Codrix
Senior Member
- May 18, 2019
- 192
- 219
Salamu kwenu.
Mimi kwa sasa ni mwanafunzi mwaka wa 3, chuo kimoja cha taasisi ya dini, kozi ya uuguzi ngazi ya diploma ikiwa imebaki kama miezi miwili nimalize chuo kuna changamoto zifuatazo.
1. Kupungukiwa ada ya masomo, mzazi uwezo wake wa kulipa ada umekuwa ni mgumu, hana pesa maana alipoteza kazi, yupo tu kwa sasa hivyo basi maisha ya chuoni yamesogea mpaka sasa kwa mazungumzo ya mzazi wangu na chuo kuwa wavumilie atalipa, anatafuta angalau mteja wa kiwanja chake auze apate pesa lakini inachelewa maana mteja hapatikani, naelekea mwisho hivyo wanataka kulipa kwanza pesa yao ndio nitafanya mtihani wa mwisho, isipolipwa sifanyi mtihani, nadaiwa 4.3m Jumla ya ada ni 9m kwa miaka mitatu ya diploma mzazi amefanikiwa kulipa 4.7m, ili kufanya mtihani wa mwisho.
MIPANGO YANGU.
1.Niendelee kusubiri uamuzi wa chuo juu ya hatima yangu, kama wataamua nifanye mtihani ama la, endapo nikiruhusiwa kufanya mitihani na kugraduate, nitafute kazi kwa kutumia leaving certificate, endapo nikifanikiwa kupata kazi nianze kupunguza deni, mfano nikilipwa laki 2,nitumie laki moja kujikimu na laki moja nitumie kulipa ada kwa kila mwezi mpaka nitakapomaliza deni hilo nikishirikiana na mzazi, nitakapomaliza ndipo nitapata cheti changu nikitumie kuomba nafasi serikalini.
2.Nisipofanikiwa kufanya mtihani, hapa sitakuwa na leaving certificate wala document yoyote ya kunitambulisha nimemaliza chuo, nitakuwa nimepoteza miaka mitatu, hivyo sitokuwa naajirika, itanibidi nirudi kufanya kazi za kibarua, biashara binafsi hapa nimepanga nitatafuta namna ya kuweza kupata pesa nirudi tena shule nikasome kwa pesa yangu.
3.Niondoke nyumbani nikatafute popote pesa ya kuweza kukamilisha malengo yangu, muda mwingine nawaza nisipofanikiwa kufanya mtihani au kupata kazi, nisahau kabisa kuhusu mambo ya shule.nifanye maisha mengine kabisa.
*Tumejaribu kutafuta wafadhili Hatujafanikiwa
*Kusoma pia imekuwa ni changamoto maana usumbufu chuoni ni mwingi kwa ajili ya pesa yao.
*Ndugu wenye uwezo baba akiongea nao wanasema hawana kitu
Samahani mimi sio mzuri katika uandishi, naombeni ushauri wakuu maana nahisi nipo njia panda.
Shukrani
Mimi kwa sasa ni mwanafunzi mwaka wa 3, chuo kimoja cha taasisi ya dini, kozi ya uuguzi ngazi ya diploma ikiwa imebaki kama miezi miwili nimalize chuo kuna changamoto zifuatazo.
1. Kupungukiwa ada ya masomo, mzazi uwezo wake wa kulipa ada umekuwa ni mgumu, hana pesa maana alipoteza kazi, yupo tu kwa sasa hivyo basi maisha ya chuoni yamesogea mpaka sasa kwa mazungumzo ya mzazi wangu na chuo kuwa wavumilie atalipa, anatafuta angalau mteja wa kiwanja chake auze apate pesa lakini inachelewa maana mteja hapatikani, naelekea mwisho hivyo wanataka kulipa kwanza pesa yao ndio nitafanya mtihani wa mwisho, isipolipwa sifanyi mtihani, nadaiwa 4.3m Jumla ya ada ni 9m kwa miaka mitatu ya diploma mzazi amefanikiwa kulipa 4.7m, ili kufanya mtihani wa mwisho.
MIPANGO YANGU.
1.Niendelee kusubiri uamuzi wa chuo juu ya hatima yangu, kama wataamua nifanye mtihani ama la, endapo nikiruhusiwa kufanya mitihani na kugraduate, nitafute kazi kwa kutumia leaving certificate, endapo nikifanikiwa kupata kazi nianze kupunguza deni, mfano nikilipwa laki 2,nitumie laki moja kujikimu na laki moja nitumie kulipa ada kwa kila mwezi mpaka nitakapomaliza deni hilo nikishirikiana na mzazi, nitakapomaliza ndipo nitapata cheti changu nikitumie kuomba nafasi serikalini.
2.Nisipofanikiwa kufanya mtihani, hapa sitakuwa na leaving certificate wala document yoyote ya kunitambulisha nimemaliza chuo, nitakuwa nimepoteza miaka mitatu, hivyo sitokuwa naajirika, itanibidi nirudi kufanya kazi za kibarua, biashara binafsi hapa nimepanga nitatafuta namna ya kuweza kupata pesa nirudi tena shule nikasome kwa pesa yangu.
3.Niondoke nyumbani nikatafute popote pesa ya kuweza kukamilisha malengo yangu, muda mwingine nawaza nisipofanikiwa kufanya mtihani au kupata kazi, nisahau kabisa kuhusu mambo ya shule.nifanye maisha mengine kabisa.
*Tumejaribu kutafuta wafadhili Hatujafanikiwa
*Kusoma pia imekuwa ni changamoto maana usumbufu chuoni ni mwingi kwa ajili ya pesa yao.
*Ndugu wenye uwezo baba akiongea nao wanasema hawana kitu
Samahani mimi sio mzuri katika uandishi, naombeni ushauri wakuu maana nahisi nipo njia panda.
Shukrani