Mkuu wangu KK. Lowassa ana makosa yake kama mwanadamu yeyote,lakini maoni ya wanasiasa muflisi kutuaminisha Watanzania kwamba yeye ndiye tatizo na tuko hapa kwasababu ya Lowassa nayakataa kwa nguvu zote! Hawa wanasumburiwa na uwoga maana hawana mafanikio yeyote wanaweza kuonyesha ktk utendaji wao ktk serikali na chama kujilinganisha na Lowassa. Toka kesi ya fidia ya Dowans ambako tutalipa mabilioni ya shilingi kwasababu ya vita ya makundi hasimu ndani ya CCM kugombea madaraka huwezi niaminisha tena kwamba ndani ya CCM kuna viongozi wanapambana na ufisadi. Wote hawa ni mafisadi. Tena heri ya Lowassa alikubari kuwajibika kwa makosa ya chini yake.