Nani ni jasiri kama DED&RAS Kagera?

Nani ni jasiri kama DED&RAS Kagera?

Kila nikitafakari sipati picha!ni ujasiri ulioje?hivi dhahama la tetemeko la ardhi serikali ikafungua akaunti maalum ya michango kusaidia maafa Kagera....

Then kuna ndugu wajasiri wao wakafungua ya kwao inafanana na ile akaunti maalum wapige mpunga!zama hizi huu ujasiri unatoka wapi?kila kukicha nchi hii haikosi maajabu....hii inadhihirisha yafuatayo;

1.Kuna waungwana ni majasiri kupita maelezo yaani anaweza mkaba roba simba dume kavukavu.
2.Tulikua tunapigwa sana wakati wa kuchangia maafa..kupita kiasi
Hivi apa mkuu wa mkoa anaponaje ? Au yeye kazi yake ni kusimamia nini zaidi mkonani ?
 
Kila nikitafakari sipati picha!ni ujasiri ulioje?hivi dhahama la tetemeko la ardhi serikali ikafungua akaunti maalum ya michango kusaidia maafa Kagera....

Then kuna ndugu wajasiri wao wakafungua ya kwao inafanana na ile akaunti maalum wapige mpunga!zama hizi huu ujasiri unatoka wapi?kila kukicha nchi hii haikosi maajabu....hii inadhihirisha yafuatayo;

1.Kuna waungwana ni majasiri kupita maelezo yaani anaweza mkaba roba simba dume kavukavu.
2.Tulikua tunapigwa sana wakati wa kuchangia maafa..kupita kiasi
Hizo ndo product za mafisiem
 
Bado mkuu wa Mkoa nae Shoka limekwisha kuwekwaa Tatizo hapo ni Lowassa kupokelewa Huyo KIJUU hata maliza mwezi atapangiwa kazi nyingine
Kwa Mjeda hagusiiiiii!! Akimtimua mje mniamshe wakuu!
 
Mijitu mingine bwana kazi ushabiki tu hivi unauhakika subiri uchunguzi ufanyike,ndiyo maana mkuu mwenyewe kasema vyombo vya ulinzi vichunguze,sasa wewe pelelepelele
Wapigaji wanachama chao kumbe!
Mtoa mada kawashika pabaya'eh! Mbona mmecharuka kwa mambo madogomadogo yanayozungumzika? Kwa hiyo mambo ya watuhumiwa hayazumgumzwi?
Kama ni hivyo tungepataje taarifa za mijizi hiyo?
Tetea tetetetete! vimbisha misuli ya shingo lakini kumbuka hao jamaa zako majizi ya mkoani Kagera,hata wakipatikana na hatia kamwe hawataitwa wezi, bali wataitwa wafungwa.
Ni muda gani sasa sisi tuliokerwa tutaweza ku-express na kutaja waziwazi sifa za hao watuhumiwa kuwaita wezi?
 
Kwa Mjeda hagusiiiiii!! Akimtimua mje mniamshe wakuu!
Utaamshwa nakwambia. Wiziwizi awamu hii haunaga cha mjeda wala ndugu mheshimiwa katika kutumbuliwa. Kamuulize Kilango! Tangia enzi za mwalimu, hadi awamu ya 4, hangeweza kufumuliwa "fumu"namna hiyo, kutokana na hadhi ya mmewe katika nchi hii.
Badala yake angehamishwa ama,ungepitishwa uchunguzi magumashi kuua tuhuma.
Kwa hili la Kagera, labda kweli asiwe amehusika moja kwa moja,aidha kwa uzembe wa aina yoyote ile ama kwa hila kuruhusu kashifa hiyo itendeke.
Yeye kama mkuu wa kaya ya mkoa alitakiwa kuchukua hatua madhubuti mapema, kabla ya mamlaka za juu yake kuliona na kuchukua hatua. Haiwezekani baba yako atoke nyumbani kwake kuja kukueleza wizi uliofanyika nyumbani kwako,wakati wewe ukawa hauelewi chochote! Haiwezekani.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom