Naomba ushauri

Naomba ushauri

Digoxin JR

Member
Joined
Jul 1, 2014
Posts
83
Reaction score
14
Kuna mdogo wetu wa kike aliondoka miaka miwili ilyopita, alituaga ameenda kutafta kazi hyo ilikua ni baada ya kupata certificate yake ya mambo ya uhasibu.. leo amekuja nyumban baada ya hyo miaka miwili akiwa na mtoto mchanga(mwez mmoja). Cha ajabu tunamhoji baba wa huyo mtoto ni nan hataki kusema anakaa tu kmya.. tumechukua jukumu la kumhoji kwa sababu amekuja na mtoto ambaye tiyar kwa tamadun zetu sio sehemu ya ukoo wetu. Tumeita had wazee wa kijiji lakin bado hataki kusema baba wa mtoto niyup.. tunaomben ushauri wa mawazo jamani tufanyeje???
 
kwaza poleni sana kwa matatizo hao ila chamsingi nikukaa nae kiumakini mimi namini ataongea tu ika msimpige mana hata mkimpiga haitasaindia hata kidogo jalibuni kumsii kwa utalatibu mimi nihao tu kwa ushauli wangu ndo huo
 
Mngempa muda kwanza, mmeharakisha mno.

Cha kufanya kwa hivi sasa msimbugudhi mwacheni, hamuwezi jua alikutana na masahibu gani. Pengine alibakwa hamuwezi jua.

Msimtenge na kumfanya kujisikia jamii haimtaki, endeleeni kuwa nae baada ya muda kidogo kidogo atakuja kufunguka kuwaambieni kilichomsibu
 
hata mimj na chagiq hio hoja nikweli huwezi jua kilicho mpata namini akitulia bona ataongea yaeye mwenyewe kuweni wapole na msimuone kama wa kwajilani muacheni madonda ya moyoni yaishe
 
Hicho ndio cheti cha kazi wala achaneni nao
 
Nyie alipoaga miaka 2 yote mlikua hamjui alipo? Hamkuwasiliana nae kipindi chote?! Leeni jombaa bhana.
 
Mkisha jua baba wa mtoto iwasaidie nini ? Kama kauchuna basi mkaushieni,lakini jamaa si anasimamia shoo
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom