Tumekua tukisikia habari za Dr Slaa kwa namna tofauti kutoka kwa viongozi wa chadema,baada ya kile kikao 26. 7 .2015.
Mwanzo kabisa tuliambiwa yuko katika shughuli nyeti za chama,mara yupo safarini,kafungiwa,ndani na mkewake, etc.
Kufuatana na kauli ya Dr alikua ameandika barua ya kujiuzulu, viongozi wengi wa chama wamekua wakitoakauli za uwongo kuhusu sakata hili.
Mwenyekiti alitamka akasema wakati ukifika nitaeleza yalijiri. Akihutubia mkutano mkuu wa CHADEMA Mwenyekiti alisema nimeonana na Dr Slaa nimeongea nae kwa masaa mawili lakini hawakuafikiana.
Baada ya hapo Mwenyekiti amekuwa akimshambulia Dr kiaina, kulikua na tuhuma za mwenyekiti kupokea fedha mpaka leo hajakanusha.
1. Kama Dr aliandika barua ya kujiuzulu kwanini mwenyekiti hakuwatangazia mkutano mkuu badalayake anasema dr amesema tuendelee tutakutana nae mbele.
2. Je ni kweli hawakua wamejiandaa kua na mgombea urais wachadema.mwenyekiti alisema hadharani kwamba akianza mchakato huu wa el hakuna aliekua anajua ndani ya chama ila Maalim Seif Tundulisu anasema yake na Slaa anasema yake, nauliza nani anasema kweli?
3. Kama ni kweli mchakato wakumleta EL CHADEMA ulikua umeanza kabla ya kura za maoni CCM je EL alikua msaliti ndani ya CCM.
4. Sitaki kuamini kama alivyosema Dr kwamba Naibu Katibu mkuu alimwambia kwamba jambo hili limeshaamuliwa usijisumbue, yaani dili teyari, gia imebadilishwa angani.
5. Tumeshuhudia Chacha Wangwe, Zitto, Mwigamba, Kitila watu, walioshinda kwenye kura za maoni wakaenguliwa na sasa Dr tunaambiwa ni wasaliti hakuna wasafi huko?
Mwisho kama EL akijitoa kwenye kinyang'anyiro au akishindwa nana atabeba lawama?
Kwanini kila anayetoa yake ya motoni anakua msaliti, ndio demokrasia hiyo?
Mwanzo kabisa tuliambiwa yuko katika shughuli nyeti za chama,mara yupo safarini,kafungiwa,ndani na mkewake, etc.
Kufuatana na kauli ya Dr alikua ameandika barua ya kujiuzulu, viongozi wengi wa chama wamekua wakitoakauli za uwongo kuhusu sakata hili.
Mwenyekiti alitamka akasema wakati ukifika nitaeleza yalijiri. Akihutubia mkutano mkuu wa CHADEMA Mwenyekiti alisema nimeonana na Dr Slaa nimeongea nae kwa masaa mawili lakini hawakuafikiana.
Baada ya hapo Mwenyekiti amekuwa akimshambulia Dr kiaina, kulikua na tuhuma za mwenyekiti kupokea fedha mpaka leo hajakanusha.
1. Kama Dr aliandika barua ya kujiuzulu kwanini mwenyekiti hakuwatangazia mkutano mkuu badalayake anasema dr amesema tuendelee tutakutana nae mbele.
2. Je ni kweli hawakua wamejiandaa kua na mgombea urais wachadema.mwenyekiti alisema hadharani kwamba akianza mchakato huu wa el hakuna aliekua anajua ndani ya chama ila Maalim Seif Tundulisu anasema yake na Slaa anasema yake, nauliza nani anasema kweli?
3. Kama ni kweli mchakato wakumleta EL CHADEMA ulikua umeanza kabla ya kura za maoni CCM je EL alikua msaliti ndani ya CCM.
4. Sitaki kuamini kama alivyosema Dr kwamba Naibu Katibu mkuu alimwambia kwamba jambo hili limeshaamuliwa usijisumbue, yaani dili teyari, gia imebadilishwa angani.
5. Tumeshuhudia Chacha Wangwe, Zitto, Mwigamba, Kitila watu, walioshinda kwenye kura za maoni wakaenguliwa na sasa Dr tunaambiwa ni wasaliti hakuna wasafi huko?
Mwisho kama EL akijitoa kwenye kinyang'anyiro au akishindwa nana atabeba lawama?
Kwanini kila anayetoa yake ya motoni anakua msaliti, ndio demokrasia hiyo?