Naomba Mbwana Samatta apewe mtaa Dodoma

Naomba Mbwana Samatta apewe mtaa Dodoma

mchanga mchanga

Senior Member
Joined
Jun 13, 2017
Posts
115
Reaction score
82
Kwa heshima na taadhima nawaomba wakuu wangu wa serikali ya awamu ya 5 mfikirie kumpatia kijana wetu Mbwana Ally Samatta mtaa katika jiji la Dodoma, kutokana na mchango wake mkubwa katika soka letu la Tanzania.

Samatta ni balozi wetu pekee kwenye mashindano ya UEFA, michuano mikubwa barani Ulaya. Ameitangaza vyema sana nchi yetu.

Ni Mtanzania pekee ambae ameweza kushiriki michuano hii na kufanikiwa kufunga magoli matatu. Na vilevile ni mchezaji tegemeo wa timu yetu ya Tanzania.

Naamini serikali sikivu itapokea ombi langu.
 
Mbwwna Samatta ameanza kupata changamoto kubwa pale Genk kwani ujio wa Koch's mpya. H. Wolf toka Ujerumani umeanza kumfanya awe chaguo LA pili (kuanzia bench) katika ushambuliaji. Leo ni mechi ya pili namwona Mbwana Samatta akianzia benchi dhidi cgaguo LA kwanza kwa sasa .P. Unuachu toka Nigeria.
 
Kwa heshima na taadhima nawaomba wakuu wangu wa serikali ya awamu ya 5 mfikirie kumpatia kijana wetu Mbwana Ally Samatta mtaa katika jiji la Dodoma, kutokana na mchango wake mkubwa katika soka letu la Tanzania.

Samatta ni balozi wetu pekee kwenye mashindano ya UEFA, michuano mikubwa barani Ulaya. Ameitangaza vyema sana nchi yetu.

Ni Mtanzania pekee ambae ameweza kushiriki michuano hii na kufanikiwa kufunga magoli matatu. Na vilevile ni mchezaji tegemeo wa timu yetu ya Tanzania.

Naamini serikali sikivu itapokea ombi langu.
Kwa lipi la kunufaisha nchi?
 
Yaan Tumpe mtaa Samata kabla ya Mzee Philip Japhet Mangula?

Unajua role ya huyu Mzee kwa Nchi?

Samata kafanya nini cha maana kwa nchi?
 
Back
Top Bottom