Naomba ushauri

Naomba ushauri

Mabawe

Member
Joined
Jun 22, 2014
Posts
22
Reaction score
0
Habari za kazi wanajamvi,

Niliwahi kuomba ushauri hapa,nashuuru nilifanikiwa.

Kuna tatizo limetokea tena kwa huyu mzazi mwenzangu, aliomba awe anakuja kumuona mtoto binafsi sikuafikiana nae na sikuwahi kumuosha ninapoishi amepatafuta mpaka amepapata.

Ameibuka anadai anataka tuoane tulee mtoto, la tatizo mwenzangu sijui niseme wivu wa kijinga hataki niwe na namba za wafanyakazi wenzangu hata ndugu zangu asiowajua ni matatizo hajawi kuja kujitambulisha kwa ndugu zangu na wala hawajui.

Nikipigiwa simu anafoka weka loudpeaker kila wakati anakagua simu ila ya kwake hakuna kushika na anataka nibadilishe line na nilishamwambia simtaki hanielewi.

Ninakofanya kazi nimepata mkopo mungu amenisimamia nimeanzisha biashara na pia mwanangu nampa matunzo bila shida hatumuombi chochote ndio maneno eti nina kiburi,na anataka niwe nampa pesa yeye kazi hana na mie siwezi kumpa.

Naombeni ushauri nifanye nini sina raha mpaka ananitishia maisha
 
Achana naye lea mtoto wako, atakuzingua na wivu wake wa kijinga
 
dahh mim ningekuwa wew ningemtikisa mpk akame ila sema na wew unamoyo sana kama bado unampnda fula hivi eT??????? ila cha msingi ni msimamo wako ila kama utayumbishwa alafu hajakuoa ni changamoto kubwa uliyonayoooo
 
cc12 itabidi nijifunze hilo maana ni ujinga sana kumwendekeza
 
Habari za kazi wanajamvi,

Niliwahi kuomba ushauri hapa,nashuuru nilifanikiwa.

Kuna tatizo limetokea tena kwa huyu mzazi mwenzangu, aliomba awe anakuja kumuona mtoto binafsi sikuafikiana nae na sikuwahi kumuosha ninapoishi amepatafuta mpaka amepapata.

Ameibuka anadai anataka tuoane tulee mtoto, la tatizo mwenzangu sijui niseme wivu wa kijinga hataki niwe na namba za wafanyakazi wenzangu hata ndugu zangu asiowajua ni matatizo hajawi kuja kujitambulisha kwa ndugu zangu na wala hawajui.

Nikipigiwa simu anafoka weka loudpeaker kila wakati anakagua simu ila ya kwake hakuna kushika na anataka nibadilishe line na nilishamwambia simtaki hanielewi.

Ninakofanya kazi nimepata mkopo mungu amenisimamia nimeanzisha biashara na pia mwanangu nampa matunzo bila shida hatumuombi chochote ndio maneno eti nina kiburi,na anataka niwe nampa pesa yeye kazi hana na mie siwezi kumpa.

Naombeni ushauri nifanye nini sina raha mpaka ananitishia maisha
NAkuona ma ww hujielewi hivi inakuaje mtu hukuonana nae kwa muda then amepatafuta unapo kaa amepafaham harafu ghafla unawasiliana nae tena unampa na sim anataka uweke loudspeaher unapoongea na cm,na mpaka unazoeana nae tena ulianzaje mtu alikuzalisha na hakuwa na mpango na ww?usitufanye wajinga bwana ww huyo unampenda ss unataka kutuchonganisha bure,ww linywe yuu limalize mwenyewe
 
namba anayo sikuwahi kubadilisha anakuja kumuona mtoto lakini namshangaa anakuwa na wivu na mtu asie mpenzi wake hapo ndio tatizo nilishamwambia simhitaji tena hanielewi
 
ndio mie ni binadamu nina mapngufu yangu pia, lakini ilishakubali kila mtu ashike njia yake mungu hamtupi mja wake nina muda malezi ya mwanangu bado na yeye tena kisa anaona ninacho hapana kwakweli
 
Pole sana dada yangu, wanaume (japo sio wote ila ni wengi) sijui tumekula maharage ya wapi? Tumekuwa watu wa kuzalisha na kukimbia majukumu. Kina dada wanajitahidi kutulelea watoto Lakini choko choko haziishi. Nakushauri jitahidi kila unapoongea nae onyesha unamaanisha kile unachosema (hata kwa body language). Vinginevyo dawati la jinsia linamhusu.
 
Pole sana dada yangu, wanaume (japo sio wote ila ni wengi) sijui tumekula maharage ya wapi? Tumekuwa watu wa kuzalisha na kukimbia majukumu. Kina dada wanajitahidi kutulelea watoto Lakini choko choko haziishi. Nakushauri jitahidi kila unapoongea nae onyesha unamaanisha kile unachosema (hata kwa body language). Vinginevyo dawati la jinsia linamhusu.

Asante sana kwa ushauri mkuu nitaufanyia kazi
 
Kuwa serious na mambo yako usionyeshe kumjali kabisa, atatokea mlango alioingilia bila kuaga
 
Pole sana dada yangu, wanaume (japo sio wote ila ni wengi) sijui tumekula maharage ya wapi? Tumekuwa watu wa kuzalisha na kukimbia majukumu. Kina dada wanajitahidi kutulelea watoto Lakini choko choko haziishi. Nakushauri jitahidi kila unapoongea nae onyesha unamaanisha kile unachosema (hata kwa body language). Vinginevyo dawati la jinsia linamhusu.

maharage tuliyokula ni ya sauzi afrika
 
Back
Top Bottom