Naomba nifahamishwe kuhusu cheti cha ndoa

Naomba nifahamishwe kuhusu cheti cha ndoa

shegacool2015

JF-Expert Member
Joined
Feb 6, 2014
Posts
394
Reaction score
133
Habari za usiku ndugu zangu...naomba niulize, hivi vyeti vya ndoa vizovyotolea na Bakwata vinafahamika serikalini? Au kuna vingine vyeti tofauti na hivyo?
 
Habari za usiku ndugu zangu...naomba niulize, hivi vyeti vya ndoa vizovyotolea na Bakwata vinafahamika serikalini? Au kuna vingine vyeti tofauti na hivyo?

Ndoa inafugwa kwa sheria za nchi ila dini ni wakala wa ufungishaji ndoa vyeti vyote vinatoka serekalini hivyo ni ndoa halali.
 
Ndoa inafugwa kwa sheria za nchi ila dini ni wakala wa ufungishaji ndoa vyeti vyote vinatoka serekalini hivyo ni ndoa halali.

Asante Sana, kwahiyoo hua hakuna vyeti vya serekalini?
 
vyeti vyote ni vya serekali uwe umefunga kanisani msiktini au bomani cheti ni komoja na vinatoka serekalini ila dini uwawanatoa hati ya ziada kuonyesha umefunga kwa taratibu ya dini fulani nadhani umenielewa.
 
Habari za usiku ndugu zangu...naomba niulize, hivi vyeti vya ndoa vizovyotolea na Bakwata vinafahamika serikalini? Au kuna vingine vyeti tofauti na hivyo?

Mkuu kwani we unataka cheti cha wapi.

Ongea vizuri.
 
Vyeti vya serikalini vipo!! Ukiachana na vyeti vinavyotolewa vya kidini..
 
hivyo vya dini haramu cheti kiko kimoja ukifunga msikitini kimoja ....kanisani kimoja...kingine ni cha serikalini hiki wanaita ...pale magomeni kwa watu wa upande wetu kama unaona miyeyusho unaenda na msimamizi na mpiga picha unaulizwa maswali unakamata cheti chako
 
najiuliza hivi ukioa mke wa

2

3

4

nao wanapewa vyeti???
 
Cheti ni kimoja ila ndugu yangu hicho cheti ni dhuluma ya mali zako mkishakisaini ujue mali ni zenu
 
Mamlaka pekee inayotoa vyeti vya ndoa ni serikali kwa mujibu wa sheria ya ndoya ya mwaka 1971. Bakwata kwa mujibu wa sheria hii ni baraza la usuluhishi la kidini inapotokea mgogoro wa ndoa. Vyeti vya bakwata havina nguvu yoyote kisheria ni utambulisho wa kidini kama vilivyo vyeti vya ubatizo kwa wakatoliki. Sheikh aliye na kibali cha kufungisha ndoa anapaswa kutoa cheti cha ndoa cha kiserikali
 
Mamlaka pekee inayotoa vyeti vya ndoa ni serikali kwa mujibu wa sheria ya ndoya ya mwaka 1971. Bakwata kwa mujibu wa sheria hii ni baraza la usuluhishi la kidini inapotokea mgogoro wa ndoa. Vyeti vya bakwata havina nguvu yoyote kisheria ni utambulisho wa kidini kama vilivyo vyeti vya ubatizo kwa wakatoliki. Sheikh aliye na kibali cha kufungisha ndoa anapaswa kutoa cheti cha ndoa cha kiserikali

Mkuu, kwa hioo Kama nataka cheti kinachotsmbuliwa kisheria inabidi nitafute cha serekali? Taratibu zakukipata ziko VP??
 
Mkuu, kwa hioo Kama nataka cheti kinachotsmbuliwa kisheria inabidi nitafute cha serekali? Taratibu zakukipata ziko VP??

wafungisha ndoa wote wawe mapadri au masheikh wako registered kwa dc husika. Wanapaswa wawe na vitabu vya vyeti vya ndoa. kama umefunga hukupata cha serikali beba hicho cha bakwata mkafanye formality kwa dc. dc ndio mkuu wa wilaya.
 
asante sana, kwahiyoo hua hakuna vyeti vya serekalini?

vyeti vyote VYA NDOA NI VYA serikali ,hao wote ni mawakala wanaenda kuchukua serikalin,i awe shehe ,padri au mchungaji wote ni mawakala wa serikali
 
Ukijua mana ya ndoa nini na ukajitambua cheti ni ushetani,na hakidhihirishi agano kwa wakristu wataungana nami hakuna mahali panapruhusu certified mariage
 
Back
Top Bottom