kwa wale wanaozani mwanamke ni dhaifu, itakua ni msemo tu!! juzi tu mtaani kwetu bosi mmoja na kiongozi wa serikari halijikuta kwenye wakati mgumu baada ya kuleta nyumbani mtoto wake wa kike aliezaa na binti mmoja mtaa wa pili, sasa ana miaka mitano huku akitoa kauri .....KITANDA HAKIZAI HARAMU na akalazimisha mtoto lazima akae home kwake. sasa kilichonifanya niamini kuwa wanawake wana nguvu zaidi ya wanaume kwa kwa kuonesha emotional maturity ni pale alipomueleza mumewe hakuna taabu ila na wewe uwe mvumilivu.......... mimi kesho ntamleta mtoto wangu niliezaa na jamaa mmoja pindi nilipokuwa shule( sekondari), haikuwa hajizi kweli kesho yake wife yule kaja na mtoto wa kike pia umri 15yrs na alipoulizwa ulizaa na nani akataja jamaa mmoja mtaani kwetu ambae kitaa pote wanamjua ni fataki mwanzo mwisho........ jamaa huyo kuskia hivyo alipatwa na mshituko na kupoteza fahamu, thanks God tunaelezwa badae alizinduka hila hajaweza hata kutoka ndani kwa mda wa wiki sasa. SASA NIMEELEWA WANAUME NI DHAIFU KULIKO WANAWAKE. mkuki kwa nguruwe kwa binadamu mchungu.:angry::angry::angry: