BABA NEJAD
Member
- Nov 24, 2014
- 43
- 44
Habari za Weekend, natumai muwazima.
Mchana wa leo nimepigiwa simu na mdogo wangu ambae anasoma chuo kikuu cha mtakatifu Joseph kampasi ya Boko katika fani ya Medical Doctor (MD) . Katika maelezo yake alinambia Mkuu wa chuo amewaambia wanafunzi wote ambao wanasoma MD wenye alama D ya chemistry au biology, warudi nyumbani haijalishi wako mwaka wa ngapi kwa sababu wanaharibu sifa ya chuo hicho.
Walipotaka kupewa barua ya kusimamishwa masomo Mkuu wa chuo aligoma, akidai wao wanaangalia cheti tu na hawatatoa barua kwa mtu yeyote bali warudi nyumbani na chuo ndio mwisho.
Kinachoniumiza kichwa ni kuwa huyu jamaa anaingia mwaka wa pili sasa hv, na tangu mwaka jana tumejibana tukalipa ada zaid ya milioni 4 kwa sababu alipewa asilimia 80% ya mkopo kwa hyo kiasi kinachobaki tunamlipia. Vile vile TCU ndio ambao walimdahili na kumpangia chuo hicho na kusajiliwa akaanza masomo tangu mwaka jana, sasa hv wanabadilika kama kinyonga.
Naomba ushauri wenu wadau nifanyaje ili huyu jamaa aweze kuipata haki yake ya elimu au hata kurejeshewa kile ambacho tumelipa kwa mwaka mzima uliopita.
Ahsanteni, natanguliza shukrani zangu kwa ushauri wenu.
Mchana wa leo nimepigiwa simu na mdogo wangu ambae anasoma chuo kikuu cha mtakatifu Joseph kampasi ya Boko katika fani ya Medical Doctor (MD) . Katika maelezo yake alinambia Mkuu wa chuo amewaambia wanafunzi wote ambao wanasoma MD wenye alama D ya chemistry au biology, warudi nyumbani haijalishi wako mwaka wa ngapi kwa sababu wanaharibu sifa ya chuo hicho.
Walipotaka kupewa barua ya kusimamishwa masomo Mkuu wa chuo aligoma, akidai wao wanaangalia cheti tu na hawatatoa barua kwa mtu yeyote bali warudi nyumbani na chuo ndio mwisho.
Kinachoniumiza kichwa ni kuwa huyu jamaa anaingia mwaka wa pili sasa hv, na tangu mwaka jana tumejibana tukalipa ada zaid ya milioni 4 kwa sababu alipewa asilimia 80% ya mkopo kwa hyo kiasi kinachobaki tunamlipia. Vile vile TCU ndio ambao walimdahili na kumpangia chuo hicho na kusajiliwa akaanza masomo tangu mwaka jana, sasa hv wanabadilika kama kinyonga.
Naomba ushauri wenu wadau nifanyaje ili huyu jamaa aweze kuipata haki yake ya elimu au hata kurejeshewa kile ambacho tumelipa kwa mwaka mzima uliopita.
Ahsanteni, natanguliza shukrani zangu kwa ushauri wenu.
