Naomba mke wangu akipata mimba asiwe hivi...

Uyapokee yote yatakayokupata,hata ukiaibishwa uwe na uvumilivu,siku hizi wanawake wenye mimba wanataka Burger au Pizza na inatakiwa isindikizwe na Savannah na sio kula udongo tena ,hizi ndoa za masister duu zina karaha. Hizi mimba mbona zitatutoa roho na karaha inakuja pale mimba ni yako ila anasema mimba inampenda mwanaume mwingine harafu inamchukia muhusika mwenye mimba hizi swagger ni hatari sana.

Mwanamke huanza deko pale anapojua mume/mpenzi wake anapenda watoto na yeye ndio ame conceive mimba yake ya kwanza,hapo lazima uwe na crate la Savannah na Burger Hut zote lazima wakujue sababu mimba haitaki ugali wala dagaa ila mimba inataka Burger na Pizza tu, tena iwe imeambatana na savvanah ,hakika dunia hadaa ulimwengu shujaa.

Siku zote uzi hufuata sindano na sindano haiwezi fuata uzi kwa maana hii hakuna jinsi inabidi ukubali kununua piza na Burger na uridhie mimba yako yatakiwa impende mwanaume mwenzio ambaye hakushiriki kwenye utunzi wa mimba na bila kusahau tu savanna tuwili kila siku, if you’re man enough to knock her up then, you better be man enough to support the child.

#GedsellianTz
Hapo likizo kwa mama yake inamhusu..
 
Kuweni makini wajawazito wenu wasile machips, makitimoto, mayai nahayo mapiza yenu kuna hatari ya kuzaa watoto wenye vichwa vikubwa ndani kukajaa maji, watoto vikaza bichwa kubwa ubongo wa mende, be warned.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom