Naomba ufafanuzi

mdesi

JF-Expert Member
Jul 18, 2013
1,349
2,086
Habari za humu wana jf, naomba nianze kwa kusema mimi ni si mfuasi wa ccm, naunga mkono upinzani sana tena mno.

Huwa napata wakati ngumu sana, na pengine leo nikasaidiwa kupata utatuzi kutoka kwa wadau humu ndani. Ni hivi, mh. Edward Ngoyai lowasa na Fredrick Sumaye, ambao waliamua kwa dhati kabisa kuachana na rangi ya kijani na kujiunga na makamanda kwa lengo la kuleta mabadiriko, ni jambo zuri na lakuungwa mkono na wapenda mabadiriko.
Kinacho nitatiza hawa jamaa sijawahi kuwaona wakiwa wamevaa magwanda ya chadema hata siku moja, ili hali wakati wakiwa ccm walikuwa na mashati, kofia na isitoshe hata siruali na viatu vya ccm. Inakuwaje huku hawataki kuvaa?

Au hawakupewa? Hawa jamaa huwa wananitia wasiwasi kuwa huenda wanatumiwa na ccm ili kuharibu nguvu ya upinzani, kimwili wapo chadema lakini kiakili na mioyo yao ipo Lumumba.

Ukikumbuka wadau halisi wa chama Dr. Slaa, Mbowe, Mnyika na wengine walikuwa hawaachi kuvaa nguo za chama hata siku moja kuonyesha mapenzi na imani ya chama chao.

My take, hawa jamaa walipo chadema kimwili wasiwe wanashirikishwa mipango nyeti ya chama na wasipate fursa kuzijua siri za chama. Vinginevyo tutajikuta mda ukikaribia wa kufanya uchaguzi watu wanarudi walokotoka wakiwa wanajua siri zote na mipango ya chama. Take my note wakuu I love oppositions!
 
kwani wakivaa ndio watakuwa na mapenzi mema na chama..?
waekeeni wachunguzi wawachunguze ili mjue mko nao kweli au dodoso tu.
jambo hili nililihisi toka 2015 alipohamia chadema,chadema lzm wawe waangalifu sana usikute walishaga tuma vibaraka kabla ya wenyewe kujiunga na chama hivyo wamekuja kutimiza lengo
 
heheee! alie kwambia nguo ni sign ya mapenzi mema na kitu Fulani alikudanganya wangapi wanavaa hayo majezi lakini wamejawa na usaliti na unafiki pia?
 
Back
Top Bottom