Mkuu familia yenu sio ya kipato cha chini kama ilivyo kwa watanzania wengi. Mmeweza kusoma Loyola na kicha ya kuwa na option nyingi hapa nchini mkampeleka China.Hapa inakua ngumu watu kutoa msaada kwanza hawana uhakika wa maelezo mana hayana vithibitisho, pili Tanzania tuna familia pana( uncles, aunts etc)haujasema nyie kama wanafamilia mmejichanga kufikia wapi na mmekwama wapi. Suala la kupostpone masomo kwa elimu ya chuo linafanyika vyuo vingi ulimwenguni, mambo yakiwa magumu unamute kwa taarifa rasmi chuoni then yakikaa sawa unarudi.
Kinachofanya watu watulie tulii ni mentality mlizonazo familia nzima kwa ujumla. Kuanzia mama mpaka watoto. Mentality yenyewe ni kwamba mnataka kila mnachokianzisha basi kifike mwisho no matter what. Lakini kaeni mkijua kwamba maisha hayako hivyo. Kuna ups & downs ambazo mnatakiwa mkubaliane nazo pia.naelewa concern yako kaka,,,ila labda nikuelezee vizuri,,,tumesoma loyola kwa misaada ya ndugu,,,mfano mimi nimesomeshwa kwa msaada mkubwa wa bibi yangu mzaa mama,,na hao wadogo zangu wamesomeshwa na mama ila bibi nae alikuwa akiweka msaada wake,,ila licha ya hivyo mimi nimemaliza pale loyola na deni la 1.5m na mpaka leo cheti changu cha form 6 kipo pale kimeshikiliwa....usione ilo jina loyola tu kaka ukadhani tumetokea familia yenye kipato,,,hapana...kuanzia form one mpaka form six,,,mimi na wadogo zangu tumekuwa watu wakutolewa nje kwaajili ya ada,,,tumekuwa wakutolewa darasani na kurudishwa nyumbani...nakumbuka assistant head master alikuwa akija darasani kutoa watu wanaodaiwa ada,,lazima jina langu liwepo,,na nikifika ofisini nakutana na wadogo zangu then tunarudishwa nyumbani...tumemaliza shule kwa shida sana....Huyo wa china alienda huko baada ya kukosa medical school hapa bongo,,,her target ilikuwa muhas au bugando ila hakufanikiwa kupata,,,mama na bibi wakapambana mpaka mwisho ili mtoto afikie ndoto zake na kumpeleka China...na ata alivyoenda huko china,,bado mama amepambana sana,,mno yanii...ila round hii ambayo ndo ya mwisho imetukuta pabaya sana,,,tumejaribu kupambana ila mambo hayaendi,,since September ilibidi tuwe tumelipa ada yake ila mpaka sasa bila bila...
Hata mwezi huna, na post ya kwanzakizinga cha millioni 6, jf imevamiwa,kwa kweli.
Kinachofanya watu watulie tulii ni mentality mlizonazo familia nzima kwa ujumla. Kuanzia mama mpaka watoto. Mentality yenyewe ni kwamba mnataka kila mnachokianzisha basi kifike mwisho no matter what. Lakini kaeni mkijua kwamba maisha hayako hivyo. Kuna ups & downs ambazo mnatakiwa mkubaliane nazo pia.
Swali kubwa tunalojiuliza hapa ni kwamba ina maana mama mtu hakupata experience kwako? Kwa nini alirudia makosa yaleyale kwa wadogo zako ilihali wewe ilishindikana tena ukiwa mmoja? Mbaya zaidi akakubali kumpeleka mtoto mmoja nje ya nchi. Nauli ya kwenda tuu inatosha ada ya mwaka mzima kwenye vyuo vya hapa bongo.
Naomba usituelewe vibaya mkuu, mnachotakiwa kujua ni kwamba tupo wengi ambao tumesoma fani tusizozipenda sababu ya hali halisi ya uchumi, tupo tuliosoma kozi za miaka 3 kwa miaka 4/5/6 kwa sababu mbalimbali ikiwamo mkwamo wa uchumi n.k n.k. Kinachowaudhi watu hapa ni kwa nini nyie hamtaki kukubali ups & downs? Kwa nini mnataka muende one way forward wakati mnajua hali halisi ya uchumi wenu? Why you are forcing things?
Ujue kusoma sio emergency! Kwamba eti asipomaliza mwaka huu atakufa. Hapana. Na kwa nionavyo mna uwezo wa kupostpone masomo yake kisha mjipange hata mwakani akamalizie. Yani mkikubali kuenda taratibu mtaweza kuhandle kila kitu vizuri tuu, shida yenu hasa ipo kwenye uvumilivu. Hamtaki kuwa wavumilivu.
Mimi nakushauri kwa mara nyingine tena pelekeni mambo taratibu kulingana na nafasi na uwezo wenu. Lakini mkifosi sana nyumba nzima mnaweza mkadata.
Kama kuna mahali nimekukwaza nisamehe mkuu.