makua
JF-Expert Member
- Dec 9, 2013
- 208
- 40
Habari zenu wanajamvi!
Mimi ni kijana (mvulana), ninaelimu yangu ya kuungaunga, nimegraduate mwaka 2011 kozi ya utunzaji kumbukumbu ngazi ya cheti (certificate of records management)
Nimefanya kazi kwa ujitolea kama mtunza kumbukumbu msaidizi kwa mda wa miezi kumi yaani january-october, 2012
Baada ya kuona maisha yanazidi kuwa magumu nikaamua niache kazi kwani nilikuwa nafanya pasi kulipwa hata kidogo, ndipo nikaanza kutengeneza sofa, nilikuwa nafanya katika ofisi ya mtu kwa makubaliano anilipe kila kazi nayofanya, mwanzoni tulienda vizuri ila mwishoni pakawa na mabadiliko, katika kazi tano,ananilipa mbili zingine halipi, nikaamua niache.
Nikawa nahamasisha baadhi ya vijana ambao ni mafundi wa sofa ili tuungane na tufungue ofisi kubwa ambayo itakuwa miliki yetu hivyo tutaepukana na manyanyaso ya mabosi, ila waliishia kuitikia bila utekelezaji...
Kwa sasa lengo langu ni kufungua ofisi yangu ya kutengeneza sofa na kuziuza, natumaini nikifanikiwa basi nitatengeneza ajira zisizopungua tatu. (mafundi wawili na muuzaji mmoja)
OMBI
1: Kwa sasa naomba nipate kibarua chochote chenye kunipatia kipato ambacho nitaweza kufikia malengo yangu.
2: Nimetembelea baadhi ya taasisi za kifedha ili nipate mkopo ila nimeshindwa kupata vigezo vya kukopa.
Kwahiyo kama kuna mtu ambaye yukotayari kunisapoti kivyovyote basi nahitaji msaada.
3: Kama kuna mafundi wa sofa au wenye uhitaji wa fundi humu basi naomba kampani yenu tuwepamoja ili maisha yaendelee..nipo tayari niishi mahali popote duniani ilimradi maisha yaende.
Naishi Dar es salaam, Magomeni.
Nawasilisha
Mimi ni kijana (mvulana), ninaelimu yangu ya kuungaunga, nimegraduate mwaka 2011 kozi ya utunzaji kumbukumbu ngazi ya cheti (certificate of records management)
Nimefanya kazi kwa ujitolea kama mtunza kumbukumbu msaidizi kwa mda wa miezi kumi yaani january-october, 2012
Baada ya kuona maisha yanazidi kuwa magumu nikaamua niache kazi kwani nilikuwa nafanya pasi kulipwa hata kidogo, ndipo nikaanza kutengeneza sofa, nilikuwa nafanya katika ofisi ya mtu kwa makubaliano anilipe kila kazi nayofanya, mwanzoni tulienda vizuri ila mwishoni pakawa na mabadiliko, katika kazi tano,ananilipa mbili zingine halipi, nikaamua niache.
Nikawa nahamasisha baadhi ya vijana ambao ni mafundi wa sofa ili tuungane na tufungue ofisi kubwa ambayo itakuwa miliki yetu hivyo tutaepukana na manyanyaso ya mabosi, ila waliishia kuitikia bila utekelezaji...
Kwa sasa lengo langu ni kufungua ofisi yangu ya kutengeneza sofa na kuziuza, natumaini nikifanikiwa basi nitatengeneza ajira zisizopungua tatu. (mafundi wawili na muuzaji mmoja)
OMBI
1: Kwa sasa naomba nipate kibarua chochote chenye kunipatia kipato ambacho nitaweza kufikia malengo yangu.
2: Nimetembelea baadhi ya taasisi za kifedha ili nipate mkopo ila nimeshindwa kupata vigezo vya kukopa.
Kwahiyo kama kuna mtu ambaye yukotayari kunisapoti kivyovyote basi nahitaji msaada.
3: Kama kuna mafundi wa sofa au wenye uhitaji wa fundi humu basi naomba kampani yenu tuwepamoja ili maisha yaendelee..nipo tayari niishi mahali popote duniani ilimradi maisha yaende.
Naishi Dar es salaam, Magomeni.
Nawasilisha