ile mwaka 2022 mpaka leo maisha yangu yamebadilika. Yaani ni mimi na aviator tu kila pesa nikipata naweka huko na ninaliwa yaani kuna kipindi kwa wiki naliwa si chini ya 3M...
Imagine, yaani najitahidi kuacha lakini siwezi ile uchungu wakupoteza napata kiu kila ninaposhika pesa a naongeza dau na mpaka moyo wangu umekuwa siku hizi kama hauna hisia tena, naweza eka leo 250K ikaliwa ndani ya dakika kumi, nabaki mtupu kuombaomba.
Imefika hatua nataka kuuza mpaka magari yangu ili nicheze Aviator, thanks kea girlfriend wangu anayenishaurigi nisiuze gari ingawa hajui mimi nacheza kamari, yaani hii siri natoa hapa kwenu sijawahi mwambia mtu yeyote.
Kuna saa nawaza nikate eneo a shamba langu niuze ili niweze kurudisha pesa niliyopigwa na mhindi kwenye Aviator maana kwa mwaka toka 2022 napoteza si chini ya milioni 25-35 kwa hesabu za juu juu nilizofanya.
Nawaza kama Aviator ningeijua kabla sijafanya chochote kwenye maisha leo nisingekuwa na kitu chochote, ila hatari iliyopo ni kuwa sasa yaani kwa siku naweza kupata laki tatu nne ila yote inaisha kwa Aviator,
Hakuna hela inakaa mkononi, mpaka inataka kuharibu mahusiano, girlfriend wangu anajua nina uwezo wa kuwa na hela ila kuna wakati anasema inakuwaje nashindwa kumhudumia pesa napeleka wapi ila kumwambia mimi ni teja wa kamari ya Aviator nashindwa naona aibu nazidi kujichimbia kaburi la umasikini mfarakaniko na self denial...
Naombeni maana imenibidi niandike hili baada ya uchungu nimeweka leo jumla ya 400K na mhindi kala yote yaani asubuhi nilikua na 400K mda huu sina hata mia na kuna saa nilipata mpaka 3.6M ila mhindi akairudisha yoooote.
Mazee nimechoka haya maisha naomba mtu aniambie jamani niachaje kamari hiii!? Sitaki haya maisha....
Kuna saa napata hasira balaa ataka mpaka kujidhuru naniuliza nina pepo gani!?
Naomba msaada wa hali na mawazo niweze kuachana na hii kamari ya mchezo wa Aviator.