Kama hufanyi makosa unawasi wasi gani.
Huyo anaye kuitwa player ungeomba kamchezo naye basi :violin:
Usinilaumu kufikiria hayo hasa kwa tunavyosikia jinsi maisha ya huko yalivyo. Tunasikia huko hakuna wakati wa kupoteza kwa ajili ya kazi. Sasa unapotwambia kuwa wake watatu wa watu tayari wanakufuatilia bila shaka ipo nafasi ya kujitanua. Halafu haya mawakati unayokutana kutana na wenzako kiasi cha wanamama kukushobokea yanapatikana wapi, iwapo hakuna mataimu ya kutanua huko?
Wadada wengi makini hawapendi wanaume wa design yako; mimi mmoja wapo. Simshangai huyo dada aliyekuona player. Maana ni dream za wadada makini kuwa na private husband na si cha wote.
Mimi mume wangu kila mtu wa jinsia ya kike ambaye si ndugu yangu ananilalamikia kuwa anaringa (marafiki na ofisi mates wangu) kisa uwa anawachunia kama hawajuhi wakikutana mitaani. Unajua nawajibu vipi? Jamani mume wangu wala hana maringo. Kimoyo moyo nasema ongeza maringo mume wangu; na wala simwambii eti achangamkie rafiki zangu; wa kazi gani?
Nani anataka mwanaume anayemkenulia kila mtu???? Hata mimi ukinikenulia kenulia kila tunapokutana na kunichangamkia kupitiliza najua unanitaka.
Katika mwaka mmoja tu (june 2011 hadi July 2012) wake za watu watatu wamenifata kunitaka kimapenzi. Ninachotaka kujua ni kwa nini? ni kosa gani nifanyalo kiasi kuwa wake za watu wafikiri nawataka?
Wote nimewakwepa, lakini kinachonishangaza ni kwa nini hasa waache waume zao na kunifuata mimi? Wakati huo huo kuna mwanamke ambae yuko single na ananivutia mno lakini ananipiga chenga mwaka na nusu sasa na anasingizia eti ananihisi mimi ni player, jambo ambalo sio kweli kabisa!
Mmoja kati ya hawa wake za watu amefika hadi kudai kuwa anajua hasa kuwa ninamzimia, na ni woga tu ndio unaonizuia mimi kumfuata, na kwa sababu hiyo ndiyo yeye kaamua ku make the first move. Wote wamedai kuwa ucheshi wangu na tabasamu zangu niwaonapo njiani na sehemu za mikusanyiko ni ishara ya kuwa niko interested. Hilo sio kweli kwani hiyo ni hulka yangu kuwa mcheshi kwa kila nimjuae sio kwao wao tu, tabasamu kwangu ni jambo la kawaida. Daima huwa na dakika chache za kusimama kusalimiana na kuzungumza na niwajuao nikutanapo pahali popote pale.
Hivi ndugu zangu kuwa mcheshi na mchangamfu ni kosa? Huku ugenini ukianza kutokusalimia au kutotaka kujuana na watanzania wenzako ni hatari, kwani mbali ya wao kukuona kuwa unajipenda na kuwadharau wenzako pia nao watakutenga, jambo amablo sio jema hasa ukizingatia kuwa tuko mbali na familia zetu, binaadam mzima leo hujui kesho utaamkaje.
Hebu niambieni nifanyaje ili kuepukana na matatizo haya. Imeanza wake wa watu kuhisi nawataka, isije ikaja kufika waume zao kufikiria nawaibia wake zao.
umeshawahi kusikia msemo tembea uone mambo? basi ndio hayo sio kila unalosikia ni kweli, watu wanapenda kutia chumvi wanapohadithia maisha na mapirika ya walipo, hawasemi yote na huwezi kuyajua yote hadi pale ukienda mwenyewe na kuona kwa macho yako. Mfano ni huo ulosema kuwa hakuna wakati wa kupoteza kwa ajili ya kazi, sio kweli, mimi binafsi kwa mfano, nafanya kazi jumatatu hadi ijumaa saa tatu hadi kumi na moja na nusu, week end niko off, natumia siku hizo kupumzika, kufanya mambo yangu ya binafsi nyumbani, kwenda kuona mechi za mpira, kutembelea rafiki na jamaa pamoja na kuwasiliana na walio nyumbani. Mara chache huenda ofisini kama kuna jambo muhimu au kama niko nyuma katika moja ya kazi zangu. Sasa tu kwa kuwa wako watu wengine kwa sababu zao wenyewe hutafuta kazi za week end kuongezea na kazi ile ya jumatatu hadi ijumaa, hapo ndio tena wanapowaambia kuwa maisha ya nje hakuna kupumzika au kupoteza muda, lakini ukweli ni kuwa huo ni uamuzi wao na sio hali halisi ilivyo kwa kila mtu. Nadhani umenielewa kidogo.
Nimekuelewa sana na tukirudi kwenye mada yetu, mambo mawili yanajionyesha hapo. Una wakati wakutembelea jamaa wa kutosha na alhamdullilah una kazi soundly vitu hivi wakati mwengine vinachangia matatizo. Na ndio maana nikasema hapo awali kuwa makini na hizi ulizosema safari za kutembelea jamaa. Hebu jidai kuwa nawe uko bize kidogo ili kupunguza hayo mawasiliano. Wanawake watakutega hao ufikiri kuwa labda wanafatia tabasamu zako kumbe wana hesabu za baadae.
Wadada wengi makini hawapendi wanaume wa design yako; mimi mmoja wapo. Simshangai huyo dada aliyekuona player. Maana ni dream za wadada makini kuwa na private husband na si cha wote.
Mimi mume wangu kila mtu wa jinsia ya kike ambaye si ndugu yangu ananilalamikia kuwa anaringa (marafiki na ofisi mates wangu) kisa uwa anawachunia kama hawajuhi wakikutana mitaani. Unajua nawajibu vipi? Jamani mume wangu wala hana maringo. Kimoyo moyo nasema ongeza maringo mume wangu; na wala simwambii eti achangamkie rafiki zangu; wa kazi gani?
Nani anataka mwanaume anayemkenulia kila mtu???? Hata mimi ukinikenulia kenulia kila tunapokutana na kunichangamkia kupitiliza najua unanitaka.