Strong ladg
JF-Expert Member
- Jul 15, 2021
- 407
- 1,054
Ndugu wataalamu, kuna mdogo wangu yuko chuo anaanzisha biashara ya kuuza vitu mtandaoni. Kila kitu tayari hadi usajili wa Brela (kasajili jina la biashara). Ishu ipo kwenye masuala ya TRA, TIN Number n.k. Kwa uelewa wangu mdogo ni kuwa mtu ambaye mauzo yake kwa mwaka ni chini ya milioni 4 halipi kodi, pia mdogo wangu hatarajii kwa sasa kuweza kuingiza milioni 4 kwa mwaka.
1. Je atatakiwa kulipa kodi? ( Labda sheria zimebadilishwa)
2. Anavyoenda TRA ajipange vipi kwa usalama wa biashara yake inayoanza?
Ushauri, ukosoaji, maoni yanakaribishwa. Asanteni
1. Je atatakiwa kulipa kodi? ( Labda sheria zimebadilishwa)
2. Anavyoenda TRA ajipange vipi kwa usalama wa biashara yake inayoanza?
Ushauri, ukosoaji, maoni yanakaribishwa. Asanteni