Naomba nisaidiwe juu ya hili

Naomba nisaidiwe juu ya hili

Ninaimani kuwa wapo wengi humbu ndani wanapenda kunisaidia kwa kunipa mkopo ila wanawasiwasi kwani nishaweka wazi kuwa sina dhamana,,

Naomba niweke maelezo haya kuonesha nia yangu ya uhitaji na uhakika kwa uaminifu wangu...

Nilimaliza darasa la saba mwaka 2002 pamoja na kufaulu ila ilishindikana kupata ada ya kujiunga na sekondari,
Nikawa mpole,nikaweka nia ya kusoma hivyo nikaanza kujifundisha kutengeneza sofa kwa rafiki angu hadi mwaka 2004 niliamua nianze kuhangaikie elimu,kwasababu bado hali ya kifedha haikua vizuri Nikawa nawatumia rafiki zangu ambao walikuwa shule,muda walipokuwa wanakutana kwaajili ya discussion nami nilihudhuria,na pia niliwaomba waliozidi kidato wakawa wananifundisha kwa malipo machache yasiyo zidi tsh.2000 kwa mada za biology na math pia tsh.500 hadi 1000 kwa mada za masomo mengine ya sanaa, nilijikakamua hadi nikapata ada ya usajili hivyo nilijisajili kwa ajili ya mitiani ya QT ktk kituo cha elimu ya watu wazima..

Mwaka 2005 nilifanya mtihani QT na nilifanikiwa kufaulu,zoezi likaendelea la kujisomea huku natafuta ada ya mtihani,nikaja kufanikiwa kufanya mtihani mwaka 2008,,,matokeo hayakua mazuri ila nilipata cheti.

Nilizidi kuweka nia ya kufika mbele zaidi kielimu na kimaisha pia,nilifanya mpango kunajamaa flani,nilikuwa simjui hapo mwanzo,nilimtengenezea sofa akapenda kazi yangu na akawa rafiki yangu...nilijaribu kumuomba anikopeshe kiasi cha pesa,nashukuru alinikopesha laki 5 bila riba wala masharti mazito zaidi ni deadline ya marejesho...

Nilifanya biashara na nilirejesha kabla ya deadline,...nilimake pesa kwa mwaka mzima 2009-2010,,,Nikaamua niingie college mwaka 2011,january-december,nashukuru nikasoma bila matata ila nilifulia ktk biashara kwaajili ya matumizi na malipo ya college....nikapata cheti na mwaka 2012 nikaanza michakato ya kutafuta kazi/kibarua hadi leo bila mafanikio yeyote.

LENGO

Nipate pesa,nifanye biashara ili nijiendeleze kielimu kwani ninamalengo ya kupata japo degree.

Wapendwa,kuhusu dhamana ya vitu:
Ninaishi dar es salaam-magomeni (nimepanga),,,ndani nina kitanda,tv na deki,feni na vyombo vidogo vidogo...thamani yake ni kama laki 5 hivi

Je, kwa hivi vitu ninaweza kupatia mkopo?
 
Hongera kaka, umetumia akili ya ziada kuonesha njia ya kujikwamua na hili janga la umaskini....
 
Bado sijafanikiwa......natarajia msaada toka kwenu wadau.
 
Katika pilikapilika zangu za kutafuta mtaji wa pesa kwa ajili ya kufanyia biashara,nimeenda katika taasisi fulani ya kifedha na wakanipa vigezo vyao kuwa inabidi niwe na TIN namba ya biashara na leseni ya biashara hapo ndipo nitafikiriwa kupewa mkopo (mean hupati mkopo hadi uwe na biashara)

Kwakuwa kunabidhaa nilisha tengeneza na shida nipate frem ili niuze bidhaa zangu, nikaamua niende TRA kwaajili ya kupata hiyo TIN,wakanipa fomu ili nijaze, na sasa nisha kamilisha kujaza ,kesho tar 6/march inabidi nikachukue TIN

Shida itakuwa kupata leseni kwani nimeambiwa inagharim kama laki 2 wakati hapanilipo nina elfu tano tu ya kula, sijui itakuwaje...

Naombeni Ushauri na mawazo yenu wadau kwani naamini SIWEZI BILA NYIE.
 
Back
Top Bottom