Naomba kuelimishwa kuhusu Shudhuly

ومن لم يعرف تفسير الحديث ويبلغه عقله، فقد كفي ذلك وأحكم له، فعليه الإيمان به والتسليم له.
"...na yeyote ambaye hajaijua tafsiri ya hadithi na imefikia ukomo akili yake, basi hakuna shaka ameshatoshelezewa hilo na ameshahukumiliwa, basi ni juu yake kuamini hadithi hiyo na kujisalimisha kwake....."

usuulu ssunnah ya al imaam ahmad
hayo maneno yaponwazi kwamba ambaye hajaelewa tafsiri ya hadithi,kwa maana wapo wengine wataelewa mbona maneno yako wazi ?

Wewe kama hauelewi tafsiri ya hadithi fulani hautakiwi kulazimisha wenzio nao ati wawe hawajaelewa kama wewe,hiyo haipo,wapo watu wana ufahamu wa mbali.

Mfano nakupa : kuna mwanachuoni alipoulizwa maana ya hadithi "dunia ni jela ya muumini na pepo ya kafiri"

yule mwanachuoni akajibu "dunia ni jela ya muumini ukilinganisha na peponi kulivyo,na ni pepo ya kafiri ukilinganisha na motoni kulivyo.

hapo ndio utajionea kwamba okaay kumbe kuna ambao hawakuelewa hiyo hadithi mpaka wakamuuliza huyo mwanachuoni na akawajibu.

hivyo Hakuna sehemu pameandikwa kwamba hatutakiwi kuzielewa hadithi kwa akili zetu,huo ni ufahamu wako ndugu yangu.
au andiko husika liko kadha wewe ukasema hapana sio hivyo kwasababu hii haiingii akilini,
Wanaopinga wanapinga ufahamu wenu na sio maandiko,ebu elewa hii hoja kwanza kwamba WALE MNAOWASHUTUMU KUPINGA DALILI UHALISIA NI KWAMBA WANAPINGA UFAHAMU WENU,ILA NYINYI MNAWABAMBIKIA KWAMBA WANAPINGA DAILI NA HIYO NI DHULMA KWA NDUGU ZENU.
yaani mto nile chanzo si kipo hapo ziwa nyanza? mbinguni tena? hili hapana.
Hii ni mifano yako iliyotoka kwako ili uipe nguvu hoja yako na wala haijatoka kwa hao unaowasema kwamba wanapinga dalili.

Uadilifu ni kuweka mifano ambayo kwa hakika ni ya uhalisia kutoka kwa watu unaowapa tuhuma hizo na sio vinginevyo.
hadithi ya jaabir ibn sulaym Allah amridhie, kwamba mtume swala na salaam ziwe juu yake amesema: "jiepushe na kurefusha nguo chini ya kongo mbili, kwasababu kufanya hivyo ni katika kiburi, na hakika Allah hapendi kiburi."hadithi
HAidhi hii haipingi hadithi zingine kama ile isemayo "mwenye iuburuza nguo kwa kiburi.."

Hivyo zipo hadithi kadhaa ambazo zinaashiria kiburi mpaka sahaba mmoja alipomuambia mtume kwamba yeye kikoi chake kinaburuza mtume akamuambia kwamba "WEWE HAUFANYI KWA KIBURI".

Kwa maana kiburi na majivuno ndio kunasababisha uharamu wa jambo hilo.

Unapotoa hadithi nyingine bado haujaivunja hadithi nyingine kwa sbaabu zote zipo katika vitabu vya hadithi.

Hivyo basi suala hili linabaki kuwa pana kinyume na mnavyolilazimisha ndugu zetu nyie wa kisalafi kwamba iwe haramu wakati hadithi zimekuja kwa lafdhi tofauti.
 
Yale sio mapepo. Wanasoma quran kwa mizuka na kucheza na kufurahi.

Utaniambia wanaocheza makanisani nao ni mapepo?
Hahaha!

Sheikh! Uislamu haujakataza kucheza. Bali unachezaje? Hata katika makabila ya waarabu kuna tamaduni za kucheza traditional dance na hazina mashaka zimeruhusiwa kwenye dini.

Mfano Saudia wanacheza vizuri wananesa nesa na mapanga hivi! Iraq kama wanashikana mikono hivi.

Swali ni unachezaje? Mwanamke ameruhusiwa kucheza lakini imma akiwa na wanawake wenzake au akiwa na mume wake.

Mwanaume umeruhusiwa kucheza mfano ndiyo kama huo wa ngoma za kiutamaduni hata Cristiano Ronaldo alicheza hiyo na upanga. Lakini hauruhusiwi unaanza kucheza mapigo ya mwanamke. Hii haipo!

Kwa hiyo kama unamdhukuru Allah na unajisikia raha wewe cheza kwa kunesa vile. Ni kama mwengine akisoma Qur'an raha inampanda mpaka ananesa nesa.
 
Nilichokisema mimi:
"Mchoraji picha za aina hizo, mchongaji masanamu/vinyago, mpiga picha za kawaida/video ni ktk makundi ya watu watakaopata adhabu kali sana tena sana na iumizayo."

Alichoniambia mimi safuher nikifanye:
"Mkuu tuoaomba dalili ambayo imeainisha kama hivi ambavyo umeainisha wewe."

Jibu: Sina dalili iliyoainisha "exactly ' kama hivi ambavyo nimeanisha bali nimetumia akili ktk kulitolea ufafanuzi suala hili linalohusiana na mapicha. Hakika ktk Quran na Sunnah hakuna mahali imetajwa video kwa mfano. Mimi nilichofanya ni ufafanuzi tu.
 
nimetumia akili ktk kulitolea ufafanuzi suala hili linalohusiana na mapicha.
kwamba Mtume ashindwe kufafanua jambo kisha uje kulifafanua wewe kweli kaka ?
mpiga picha za kawaida/video ni ktk makundi ya watu watakaopata adhabu kali sana tena sana na iumizayo."
IMaamu al fauzan mpaka leo anapiga picha kule saudia na anarekodi video,ibn baazi naye alifanya hivyo,ibn uthaymen naye alifanya hivyo na maulamaa wengine wakubwa tu..

Jee hawa nao hawakuelewa hiyo hadithi ama ni matamanio yao ya nafsi au nao ni wapinga dalili waziwazi ?
 
Akhy. Picha za viumbe vyenye roho ktk binadamu na wanyama ni haramu kaka. Mchoraji picha za aina hizo, mchongaji masanamu/vinyago, mpiga picha za kawaida/video ni ktk makundi ya watu watakaopata adhabu kali sana tena sana na iumizayo.
Lakini pia, yule anayening'iniza picha hizo ukutani au kuvaa ktk nguo, au mapazia/mazulia na mfano wa hayo pia atapata adhabu kali siku ya kiama. Na mapicha hayo ukiyaweka ndani ya nyumba basi tambua kuwa malaika wema hawaingii ndani ya nyumba yk.
Aidha ktk hili kuna mlango wa dharura kutokana na sheria zilizowekwa na serikali. Mfano, kwa matumizi ya passport, vitambulisho na mfano wa hayo.
Elimu kama hizi utazipata ktk madrassa za Masalafi pekee.
Utakuta watu wanapiga mapicha/mavideo ndani ya Misikiti. Utakuta ndani ya Misikiti kuna poster zina picha za viumbe vyenye roho. Haya ni mambo ya maasi makubwa ktk Uislam. Allah awaongoze wote wenye kufanya matendo haya maovu kabisa.
Mwisho, yeyote mwenye kutaka dalili na ushahidi juu ya jambo hili basi awasiliane nami Whatsapp 0688999006. Ninaheshimu privacy za watu.
Miongoni mwa Faida utakayoipata kupitia link nitakayokupaia:
1. Utapata elimu sahihi kupitia Quran na Sunnah.
2. Masheikh wetu na Maduat wanatumia AKILI kubwa kufikisha Da,wah kwa lengo la kujenga ufahamu kamili kwa Muislamu yyt.
Unatumia hela?
 
Akina ibn uthaymeen , akina ibn baazi ,akina fauzani ambao wnaonekana mpaka leo kwenye tv wasione uharamu huo ati waje kuona hawa watanzania ?

Maulamaa mnaojinasibu kuwafuata mkuu wao wanaonekana kwenye picha na video.

Ni ipi aya ama hadithi iliyosema kwamba uharamu wa picha ni kwa watu na wanyama tu ?
Kauli Ya Shaykh Ibn Uthaymiyn Kuhusu Maoni Yake Kuhusu Suala La Kupiga Picha.

Sun 9 Dhul Qidah 1436AH, Aug 23 2015

بِسْمِ اللهِ الرَّحْمٰنِ الرَّحِيْمِ
Kutoka kwa Muhammad bin Salih al-Uthaymiyn kwenda kwa ndugu yake mtukufu Sheikh…Allah amuhifadhi na amjaalie kutokana na Wachamungu, kutoka kwa washirika wake wema, na kundi lake lililofaulu. Ameen

Kuhusu yale yafuatayo:

“…Na hayo uliyoyabainisha, Mwenyezi Mungu akulinde kutokana na kurudiwa jibu langu kwa ajili ya kuruhusiwa kwa picha zilizopigwa na kamera: basi nitakujulisha ndugu yangu kwamba sikuruhusu kupiga picha (nia ya picha ni ambayo ina roho kutoka kwa wanadamu na wengine) isipokuwa kwa lazima au haja, kama: uraia, leseni, kuanzisha haki na kama.

Ama kupiga picha kwa ajili ya heshima, kumbukumbu, au kujifurahisha kwa kuzitazama, basi sikuruhusu hilo iwe ni masanamu au picha zilizotengenezwa kwa mkono au mashine kutokana na ujumla wa kauli ya Mtume swallallahu alayhi wa sallam:

“لا تدخل الملائكة بيتاً فيه صورة”

"Malaika hawaingii katika nyumba ambayo ndani yake kuna sanamu."

Malaika hawataingia kwenye nyumba ambayo ina picha ndani yake

Na sijaacha kutoa hukumu kwa hilo na kumuamuru mwenye picha ya kumbukumbu aiharibu. Na mara nyingi mimi ni mkali ikiwa ni picha ya mtu aliyekufa.

Ama picha za vitu vyenye nafsi kama binadamu au vingine visivyokuwa hivyo, basi hakuna shaka katika kuharamishwa kwake na ni katika madhambi makubwa kutokana na uthibitisho wa kumlaani mtendaji kwa ulimi wa Mtume (Swalla Allaahu alayhi wa aalihi wa sallam). Hii inaonekana katika kile ambacho ni sanamu au kilichofanywa kwa mkono. Ama kamera inayotoa picha na hakuna hatua kutoka kwa mpiga picha ya kuchora uso au maeneo ya mwili, basi ikiwa picha itazalishwa kwa ajili kumbukumbu na madhumuni kama hayo ambayo picha hairuhusiwi kupigwa, kisha kuizalisha kwa kamera ni marufuku kwa makatazo ya njia hiyo. Ikiwa picha inatolewa kwa umuhimu au haja, basi hakuna madhara.

Hii ndio hitimisho la maoni yangu katika suala hili. Basi ikiwa ni sahihi basi ni kutoka kwa Mwenyezi Mungu na Yeye ndiye mwenye kusifiwa kwa neema. Ikiwa sio sahihi, basi ni kutokana na mapungufu yangu. Ninamuomba Allah anisamehe kwa hilo na aniongoze kwenye yaliyo sahihi. Assalamu Alaykum wa Rahmatullahi wa Barakatuhu”

[Majmuu' al-Fatwa wa Rasaail (2/287)
 
Kauli Ya Shaykh Ibn Uthaymiyn Kuhusu Maoni Yake Kuhusu Suala La Kupiga Picha.

Sun 9 Dhul Qidah 1436AH, Aug 23 2015

بِسْمِ اللهِ الرَّحْمٰنِ الرَّحِيْمِ
Kutoka kwa Muhammad bin Salih al-Uthaymiyn kwenda kwa ndugu yake mtukufu Sheikh…Allah amuhifadhi na amjaalie kutokana na Wachamungu, kutoka kwa washirika wake wema, na kundi lake lililofaulu. Ameen

Kuhusu yale yafuatayo:

“…Na hayo uliyoyabainisha, Mwenyezi Mungu akulinde kutokana na kurudiwa jibu langu kwa ajili ya kuruhusiwa kwa picha zilizopigwa na kamera: basi nitakujulisha ndugu yangu kwamba sikuruhusu kupiga picha (nia ya picha ni ambayo ina roho kutoka kwa wanadamu na wengine) isipokuwa kwa lazima au haja, kama: uraia, leseni, kuanzisha haki na kama.

Ama kupiga picha kwa ajili ya heshima, kumbukumbu, au kujifurahisha kwa kuzitazama, basi sikuruhusu hilo iwe ni masanamu au picha zilizotengenezwa kwa mkono au mashine kutokana na ujumla wa kauli ya Mtume swallallahu alayhi wa sallam:

“لا تدخل الملائكة بيتاً فيه صورة”

"Malaika hawaingii katika nyumba ambayo ndani yake kuna sanamu."

Malaika hawataingia kwenye nyumba ambayo ina picha ndani yake

Na sijaacha kutoa hukumu kwa hilo na kumuamuru mwenye picha ya kumbukumbu aiharibu. Na mara nyingi mimi ni mkali ikiwa ni picha ya mtu aliyekufa.

Ama picha za vitu vyenye nafsi kama binadamu au vingine visivyokuwa hivyo, basi hakuna shaka katika kuharamishwa kwake na ni katika madhambi makubwa kutokana na uthibitisho wa kumlaani mtendaji kwa ulimi wa Mtume (Swalla Allaahu alayhi wa aalihi wa sallam). Hii inaonekana katika kile ambacho ni sanamu au kilichofanywa kwa mkono. Ama kamera inayotoa picha na hakuna hatua kutoka kwa mpiga picha ya kuchora uso au maeneo ya mwili, basi ikiwa picha itazalishwa kwa ajili kumbukumbu na madhumuni kama hayo ambayo picha hairuhusiwi kupigwa, kisha kuizalisha kwa kamera ni marufuku kwa makatazo ya njia hiyo. Ikiwa picha inatolewa kwa umuhimu au haja, basi hakuna madhara.
Mbona wao walionekana kwenye macamera je hawakujua hukumu hii ?

Fauzan mpaka leo anaonekana kwemye camera je hajui hukumu hii na fatwa ya ibn uthaymeen?

Je hawa mashekhe wa tanzania wanaweza kuwa na uchamungu wa kumzidi fauzani ?

kiasi kwamba fauzan asiogope kufanya jambo hili la haramu alafu ndugu zetu masalafitz wanaogopa kwa uchamungu wao mkubwa ?
 
Sina kawaida ya matusi kwa sababu huwenda mtu akachukulia hiyo ni sababu ya kuacha mjadala na mimi.

NImekujibu kwa hoja zilizowazi bila ya matusi ya aina yoyote.

NDugu zangu masalafi mkiona hoja hamuziwezi huwa mnasema hamjibu.

Na hiyo aliianza ndugu yetu abul fadhwli kassim mafuta alipobainishiwa hoja zenye nguvu na yule abuu haatim kuhusiana na mas'ala ya sheikh yahya al hajuuri abul fadhli alisema HAJIBUU,wakati huo huko nyuma alikuwa anajibu ila alipozidiwa hujjah akasema hamjibu tena😀

Ila ni hajibu kwa sababu hoja zinakuwa zimemzidi.

Wakati huo huo abul fadhli wakati anamradi mmombasa mmoja kuhusu "arafah" aliwahi kusema kwamba MARKAZI YA PONGWE HAINYAMAZII UBABAISHAJI WA AINA YEYOTE ILE.

Lakini unaona kuna baadhi ya mambo kayanyamazia hiyo maana yake anayoyanyamazia abul fadhli sio ubabaishaji bali ndio haki yenyewe.

Hivyo haya mambo sio kwamba umeanza wewe wameanza waalimu wenu kunyamazia hoja ambazo zinawazidi.

USHAURI WANGU : Muombe Allah ufahamu wa kuifahamu elimu,kisha usione tabu kutumia akili kuyaelewa maandiko ndugu yangu.

Na Allah ndio mjuzi.
Ndio maana nilisema nimeshajua najadiliana na mtu wa aina gani, kupoteza muda sio ada yangu, nimebainisha ninachokijua kwa sasa sina cha kukupa faida kingine kwasababu itakuwa natafuta ushindi.
 
Ndio maana nilisema nimeshajua najadiliana na mtu wa aina gani, kupoteza muda sio ada yangu, nimebainisha ninachokijua kwa sasa sina cha kukupa faida kingine kwasababu itakuwa natafuta ushindi.
Kila la heri kaka.

RUdi tu akhy al kariym ukajifunze ufahamu wa Dini na sio fikra za watu huku mafhum sahihi ya dini mkiyaweka pembeni.

Sisi bado tunaendelea kujitahidi kuifahamu Dini na tunaendelea kumuomba Allah mpaka atakapotufisha.
 
Mkuu ni vile tu umegoma kuelewa kabisa, ila post zangu nilizokujibu mambo ya kutumia akili na makusudio yetu kwenye hilo yalitosha kabisa kukukinaisha kuwa makusudio sio kuacha kudadisi na kutafakari mambo, au ni kuangalia nani mshindi? kama ndio hivyo mimi nimekubali nimeshindwa kwani sitojibu tena baada ya hapa.

Mwisho, kujua hekma ya kuharamishwa kitu fulani kama pombe, kamari, na mabaya mengine ni kitu mbali kabisa na kutumia akili yako kupingana na nusuus za kisheria, unataka kuniambia hujui wabobezi wa elimu za falsafa wanafanyaje kuleta talbiys katika aya na hadithi za mtume? watu wazushi wangapi wameangamia kwa kuacha kufanyia kazi Qur'an na sunnah kwa kigezo kuwa kuna vigezo vya elimu ya mantwiq havijaenda sawa? haya ndiyo tumeyabainisha tangu mwanzo na ubaya wake.

Na mimi najikinga na Allah kutokana na kuisemea dini yake pasi na elimu, wallahi katu sijasema watu wasidadisi wala wasitumie akili zao kufahamu mambo ya kisheria, ama hekma ya kuharamishwa mambo fulani katika dini nyingine zimebainishwa nyingine haifahamiki hekma yake, ukianza kutumia akili yako kupambana na hekma isiyotajwa utakuwa iko sahihi? nitakupa mfano wa aya moja kabla ya kufunga mjadala huu kwa upande wangu.

"Enyi mlioamini! hakika hapana vingine, ulevi, na kamari, na kuabudu masanamu, na kupiga ramli, ni uchafu katika kazi ya shetani, basi jiepusheni na hayo ili mpate kufanikiwa."

Kisha allah subhaanah akataja baadhi ya madhara ya mambo hayo, akasema:

"Hakika hapana vingine, anataka shetani kutia kati yenu uadui na chuki kwa ulevi na kamari, na akuzuieni kuachana na kumkumbuka Allah na kuswali pia, basi je! hamtoacha?!"
Qur'an 5:90-91


Hapa Allah subhaanah ametutajia baadhi ya madhara ya pombe na kamari, kuna ubaya gani sisi kutafakari kuhusu haya? lakini vipi yale yasiyotajwa hekma yake? mfano walimuuliza mayahudi mtume swala na salaam kuhusu roho ni nini roho? Allah subhaanah akateremsha:

"Na wanakuuliza kuhusu roho, sema: Roho ni katika mambo ya mola wangu, nanyi hamkupewa katika elimu isipokuwa kidogo tu."
Qur'an 17:85

Sasa akaanza mtu kutumia akili yake kudesign ufahamu anaoujua yeye na kutengeneza fikra anazozijua yeye akaanza kueleza kuwa roho iliyokusudiwa hapa ni kadha, akapingana na nasw ya Qur'an kwa kutumia akili yake, hili ndilo lililokatazwa katika matumizi ya akili kwenda kinyume na maandiko ya kisheria.

Ama mimi sitojibu tena kuhusu suala hili la kutumia akili na yanayohusiana.
Akhy, kwanza shukran kwa kuwa na mjadala wenye tija na wa kistaarabu, hatupo hapa kwa lengo la kutafuta mshindi ni nani bali ni katika kukumbushana na kuusiana kheri maana mkamilifu baina yetu hakuna...

Tukirudi kwenye hoja,..Mimi binafsi nimekuelewa vizuri kile unachomaanisha juu ya kutumia akili ni kwamba:-
1. Umeridhia kwamba akili ni muhimu kutumika kuchanganua mas'ala mbalimbali kwenye dini, Nakunukuu "wallahi katu sijasema watu wasidadisi wala wasitumie akili zao kufahamu mambo ya kisheria, ama hekma ya kuharamishwa mambo fulani" ...hapa tupo pamoja.

2. Umetolea mfano watu wa falsafa na watu wazushi,. kwamba utumiaji wao wa akili umewafanya wadai kuna vigezo vya kimantiki haviendi sawa.
....Akhy, nikutoe shaka akili iliyosalimika na kibri haiwezi kupingana na ukweli uliopo kwenye Qur'an,. hivyo watu wa namna hiyo huenda kiburi tu ndiyo kimewafikisha huko,.. maana akili kiuhalisia haipingani na Qur'an na ndiyo maana Allah kupitia Qur'an anahimiza watu wote mpaka wanafalsafa na wazushi kutumia akili zao kuelewa Qur'an...

mwisho wa siku mtu ambae anasoma ili apinge basi hata akutane na ukweli wa aina gani...atapinga tu.


Ndugu yangu,. Akili iliyosalimika inajua kuna ukomo wa ujuzi wake(yaani kuna vitu haivijui mpaka pale itakapopatikana njia ya kujua kitu husika)
Akili iliyosalimika ikiambiwa kwamba elimu juu ya roho ipo Kwa Allah,..basi itasema imesikia na Inatii hivyo...mtu akiendelea kudadisi kisha akaleta majibu yake kwamba roho ni kadha wa kadha, majibu ambayo bila shaka ni uongo,.basi huyo atakua amekosea.

Kimsingi, akili inajua kwamba kuna vitu vipo nje ya uwezo wake kuvifahamu mfano roho, mas'ala ya ghaib na kadhalika....hivyo mtu mwenye kutaka kutumia akili yake kujua undani wa vitu hivyo hawezi kuwa sahihi,.naungana na wewe.
 
Ni dalili gani ya kisheria inayosema kwamba neno "swuwrah" ni picha za watu na wanyama tu ?
In shaa Allah kesho, kwa faida ya wasomaji wengine wa uzi huu nitaleta fatwa za hao Wanazuoni wengine uliowataja. Fatwa kuhusiana na masuala ya picha.

Ila Mkuu, mbona wewe umejawa na negativity psyche ya aina hii. Kila kitu wewe unapinga tu na kutafuta neno, kauli au sentensi yoyote tu yenye uelewe uliojificha ili mradi upate msingi wa kujenga hoja mpya ya kupinga. Mfano, hadi muda huu, mtu akifuatilia post zako zote ulizozileta ktk uzi huu atagundua jinsi gani ulivyokithiri ktk upingaji wa kila kitu. Binafsi sina shaka na ninathibitisha kuwa una elimu kubwa zaidi yangu. Kuna mahali pia hata ulimtaja Shaikh wangu mbora Abu Haatim wa Bomang'ombe. Lakini mbona sikuoni ukizungumzia Uislam kwa uzuri wake.

Mfano, umetumia nguvu kubwa kuwakashifu Maswahaba. Ningetamani nione kauli zako za kuwasifu Maswahaba.

Upendezewi na kauli ya Masalafi inayosema " Tunafuata Quran na Sunnah kwa ufahamu wa wema waliotangulia".
Lakini pia unatutaka tutumie akili zetu zaidi pindipo pale tunapokutana na kauli mbalimbali za haki kutoka kwa Wanazuoni wetu.

Mfano, hapa nikimalizia kwa kusema mirungi ni haramu, kubwia ugoro ni haramu, kuvuta sigara ni haramu. Mara moja utaweza kuniambia...

"Mkuu tunaomba dalili ambayo imeainisha kama hivi ambavyo umeainisha wewe."
 
Akhy. Picha za viumbe vyenye roho ktk binadamu na wanyama ni haramu kaka. Mchoraji picha za aina hizo, mchongaji masanamu/vinyago, mpiga picha za kawaida/video ni ktk makundi ya watu watakaopata adhabu kali sana tena sana na iumizayo.
Lakini pia, yule anayening'iniza picha hizo ukutani au kuvaa ktk nguo, au mapazia/mazulia na mfano wa hayo pia atapata adhabu kali siku ya kiama. Na mapicha hayo ukiyaweka ndani ya nyumba basi tambua kuwa malaika wema hawaingii ndani ya nyumba yk.
Aidha ktk hili kuna mlango wa dharura kutokana na sheria zilizowekwa na serikali. Mfano, kwa matumizi ya passport, vitambulisho na mfano wa hayo.
Elimu kama hizi utazipata ktk madrassa za Masalafi pekee.
Utakuta watu wanapiga mapicha/mavideo ndani ya Misikiti. Utakuta ndani ya Misikiti kuna poster zina picha za viumbe vyenye roho. Haya ni mambo ya maasi makubwa ktk Uislam. Allah awaongoze wote wenye kufanya matendo haya maovu kabisa.
Mwisho, yeyote mwenye kutaka dalili na ushahidi juu ya jambo hili basi awasiliane nami Whatsapp 0688999006. Ninaheshimu privacy za watu.
Miongoni mwa Faida utakayoipata kupitia link nitakayokupaia:
1. Utapata elimu sahihi kupitia Quran na Sunnah.
2. Masheikh wetu na Maduat wanatumia AKILI kubwa kufikisha Da,wah kwa lengo la kujenga ufahamu kamili kwa Muislamu yyt.
Katika vitu ambavyo watu hupata shida kuvielezea kwenye Dini hii ni vile ambavyo vipo nje ya Qur'an.....(Nadhani unajua sababu hasa ni nini)


Unasema kuna mlango wa dharura wa kutumia picha ukaweka mfano passport na vitambulisho.... naamini dalili juu ya dharura hiyo haipo kwenye Qur'an wala Sunnah(huoni kama unakua umezusha?)

NB:- Nakushauri shikamana na Qur'an,. Ukiona jambo nje ya Qur'an lipime Kwa mizani ya Qur'an,. maana Allah amebainisha kila kitu humo yaani kama jambo ni Haram utalikuta ndani ya Qur'an na vice versa.
 
Unatumia hela?
Mkuu soma vizuri nilichopost. Kuna mahali nimeandika " Aidha ktk hili kuna mlango wa dharura.... endelea hapo. Dharura inahusiana na sheria na taratibu za miamala zilizowekwa na nchi. Pesa inaingia hapo. Hati za kimahakama, leseni za udereva nk.
Natumai umenielewa.
Ikikupendeza wasiliana nami Whatsapp 0688999006 nikutumia darsa kamili za audio juu ya Mada hii ya mapicha
 
Akhy, kwanza shukran kwa kuwa na mjadala wenye tija na wa kistaarabu, hatupo hapa kwa lengo la kutafuta mshindi ni nani bali ni katika kukumbushana na kuusiana kheri maana mkamilifu baina yetu hakuna...

Tukirudi kwenye hoja,..Mimi binafsi nimekuelewa vizuri kile unachomaanisha juu ya kutumia akili ni kwamba:-
1. Umeridhia kwamba akili ni muhimu kutumika kuchanganua mas'ala mbalimbali kwenye dini, Nakunukuu "wallahi katu sijasema watu wasidadisi wala wasitumie akili zao kufahamu mambo ya kisheria, ama hekma ya kuharamishwa mambo fulani" ...hapa tupo pamoja.

2. Umetolea mfano watu wa falsafa na watu wazushi,. kwamba utumiaji wao wa akili umewafanya wadai kuna vigezo vya kimantiki haviendi sawa.
....Akhy, nikutoe shaka akili iliyosalimika na kibri haiwezi kupingana na ukweli uliopo kwenye Qur'an,. hivyo watu wa namna hiyo huenda kiburi tu ndiyo kimewafikisha huko,.. maana akili kiuhalisia haipingani na Qur'an na ndiyo maana Allah kupitia Qur'an anahimiza watu wote mpaka wanafalsafa na wazushi kutumia akili zao kuelewa Qur'an...

mwisho wa siku mtu ambae anasoma ili apinge basi hata akutane na ukweli wa aina gani...atapinga tu.


Ndugu yangu,. Akili iliyosalimika inajua kuna ukomo wa ujuzi wake(yaani kuna vitu haivijui mpaka pale itakapopatikana njia ya kujua kitu husika)
Akili iliyosalimika ikiambiwa kwamba elimu juu ya roho ipo Kwa Allah,..basi itasema imesikia na Inatii hivyo...mtu akiendelea kudadisi kisha akaleta majibu yake kwamba roho ni kadha wa kadha, majibu ambayo bila shaka ni uongo,.basi huyo atakua amekosea.

Kimsingi, akili inajua kwamba kuna vitu vipo nje ya uwezo wake kuvifahamu mfano roho, mas'ala ya ghaib na kadhalika....hivyo mtu mwenye kutaka kutumia akili yake kujua undani wa vitu hivyo hawezi kuwa sahihi,.naungana na wewe.
MashaAllah akhy. You nail it. Allah akuhifadhi brother
 
Katika vitu ambavyo watu hupata shida kuvielezea kwenye Dini hii ni vile ambavyo vipo nje ya Qur'an.....(Nadhani unajua sababu hasa ni nini)


Unasema kuna mlango wa dharura wa kutumia picha ukaweka mfano passport na vitambulisho.... naamini dalili juu ya dharura hiyo haipo kwenye Qur'an wala Sunnah(huoni kama unakua umezusha?)

NB:- Nakushauri shikamana na Qur'an,. Ukiona jambo nje ya Qur'an lipime Kwa mizani ya Qur'an,. maana Allah amebainisha kila kitu humo yaani kama jambo ni Haram utalikuta ndani ya Qur'an na vice versa.
Akhy. Umeuliza jambo zuri mno na In Shaa Allah nitakupatia jibu ambalo litawanufaisha wengi ktk wanaofuatilia post hili. Lakini awali ya yote kwanza... Je, Unaamini kuwa picha za viumbe vyenye roho ni haramu?
 
shaa Allah kesho, kwa faida ya wasomaji wengine wa uzi huu nitaleta fatwa za hao Wanazuoni wengine uliowataja. Fatwa kuhusiana na masuala ya picha.
SAwa ndugu ila hakikisha iyo fatwa iko na dalili inayosema kwamba "swuwrah" ni matu na wanyama.
Ila Mkuu, mbona wewe umejawa na negativity psyche ya aina hii
Ni vizuri ungeonesha wapi nimeweka negative psyche unibainishie kwa hoja nami huwejda nitajifunza.
Kila kitu wewe unapinga tu
Hizi tuhuma hata masalafi wanatuhumiwa kwamba wao wanapinga kila kitu,maulidi,khitmah wanapingaaa.

Hizi tuhuma bila shaka unazijua.

Je tuhuma hizo ni za kweli dhidi ya masalafy au masalafy wanapinga kwa dalili ambazo wanazisimamia ?

Sasa basi tambua kaka kwamba hizo tuhuma zako juu yangu ni kama tuhuma za watu wengine dhidi ya masalafy wala hazina dalili wala ushahidi.

Kila pahala nilipopinga mimi nimebainisha kwa hoja kwa nini napinga na hiyo ndio mjadala unavyokuwa kaka.

Mfano, hadi muda huu, mtu akifuatilia post zako zote ulizozileta ktk uzi huu atagundua jinsi gani ulivyokithiri ktk upingaji wa kila kitu
Napinga kwa hoja kaka,katika comment zangu zijajaza matusi nimeweka hoja na maswali kadha wa kadha.
Nimestaajabu sana leo ndugu yangu salafy kumlalamikia mtu mwingine kwamba anapinga kila kitu 🙂😀😀😀

Kuna mahali pia hata ulimtaja Shaikh wangu mbora Abu Haatim wa Bomang'ombe.
Naam abuu haatim alimtandika vizuri kassim mafuta kwenye kadhia ya yahya al hajuri na alimpa hoja nzito ambazo abul fadhli mpaka leo hatoweza kuzivunja.

Na pia nipo katika group la abuu haatim la telegram liitwalo "firqatu annajiyyah nastafidi huko kwa darsa mbali mbali kama akina sheikh khamis ame,abuu haatim na wengineo..
Lakini mbona sikuoni ukizungumzia Uislam kwa uzuri wake.
Mche Allah kaka.
Nioneshe sehemu moja tu ambayo nimeusema UISILAMU VIBAYA NDUGU YANGU ?
Mfano, umetumia nguvu kubwa kuwakashifu Maswahaba.
Hili pia unanizulia kaka,na kumzulia uongo muisilamu sio sawa.

KAma kusema masahaba walipigana kwa majibu wa maandiko ndio kukashifu masahaba basi wameanza kukashifu walioandika historia hizo.
Kama kusema kuna sahaba alizini kwa mujibu wa maandiko ati tunatukana masahaba basi wameanza kukashifu walioandika.

Hakuna pahala nimekashifu masahaba bali nimenukuu historia na maandiko.

Au unadhani ile historia imewekwa ili ifichwe isisemwe ?
Ningetamani nione kauli zako za kuwasifu Maswahaba.
HAkuna kauli yangu ambayo inaonesha nimekashifu sahaba yeyote ndugu nisome vizuri.
Mfano, hapa nikimalizia kwa kusema mirungi ni haramu, kubwia ugoro ni haramu, kuvuta sigara ni haramu. Mara moja utaweza kuniambia...
NAam huo ndio utaratibu kaka.

Kama ambavyo watu wengine hudai dalili ya wazi wapi maulidi yanafaa ?

Wengine hudai dalili wapi khitma inafaa ?

Sasa iweje kwa wengine kudai dalili ya hukmu kwa jambo ambalo halikuwepo wakati huo wa Mtume iwe tabu kakak yangu ?
 
Mkuu Wildlifer pamoja na Nifah ngoja niwajibu.

Bila ya shaka rakaa ya pili kabla ya kusujudu walisoma kunut. Kunut ilisomwa na Mtume Muhammad s.a.w kipindi cha shida.

Sasa kusoma kunut mantiki ni kwamba; kama una shida soma. Ila kama mtu anajiona hana shida asiisome. Suala si bidaa, suala ni uelewa.

Shadhuli au shadhli ni jina la mwanawazuoni mkubwa. Kwa ukamilifu anaitwa Imam Abul Hassan Ash-shaadhily. Ni mwanafunzi wa Imam Abdi Ssalaam Ibn Mashish.

Imam Abul Hassan Ash-shaadhily ni mwanawazuoni pia amebobea kwenye elimu ya tasawwuf yaani Sufi. Elimu ya Sufi ni elimu yenye majina takribani 21+. Kwa jina jengine inaitwa elimu ya Tazkiya au elimu ya Zuhdi au elimu ya Tarbia au na au n.k Kwa majina maarufu inaitwa elimu ya tasawwuf.

Nini maana ya elimu ya Tasawwuf.
Imam Malik anasema; "Man tafaqaha walam yatasawwaf faqad taffassaqa. Waman tasawwafa walam yatafaqaha fadaq tandazandaqa. Akamalizia akasema waman jam-u baina huma faqad tahaqaqa." Maneno haya yanapatikana katika Hashya ya Al Adawi ya Imam Al Zurqani juzuu ya 2 ukurasa wa 195.

Imam Maliki anasema; yeyote (man iliyotumika hapa ni man shurtwiyya)-yeyote atakayesoma elimu ya fiqhi pasipo kusoma elimu ya tasawwuf basi huyo mtu atakuwa ni fasiq. Na yeyote atakayesoma elimu ya tasawwuf pasipo kusoma elimu ya fiqhi basi huyo mtu atakuwa ni mzandiki. Akamalizia akasema; na atakayechanganya mawili hayo basi atakuwa kwenye haqi.

-Imam Shafii kaizungumzia tena kwa wema. Angalia kitabu cha Muhaddith Al Ajilun kinaitwa Kashaf al Khafa wa Muzil Al Albas.

-Ibn Qayyim katika Madarij Al Salikin na Imam Suyutwi katika Tayid Al Haqiqa Al Aliya.

-Imamul Adham Nuuman Ibn Thabit Imam Abuu Hanifa anasema; kama siyo hii miaka 2 bila kuwa kujifunza elimu ya tasawwuf mimi Abuu Hanifa ningeangamia. Maneno haya unayapata katika kitabu cha Ad Durr Al Mukhtar juzuu ya 1 ukurasa wa 43.

Uthibitisho upo mwingi sana kuhusiana na Sufi ama tasawwuf. Hivyo Sufi au elimu ya tasawwuf si elimu ngeni! Bali ugeni tunao sisi katika hiyo elimu.

Sufi ama tasawwuf ni elimu ya kuitakasa nafsi. Fiqh ni elimu ya umbile la nje yaani mwili ama kiwiliwili. Elimu ya sharia(fiqh) ni kwa ajili ya kuongoza umbile lako. Funga unaotumikisha mwili wako. Kuhiji ni mwili wako unaotumikisha kuiendea ibada ya Allah. Swala ni mwili wako unaotumikisha kuiendea ibada ya Allah.

Haya yote yanatekelezwa na wewe. Lakini vipi kuhusu undani wako yaani moyo wako? Moyo wako ni safi? Mtu anaweza akafunga, kuhiji n.k lakini bado akawa ni mwenye roho mbaya, kiburi n.k: Ni kama ilivyo zakka ni inatakasa mali yako ndivyo vivyo hivyo elimu ya Sufi ama tasawwuf ni elimu ya kuitakasa nafsi yako. Na ndiyo maana inaitwa elimu ya ndani ya kiwiliwili.

Na hauruhusiwi kusoma elimu ya tasawwuf mpaka usome fiqhi. Naam, kwenye dini kuna wahuni pia! Wanawazuoni wameweka taratibu takribani 21 za kumtambua mwanawazuoni halali wa kitasawwuf.

Ama kuhusu kuweka duara na kutoa sauti kama kukabwa sauti aha! Au a-aha! A-aha! Ukisema aha! Kinahau ni mufrad. Ikitamkwa A-Aha-Aha! Hii inaitwa Jamiiu tak-siim. Kwa kufupisha hii ni dhikr Saadia. Dhikr ya kwenye koho au kukohoa! Ahaa kwa maana ni Allah! Ni jina lake Allah lile!

Nenda kaangalia katika tafsiri ya Qur'an ya Imamul Qurtubi ambaye ndiye beberu katika wanawazuoni wa tafsiri ya Qur'an. Nenda katika surat Tawba katika aya inayosema "Inna Ibrahimal awwaahuun"
-Narudia tena, katizame tafsiri na sio tarjama(subtitle). Ibrahim alikuwa akifanya hii dhikr. Katika hadithi (ambayo nimeisahau imepokelewa na nani) kuna mtu alienda kushitaki kwa Mtume Muhammad s.a.w kuna mtu anatufu Al Kaaba huku akisema ah-aha! Mtume Muhammad s.a.w akamwambia muache! Hakika huyo mtu ni awwahuun.

Imam Ghazal (kitabu chake nimekisahau nikipitia vitabu nitakuwekea inshaallah) ila ni juzuu ya 4. Mtume aliketewa habari na Jibril A.S (inna rabbuka yaq-raukka ssalaam.....) Mtume aliifanya hii dhikr ya Ah-Aha pamoja na maswahaba mpaka kilemba chake Mtume Muhammad s.a.w kilianguka chini.

Imam Suyutwi anasema hii dhikr ya kukohoa aliifanya Nabii Zakariya A.S, Nabii Ibrahim A.S na Hidhr A.S na Mtume wetu Muhammad s.a.w katika Jabal Hiraa mpaka sauti ikawa inafika umbali wa masafa maili (mile) 24. Haya utayakuta katika kitabu cha Haujat Mudhakkiriina cha Imam Suyutwi.
Mkuu Hammaz kwa hakika umekuja na jambo baya kabisa, ninyi wenzangu hamna hofu kabisa hata kidogo, hamjui kuna siku tutafufuliwa tusimamishwe mbele za Allah subhaanah? mambo yetu wenyewe yanatushinda, huu ujasiri wa kuisemea dini ya Allah pasi na elimu wala maarifa tunautoa wapi? na hii ni katika sifa ya watu madhalimu kumzulia Allah uongo.

"......na hakuna aliye dhalimu zaidi kuliko yule aliyemzulia Allah uongo, ili awapoteze watu pasi na elimu, hakika Allah hawaongozi watu madhalimu."
Qur'an 6:144

Mimi niseme tu binafsi nimejiskia vibaya sana kwa mambo uliyoandika hapa kutetea baatwil ya wazi na bali kuiwekea namna ibada adhimu ya dhikri kwa mfumo usiothibiti kabisa kutoka kwa mtume swala na salaam ziwe juu yake wala maswahaba zake wala waliowafuatia maswahaba zake, kiukweli nimejiskia vibaya sana, na haya mnayafanya kwasababu mnatambua waislamu wengi si watu wa kusoma wala hawaelewi wapi pa kushika.

Namuomba Allah anipe thabaat na tawfiyq niweze kukujibu nukta kwa nukta pasi na kuruka hata paragraph moja katika yale uliyoyaandika na yakawa sio ya sawa.

Ama suala la qunuut wakati wa majanga, sisi tumeshuhudia maimamu wa misikiti mingi kama sio yote wakisoma qunut ya witri katika swala za faradhi, na huu uzushi ama ujaahil wa wazi, kwasababu qunuut wakati wa majanga yanapowashukia waislamu sio ile qunuut ya witri wanayoisoma watu, bali hata Wildlifer bila shaka alisikia wakisema "allahumma hdinaa fiy man hadayta wa 'aafinaa fiy man 'aafyata watawallanaa fiy man tawallayta"......mpaka mwisho wake

Hii sio qunuut ya naazilah wakati wa matatizo na majanga yanapowashukia waislamu, hivyo tunasema huu ni uzushi au ujinga wa kutokujua kayfiyyah ya qunuut husika, na si uelewa kama ulivyosema, mtume swala na salaam ziwe juu yake alipata kusoma mwezi mzima katika swala za faradhi na hakuwa anasoma qunuut ya witri bali anasema ee allah muokoe fulani! na fulani! na akiwaombea dua mbaya washirikina anasema ee Allah! wapelekee ukame kama ukame wa watu wa yuusuf! na mfano wa hayo.

Hilo ni moja jambo la pili, kuhusu twariqah ya shaadhiliyyah na abul hassan al maghribiyy uliyemtaja hawa watu itikadi yao kuhusu Allah subhaanah ni itikadi ya kiupotevu ya wihdatul wujuud, wihdatul wujuud ni nini? hii ni itikadi ya kifalaasifa, na watu hawa humfanya sawa Allah na viumbe vyake, mas'ala haya ni magumu kueleweka kwa watu wanaosoma wachilia mbali kwa watu wa kawaida, ila nitatoa mifano michache ya maneno ya maimamu wakubwa wa hizi twariqah wanaoitakidi itikadi hii ya al-ittihadiyyah, amesema shekhe wa mashekhe imdaadu-llah al muhaajir al makkiyy amefariki mwaka 1317H: "kutofautisha baina ya mja na muabudiwa{Allah} ndio ushirikina halisi." pia akasema "mja kabla ya kuwepo kwake {kudhihiri duniani} alikuwa ndio mola kwa kificho, na mola ndiye mja kwa dhaahir" pia amesema shaykh fadhwl haqq al khayr aabaadi: "lau wangelazimishwa mitume kulingania kwenye wihdatul wujuud, basi ingebatilika ile hekma ambayo kwaajili ya hekma hiyo ndiyo wakatumwa mitume, basi wakaamrishwa wawazungumzishe watu kwa kadri ya uwezo wa akili zao!"
Haya maneno utayapata katika shamaaim imdaadiyyah na hayo ya pili katika kitabu chake arrawdhw.

Tizama ukafiri unaolinganiwa katika itikadi hii ya kifalsafa ambayo hao twariqah ya shaadhiliyyah ndiyo wako juu yake, na ndio wanaitakidi hivyo kunako Allah subhaanahu wa ta'alaa, allah ametakasika kabisa na itikadi hii chafu na mbovu kabisa.

Ama kuhusu swuufiyyah, hii ni mada nyingine ndefu, lakini maneno yaliyonukuliwa kuwa ni ya imaam maalik ibn anas al-aswbahiy allah amrehemu kuwa amesema: من تصوف ولم يتفقه فقد تفسق، ومن تفقه ولم يتصوف فقد تزندق
"yeyote mwenye kujifunza usufi na asijifunze fi-qhi basi amefanya ufasiqi, na yeyote atakayejifunza fiq-hi na hakujifunza usufi basi amefanya uzandiki"


Maneno haya kwa uhakika si maneno ya imaam maalik allah amrehemu, bali imaam maalik wakati wa zama zale hapakuwa mashuhuri kutumika neno "swuufiyyah" sasa sijui mkuu Hammaz umetoa wapi ujasiri wa kunukuu maneno hayo kutoka katika haashiyya ya al-adawiyy kunako sharhu ya zarqaani katika fiqh ya kimaaliki na kuyanasibisha na imaam maalik allah amrehemu, vitabu vilivyoandikwa na imaam maalik ni muwatwa'a kitabu maarufu cha hadithi na fataawa zake zilizonukuliwa katika mudawannah assughra na kubra kote huko hakuna maneno hayo kabisa, na kama nilivyotangulia kusema, neno swuufiyyah halikutumika wala kuwa maarufu katika karne za mwanzo na imaam maalik amezaliwa mwaka 93H kuashiria ni katika maimamu waliozaliwa mwishoni mwa karne ya kwanza na ni shekhe wake imaam shaafiiyy allah awarehemu wote, sasa nataka uniambie haya maneno imaam maalik ameyasema wapi na katika kitabu gani? vinginevyo amesingiziwa jambo hilo kutia nguvu itikadi za swuufiyyah na ibada zao zilizo batili kabisa.

Ama imaam shaafi'iyy Allah amrehemu yeye ni ajabu kubwa kusikiwa amewasifu masufi kwani maneno yake akiwasema vibaya sana yako maarufu mbele ya watu wa elimu, فعن يونس بن عبد الأعلى قال سمعت الشافعي يقول : " لو أن رجلا تصوف أول النهار ، لا يأتي الظهر حتى يصير أحمق " .
"imepokewa kutoka kwa yuunus ibn abdil-a'alaa ambaye ni mwanafunzi wake akisema kuwa: "nimemskia ashaafiiyy akisema "lau kwamba mtu angejifunza usufi mwanzo wa mchana basi isingefika adhuhuri mpaka awe mpumbavu." bali pia amesema:"Hajapatapo mtu kulazimiana na masufi siku arobaini, kisha ikamrudia akili yake milele."
Rejea kitabu talbiys-ibliys uk 327 na kitabu al istiqaamah cha shaykhul islaam uk 414/1


Basi huu uwe utangulizi wa kwanza wa majibu yetu kuhusu suala hili la hawa shaadhiliyyah na masufi wengine kwa ujumla, juu ya yale aliyotaja Hammaz kwa kumsingizia Allah na mtume wake uongo bali na wanawachuoni wakubwa wa kiislamu, kesho inshaallah ntaendelea nilipoishia.

Na Allah ndiye mjuzi zaidi.
 
Katika vitu ambavyo watu hupata shida kuvielezea kwenye Dini hii ni vile ambavyo vipo nje ya Qur'an.....(Nadhani unajua sababu hasa ni nini)


Unasema kuna mlango wa dharura wa kutumia picha ukaweka mfano passport na vitambulisho.... naamini dalili juu ya dharura hiyo haipo kwenye Qur'an wala Sunnah(huoni kama unakua umezusha?)

NB:- Nakushauri shikamana na Qur'an,. Ukiona jambo nje ya Qur'an lipime Kwa mizani ya Qur'an,. maana Allah amebainisha kila kitu humo yaani kama jambo ni Haram utalikuta ndani ya Qur'an na vice versa.
Kuna zama zilipita hadithi nyingi za uongo zilizushwa.

Jambo la kusikitisha utakuta kijana wa kisalafy au kijana wa kiisilamu kasoma usuulu sunna,umdatul ahkaam,riyaadh,bulughu al maraami n.k

Lakini hajamaliza japo juzuu 10 za tafsiri ya Qurani,hapo unategemea nini ?

Lazima waone Qurani haina lolote,wataona Qurani haina ufafanuzi wowote na kukimbilia kwenye hadithi ambazo nako watu hupata tabu kuzifafanua.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom