Nani Msafi

Lawkeys

JF-Expert Member
Nov 16, 2009
1,118
287
Nimekuwa nikifuatilia threads za michango mbalimbali ya wanazuoni hapa jamvini. Nimeshuhudia watu wengi kwamba wanaitakia meme nchi yetu. Watu wanajazba kali dhidi ya ufisadi, rushwa na ubadhilifu wa mali za uma.

Lakini bado nina wasiwasi kama kweli kuna msafi. Ni rahisi sana kuvutwa na msukumo wa kimapinduzi wa Libia na Misri, tukatamani hiki kibunga kipitie na kwetu huku. Shaka yangu juu ya Misri na Libia na sehemu nyingine dunia ambako kimbunga Karevolution kinapita, kwamba hivi watu wanasukumwa na nia ya dhati ya mabadiriko? au tu ni kama kipindi cha mkoloni kwamba, tukamwondoa lakini tulifanikiwa tu kubadilisha rangi ya mnyonyaji.

Una hakika gani kwamba aliyeshika bango "tumechoka na ufisadi" kwamba yeye msafi. Nadhani tunapo yaona hayo tufanye mabadiliko kwanza ya nafsi. Hata kutumia muda vibaya kijiweni huo pia ni ufisadi. Tusije tukawa mafisadi kasoro nafasi. Kabla ya kufikiria ya Misri fikiri ya nyumbani kwako, mfano, unapo toka nje ya ndoa yako, unapomdhulumu mtu haki yake, huo ni ufisadi tu.

Ufisadi, nina hakika haukui, ila nafasi ya kufanya ufisadi mkubwa ndio inaongezeka. Hivyo fisadi dagaa na fisadi papa hawana tofauti isipokuwa tu kwa kina cha maji wanapo ogelea. Most of us we are corrupt minus opportunity. Sasa, unapochangia thread za kimapinduzi usisahau mapinduzi yako binafsi.

Tusishabikie tu! Kwamba tufanye ya Misri, hapana! Una uhakika kwamba fisadi dagaa akipelekwa kina kirefu hatakuwa Papa huyu.

Challange kwako mwanamapinduzi. Usnikoti vibaya hapa. Ninataka mapinduzi ya kweli na mimi pia..
 
Nimekuwa nikifuatilia threads za michango mbalimbali ya wanazuoni hapa jamvini. Nimeshuhudia watu wengi kwamba wanaitakia meme nchi yetu. Watu wanajazba kali dhidi ya ufisadi, rushwa na ubadhilifu wa mali za uma.

Lakini bado nina wasiwasi kama kweli kuna msafi. Ni rahisi sana kuvutwa na msukumo wa kimapinduzi wa Libia na Misri, tukatamani hiki kibunga kipitie na kwetu huku. Shaka yangu juu ya Misri na Libia na sehemu nyingine dunia ambako kimbunga Karevolution kinapita, kwamba hivi watu wanasukumwa na nia ya dhati ya mabadiriko? au tu ni kama kipindi cha mkoloni kwamba, tukamwondoa lakini tulifanikiwa tu kubadilisha rangi ya mnyonyaji.

Una hakika gani kwamba aliyeshika bango "tumechoka na ufisadi" kwamba yeye msafi. Nadhani tunapo yaona hayo tufanye mabadiliko kwanza ya nafsi. Hata kutumia muda vibaya kijiweni huo pia ni ufisadi. Tusije tukawa mafisadi kasoro nafasi. Kabla ya kufikiria ya Misri fikiri ya nyumbani kwako, mfano, unapo toka nje ya ndoa yako, unapomdhulumu mtu haki yake, huo ni ufisadi tu.

Ufisadi, nina hakika haukui, ila nafasi ya kufanya ufisadi mkubwa ndio inaongezeka. Hivyo fisadi dagaa na fisadi papa hawana tofauti isipokuwa tu kwa kina cha maji wanapo ogelea. Most of us we are corrupt minus opportunity. Sasa, unapochangia thread za kimapinduzi usisahau mapinduzi yako binafsi.

Tusishabikie tu! Kwamba tufanye ya Misri, hapana! Una uhakika kwamba fisadi dagaa akipelekwa kina kirefu hatakuwa Papa huyu.

Challange kwako mwanamapinduzi. Usnikoti vibaya hapa. Ninataka mapinduzi ya kweli na mimi pia..
Uko sahihi. Lakini ili siyo swala la imani. Hatuwezi kungoja wote waokoke ili sote twende pamoja peponi. Kama wachache wenye mwamko wanaweza kuleta mapinduzi hakuna haja ya kuwangoja ndumila kuwili. Tutawashughulikia baada ya kuidhibiti mbingu.
 
Uko sahihi. Lakini ili siyo swala la imani. Hatuwezi kungoja wote waokoke ili sote twende pamoja peponi. Kama wachache wenye mwamko wanaweza kuleta mapinduzi hakuna haja ya kuwangoja ndumila kuwili. Tutawashughulikia baada ya kuidhibiti mbingu.
Usijidanganye kuwa unaweza kufanya mapinduzi then ukajiuliza what is next.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom