Nani kasema siasa na dini zinakinzana?

sulphadoxine

JF-Expert Member
Nov 1, 2010
2,257
644
Zaidi ya miaka 100 iliyopita, mwanaharakati wa siasa za mapambano, Karl Marx, alidai kwamba, “dini” ni bangi inayolevya na kupumbaza watu, wasiweze kujua adui wao wala kupigania haki zao.

Kwa mtazamo huo, Marx aliona dini kama taasisi inayopinga mapinduzi ya wanyonge, wenye kuonewa na kunyanyaswa, akatangaza vita dhidi yake.


Ni kwa sababu hii, mpaka leo dini [kanisa] havikai meza moja na itikadi za ki-Karl Marx, kwa maana ya Ukomunisti na dhana zingine za kimapinduzi za mwanadamu duniani.

Kabla ya hapo, zaidi ya miaka 2000 iliyopita, mwasisi wa Ukristo, Yesu Kristo [Nabii Issa], wakati akijibu mashtaka dhidi yake kwenye kesi ya uhaini, kwa tuhuma za kutaka kupindua Serikali ya Kaisari, alipewa mtego, aeleze ni kwa mamlaka yapi alielekeza utii wake; naye akajibu,“Cha Kaisari apewe Kaisari, na cha Mungu apewe Mungu”.

Hapo ndipo ikazaliwa dhana ya kutochanganya dini na siasa, tafsiri ambayo imewasilishwa kwa kupotoshwa katika jamii mara nyingi.


Katika makala haya nitatumia neno “kanisa” kumaanisha jumuiya za waumini wa dini mbali mbali katika jamii pana inayotawaliwa, bila ubaguzi wa ki-madhehebu.

Kwa kifupi, kanisa ni waumini wa dini chini ya madhehebu mbali mbali, na si majengo ya kuabudia kwa madhehebu fulani fulani tu.


Kwa Karl Marx, dini na kanisa vilikuwa ni vyombo vya watawala na wenye elimu, vilivyotumika kuwakandamiza na kuwaogofya

[juu ya moto wa milele], kuwadhibiti na kuwapumbaza wanyonge kwa ahadi ya “ufalme wa mbingu”, kwa kujikana wenyewe ili wasielewe chanzo cha matatizo yao yenye kusababishwa na binadamu wenzao.

Kilicho wazi hapa ni kwamba, upofu wa Karl Marx haukuwa juu ya dini, bali ugomvi wake ulikuwa juu ya watawala na mwenendo wa Kanisa kwa kutekwa na ubinafsi wa watawala, wakachanganya dini na utawala kuzaa kinachoweza kuitwa taifa na utawala wa Kiotheokrasia, kwa maana ya Taifa kuongozwa kwa misingi ya kidini, au Serikali ya makasisi.

Wapo waliomtangulia Karl Marx ambao waligundua udhaifu huo wa Kanisa pekee la Roma la wakati huo [lililotekwa nyara na watawala tangu enzi za Mfalme Constantine wa I], lakini hawakushambulia dini, badala yake walishinikiza kufanyika marekebisho katika mfumo na mwenendo wa Kanisa bila kuathiri imani na nafasi ya dini katika jamii.

Hawa ni pamoja na Mchungaji Martin Luther [1483 – 1534] aliyeanzisha Tawi la Kilutheri la Kanisa la Roma; Mfalme Henry wa VIII wa Uingereza aliyejiengua na kutangaza Kanisa lake la Anglikana; na John Calvin [1509 – 1547] aliyebuni mapokeo ya Ki-Kalvin, kwa kutaja matukio machache tu.

Wakati wa enzi za Karl Marx, kulikuwa na dini kuu mbili za Kimataifa yaani, Ukristo na Uislamu. Misahafu ya dini hizi ni Biblia [Ukristo] na Kurani kwa Uislamu. Kinyume na fikra za Karl Marx, misahafu yote miwili inatetea wanyonge na kupiga vita uonevu, ukandamizaji na unyonyaji, na kutoa wito kwa wanaoonewa kuasi dhidi ya vyanzo vya uovu na maovu. Kama Marx angeisoma vyema misahafu hiyo miwili bila kuyumbishwa na matendo ya watawala walioliteka Kanisa, wakaitumia dini kwa manufaa yao, bila shaka asingejenga uhasama na ukinzani kati ya falsafa yake na dini, badala yake angekuwa mtetezi mkubwa wa dini na Kanisa.

Tuchukue mfano wa uanaharakati na uanamapinduzi wa Kristo: Kuna wakati Kristo alizua ukinzani na watawala kwa kuwataka wajisafishe kwa maovu, uonevu na dhuluma kwa wanyonge, kitendo kilichosababisha akamatwe na kusulubiwa kwa tuhuma za kuchochea maasi dhidi ya utawala wa nchi. Kati ya wanafunzi wake 12, wawili kati yao, Simon na Yuda, kabla ya kumfuata, walikuwa wanaharakati, wakereketwa [zealots] wa haki na wapiganaji dhidi ya utawala wa kikoloni wa Kirumi nchini Uyahudi.

Uanamapinduzi wa Kristo unathibitishwa pia na maneno kama, “Nimekuja kutupa moto duniani”; au, “Sikuleta amani, bali upanga” [Luka 12: 49 – 53] kwa maana ya mapambano ya ana kwa ana dhidi ya udhalimu katika jamii.

Na kwa sababu jamii ya wakati huo ilikuwa imejaa maovu, kama ambavyo Taifa letu linaelekea kugubikwa na rushwa kubwa na ufisadi, palitakiwa wachache kujitoa mhanga kwa manufaa ya walio wengi kama yeye alivyojitoa. Na ili kufanya hivyo alisema, “Mtu ajikane mwenyewe na anifuate”. Hata siku ya kusulubiwa kwake msalabani, hakujutia vita aliyoianzisha; akawaagiza wafuasi wake wauze kanzu [nguo] zao, ili wanunue mapanga kuendeleza harakati za kuwakomboa wanyonge.

Kuhusu utajiri wa kinyonyaji, aliwaonya watawala wenye uchu wa kutajirika, kwamba hawawezi kutumikia mabwana wawili, Mungu [watu] na mali [utajiri] bila kuteteresha ukweli na haki; akasema, ni rahisi ngamia [kamba nene, sio mnyama] kupita kwenye tundu ya sindano, kuliko tajiri [uchu wa mali] kuuona ufalme wa mbingu, kwa njia ya kutenda haki na kweli.

Aliwanyuka mijeledi wezi na wafanyabiashara, walioweka mbele maslahi yao binafsi kuliko utu, alipowakuta wakiuza bidhaa kwa ulanguzi hekaluni. Ikulu, kama lilivyo hekalu na msikiti ni mahali patakatifu; kwa sababu ndipo maamuzi makuu hutokea. Ni dhambi kubwa kwa wanasiasa, kama ilivyo kwa waumini kupageuza mahali patakatifu kuwa pango la walanguzi, kama alivyobaini Mwalimu Nyerere mwaka 1990, alipoona wafanyabiashara matapeli kuizoea Ikulu, Rais na familia yake.

Usawa wa binadamu katika jamii umesisitizwa vizuri pia katika Kurani tukufu kwa kuhusishwa na zaka [zakat] na sala kuwawezesha masikini kuendesha maisha mazuri kama binadamu wengine [LXX: 24 – 25].

Kurani tukufu inasisitiza pia juu ya utu na wajibu wa kila mtu kwa jamii [jamaa], mshikamano katika usawa, na ushirikiano kwa jamii nzima [XVII: 70].

Uislamu, kama ulivyo Ukristo, unasisitiza HAKI, wema, usawa na ukweli kwa watu wote, hata kama hayo hayatamfurahisha muumini mwenyewe, wazazi au ndugu zake [IV: 135].

Karl Marx hakuweza kuzitekeleza kwa vitendo nadharia zake, kwani alifia uhamishoni Uingereza kama mkimbizi na kuacha mabunda lukuki ya vitabu vya fikra zake.

Katika zama zetu hizi, je, dini ina nafasi yoyote katika maendeleo ya jamii au bado ni yale yale ya mtazamo wa Karl Marx? Nini chanzo na sababu za watawala kutaka viongozi wa dini wasichanganye siasa na dini? Ni kipi hicho kinachoitwa kuchanganya siasa na dini?

Ukichunguza kwa makini, utaona kuwa mambo yanayopigiwa kelele na viongozi wa dini, na ambayo watawala wanadai ni kuchanganya siasa na dini, ni pamoja na mambo kama: Tofauti
 
Hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.jpg Fashisti Adolf Hitler.jpg Karl Marx.jpg
j.k.nyerere fashisti adolf hilter karl marx
 
Kuna mambo inapaswa kuyaangalia kwa umakini na ndipo tunaweza kutoa comments zenye mshiko...mfano,ni kitu gani kinacholeta kutofautiana kati ya group moja na lingine katika kila nyanja ya maisha.....maana hata hao wakristo wanatofauti zao ambazo wakati mwingine zinaleta hata uvunjifu wa amani,kupitia kurushiana maneno nk...

Lakini pia uislamu pia una tofauti zake na mnakumbuka kwenye Idd juzi wengine walifungua mapema kuliko wengine mpaka Redio moja ya pale Morogoro(Radio Imaan) wakaingia katika mgogoro mkubwa na Bakwata...Tofauti za watu ni itikadi na sio sehemu walipo......Dini na siasa ni vitu vinavyotofautiana itikadi/unaamini nini? Ni kweli kuwa dini kwa kiasi kikubwa hata kipindi cha ukoloni karne ya 18 mpka 19 ilitumika kama silaha ya kuwagawa watu hasa waafrika kwa lengo la kuwatawala...

Lakini kwa mtu anayeijua dini vizuri,hasa ya ukristo(natolea mfano maana ndio nayoifahamu vyema) inaimiza watu kuwa wema kati yao,umoja,mshikamano nk..hakuna sehemu katika biblia ianyosema tuwatenge wasio waamini wa ukristo...

Sasa kipindi cha kristo aliposema ya "kaisari mpeni kaisari na ya Mungu mpeni Mungu" yatupasa kujua aliyasema haya akiwa katika mazingira gani na kwanini? swali hili lilikuwa ni mtego kwake,maana walikuwa wanataka kumfunga kwenye mtego wa kupinga serikali ya Rumi...na baada ya kujua janja yao akasema maneno hayo..kwa wale wasomi wa biblia wanajua hatua waliyochukua wale askari..kimsingi waliondoka kimya...

Kimsingi siasa ni mapambano na wakati mwingine hata vita ikibidi,japo uwa tunaficha ukweli huu kwa kusema siasa sio mapambano,na anayesema hivyo hajui siasa maana yake ni nini... Siasa ni matumizi ya mbinu mbalimbali hata ikiwezekana mapinduzi ili mradi upate dola,kwa maana hii ndogo tu uwezi ukaweka pamoja dini na siasa hata kwa dawa...

Ni kama maji na petroli, japo kwa upande mmoja dini inaheshimu siasa na Mtume Paulo aliwai sema wakati akiwaandikia Warumi.."Kila mtu anawajibu wa kuheshimu mamlaka iliyopo,maana imewekwa na Mungu..akaendelea kusema,maana watawala hawawatishi watendao mema bali wale waendao kinyume na mamlaka" Kwa mantiki hii naweza kusema itikadi ndio zinasababisha dini na siasa...

Nawakilisha mkuu...........
 
Nimesoma kitabu kimoja kinachoitwa VITA DHIDI YA UGAIDI kilichoandikwa na YERICKO Y. NYERERE Kuna sehemu amezungumzia "uhusiano wa siasa za dunia na dini" nitaomba ni nukuu andiko lake hapa:



UHUSIANO WA SIASA ZA DUNIA NA DINI:

Historia ya siasa duniani haitengani na historia ya dini. Vitu hivi vimekuwa sambamba na vyenye mafaa kwa jamii yoyote ile duniani, lakini vikileta matatizo makubwa sana katika baadhi ya nchi duniani, matharani ubaguzi wa kiimani umeleta machafuko na uharibifu mkubwa mali pamoja na mauti dhidi ya binadamu. Vitu hivi imekuwa ni vigumu sana kutenganisha katika dunia ya leo huku machipuko ya kiimani yakija kwa kasi ya ajabu. Kwa upande wa Tanzania mfumo wa siasa umekuwa ni wa kuakisi kutoka mataifa ya Magharibi, na uakisi wake umekuwa ni kinyume.

Tukiangalia historia ya binadamu tunaona yakuwa kabla binadamu hajajishughulisha na masuala ya siasa na utawala alikuwa anajishughulisha na maswala ya dini, binadamu akawa mcha-Mungu.Ulipofika wakati wa uteuzi wa kiongozi wa jamii mtu aliyeteuliwa kushika nafasi hiyo alikuwa ni yule aliyeonekana ni mcha-Mungu. Hata katika jamii zetu za kiafrika zilizotuletea kiongozi wa utawala, pia alikuwa kiongozi wa dini. Ni huyu aliyeongoza shughuli zote za utawala na za dini katika jamii.

Itatumika biblia kutoa mifano hai kuthibitisha uhusiano wa dini na siasa. Hakuna ubishi dunia inakubali yakuwa Yesu Kristo ndiye mwanzilishi wa dini ya kikristo. Hii ni kusema kuwa Yesu Kristo alikuwa kiongozi wa dini. Kwaupande wa kabila Yesu alikuwa Muebrania. Alipozaliwa nchini Uyahudi alikuta tayari watu wa kabila lake wanadini yao ya kiyahudi. Viongozi wa dini ya kiyahudi walikuwa pia watawala waliotawala kwa kutumia sheria za kiyahudi zilizomo katika kitabu chao cha sheria kiitwacho TORATI sheria hizo za dini zikawa pia sheria za utawala. Warumi walipoanzisha utawala wao, Wayahudi waliwaruhusu Warumi kufuata sheria zao za dini ambazo pia zilikuwa sheria za utawala wao wa jadi. Kuhani Mkuu ambaye alikuwa kiongozi mkuu wa dini, alikuwa mwenyekiti wa Baraza kuu la utawala lililoitwa Sanhedrin.

Ni baraza hilo ndilo lililotoa hukumu kuwa Yesu auawe (Math 26:65-69). Hata hivyo adhabu yoyote ya kifo iliyotolewa na baraza kuu la wayahudi ilibidi ithibitishwe kwanza na mtawala wa Kirumi kabla haijatekelezwa (Yohana 18:31). Kwa upande wa Yesu Kristo alipoanza kufundisha dini yake mpya alikosoa sheria za kiyahudi ambazo aliziona hazikuwasaidia binadamu kuishi kwa upendo na amani. Aliwataka wafuasi wa dini yake mpya wasiwe na tabia ya kulipa kisasi. Kwamfano sheria za kiyahudi zinasisitiza kauli ya jicho kwa jicho na jino kwa jino. Katika (Math 5:38-41) tunasoma yakuwa Yesu hakutaka sheria hizo, alisema, "Mmesikia kwamba imenenwa jicho kwa jicho na jino kwa jino, lakini mimi nawaambia msishindane na mwovu lakini mtu akupigae shavu la kuume mgeuzie na la pili na mtu atakaye kushitaki nakuitwaa kanzu yako mwachie na joho.

Uongozi safi wa kidini wa Yesu Kristu uliwavutia wayahudi wa kawaida hata wakaona anafaa kuwa kiongozi wa utawala, wakataka kumfanya awemfalme. Lakini Yesu hakuwa tayari kujiingiza mno katika masuala ya siasa na utawala (Yohana 6:15) alizoea kusema ufalme wake sio wa ulimwengu huu (Yohana 18:36) Katika mafundisho yake, Yesu hakuwahi kuwaambia wafuasi wake wasichanganye dini na siasa. Hata hivyo aliwataka wawe waangalifu katika kuyashughulikia masuala hayo mawili. Alisema,
"Ya Kaisari mpeni Kaisari na ya Mungu mpeni Mungu". (Luka 20:25). Hakuwahi kuwataka wafuasi wake washughulike na mambo ya mungu (dini) tu na wasijishughulishe na siasa. Katika hali hii niwazi kuwa kiongozi wa dini hatakiwi kuhubiri siasa katika jengo la ibada akaacha mambo ya mungu. Vilevile anapokuwa nje ya jengo la ibada hana mwiko wakutokuzungumzia masuala ya siasa na utawala. Baada ya kufa Yesu, wafuasi wake waliendelea kujihusisha na masuala ya dini na siasa, mambo ya utawala yakiendelea kuhusishwa na dini.

"Iliaminika kuwa mamlaka yote yanatoka kwa Mungu (Warumi 13:1). Katika hali hiyo kiongozi wa Katoliki duniani Papa wa Roma alipewa mamlaka makubwa ya utawala, eneo lake la Vatican likapewa hadhi ya utawala wa nchi. Eneo hilo likapewa mamlaka kamili yakupokea mabalozi wakigeni. Hatua hiyo ilichukuliwa kutokana na imani ileile iliyojengeka siku nyingi kuwa kiongozi wa dini ndiye anayefaa kuwa kiongozi wa utawala pia maana kwanjia hiyo atakuwa nanafasi nzuri ya kupambana na maovu. Lakini wakati Papa wa Roma anashughulikia zaidi masuala ya dini kuliko ya siasa na utawala, kuna viongozi wengine wa dini wamewahi kupewa madaraka kamili ya kushika utawala wa nchi. Mfano Askofu Mkuu Makarios wa kisiwa cha Cyprus ambaye aliwahi kutembelea Tanzania. Wakati huohuo kuna nchi duniani ziliamua siku nyingi kuwa nchi za dini mfano Uingereza ni nchi ya kikristo ambapo mishahara ya maaskofu hulipwa na serikali. Pia nchi za Saud Arabia, Moroco na Libya ni nchi za kiislamu. Si hivyo tu pia kuna nchi ambazo vyama vya siasa vya kidini vinaruhusiwa mfano Ujerumani Christian Democratic Union (CDU).

Kwa upande wa Tanzania nchi iliyozoea mapokeo, ni vigumu sana kupembua ni falsafa iliyotumika kutenganisha dini na siasa. Kwakuanzia watawala wetu, wameshikilia kuwa dini na siasa ni vitu viwili tofauti kabisa, wanasema tusichanganye dini na siasa. Wanasema nchi yetu takatifu haina dini lakini watu wake wanadini. Huu ni ulaghai wa kimtazamo na kifikra, itakuwaje nchi isiwe na dini halafu watu wake wawe na dini?. Kunaumuhimu gani wa kuiombea mema nchi hii inayoaminika kuwa mungu aliiteua kuwa kisiwa cha amani na utulivu duniani ilihali wakaazi wa nchi hii wako mlengo wa kushoto na minajili ya munyazi mungu. Inafahamika yakuwa dini ilikuwepo hata kabla ya Yesu kristu na Mtume S.A.W hawajazaliwa.

Kuna kitu kipo ndani yake, bora tuwe wawazi tuuambie umma kuwa Tanzania haina dini rasmi kama ilivyo na lugha rasmi ya Kiswahili. Fikra za Mwalimu J.K Nyerere na wasaidizi wake ni vigumu sana kubeza kwani zilichambuliwa kwanza kabla ya maamuzi na ndiyo maana zinakuwa na mafaa mbele ya Tanzania yenye mshikamano, upendo, amani, utulivu na isiyo na udini wala ukabila katika kizazi hiki cha nyoka. Inaaminika kuwa mfumo uliotumika katika jambo hili ni fumbo la imani, na ndiyo siri ya amani na utulivu wa kisiwa hiki ambacho hakijawahi kuonja mtutu wa bunduki tangu enzi za akina Kinjekitile na akina Mkwavinyika (Mkwawa) kwani hata uhuru ulipatikana kwa sound (demokrasia).

Inatia simanzi na kufanya nyoyo za waungwana ziende kasi kanakwamba mtoa rohokashagonga hodi, pale inapodhihirika kuwa wale wanazuoni tuliowapa kibali cha kusimamia lile fumbo la imani, wanasimamia kinyume na maagano ya Mtakatifu Julius K. Nyerere. (Nimtakatifu kwasababu zilizo wazi). Aliwaamini, aliwapenda, akawapa elimu yakimagharibi bure kwa jasho la wananchi, lakini leo wamemsaliti! Wanataka kujua nini kilicho ndani ya fumbo la imani! Wanataka kujua uimara wa imani ya mtanzania! Tuliwapeleka wakasome magharibi, tena kwakuuza migomba na kuku huku tukijitunuku mshikamano na umoja wetu tukitumia dhana ileile iliyotupatia uhuru ya hakuna udini wala ukabila, leo wanakuja kufanyia field (mafunzo kwa vitendo) kwetu tena katikati ya mwamko wakiimani ya kila mmoja. Kunaulazima wa kuwa na mahakama ya kadhi? Je mahakama zilizopo hazikidhi haja? Je kunaulazima wa mahakimu kujua biblia, au msahafu kuliko kujua sheria za nchi? Maswali yote hapo juu jibu lake wanalo wanazuoni.

Leo wanazuoni hawa wanajaribu kila liwezekanalo kuisilimisha Tanzania, kwa shinikizo la Maulamaa wa umangani!, hii ni aibu na fedheha kubwa, Majuto yapo kwa wananchi tuliotoa leseni kwa wanazuoni hawa kutuongoza Shime! Watanzania tufikiri kabla yakuridhia majaribio ya wanazuoni hawa. Lakini wanazuoni wajue kuwa imani ya mtu haijaribiwi. Inasadikika na kuaminika kuwa Tanzania kuna dini kuu mbili, ambazo ni Uislamu na Ukristo. Kinadharia na kivitendo hakuna dini ambayo ndiyo kioo cha Taifa kama ilivyo Lugha ya Kiswahili. Kujiunga na Jumuiya za Kiislamu (Afrika na Duniani) nikuzika umoja tulionao, Amani tuliyonayo na baadaye kuzalisha chuki na Udini ndani ya nyoyo zilizo katikati ya muhimili mkuu wa kiimani. Waislamu na Wakristo tusibariki majaribio haya, kwani wahanga wa machafuko ni makabwela, kwakuwa baada ya hali ya hewa kuwa mbaya, wanazuoni hawa utawaona wakiwa katika meza pana ya kutafunia kuku wakijinasibu kwa mapatano mseto, wakati tuliovunjika viuno tukiwa tunaugulia bila ruzuku wala kifuta jasho.

Kwanadharia hiyo wanazuoni wanaandika barua za kuacha kazi! Kwaheshima na taadhima, Nguvu ya umma izijibu barua hizo kwa kuweka ugoko juu ya mchakato mgando wa Kuisilimisha TZ.

Uwezo tunao, Nia tunayo na Sababu tunayo!!!!!!
 
Uislam ni mfumo pekee duniani ambao hautaji mfumo mwingine toka nje ya uislam ili utimie au ufanye kazi! ndiyo maana unasharia zake! upo wazi kiasi unafundisha jata jinsi ya kunya (oops!! Kujisaidia am sorry jamani) lakini huo ndiyo ukweli! Sasa anayejaribu kuuchanganya na hii mifumo mingine huyo atakuwa dhalili tu. OLE WAO HAO SHURA SIJUI ZA MAIMAMU, SJUI BASUTA, SIJUI, RADIO IMANI NA HAO WAKUBWA ZAO BAKWATA!! kujifanya kwao na mseto wa dini hii iliyokamilika na siasa za Tanzania.
 
Sometimes dhana ya Karl Marx ina mashiko flani!
Kikubwa ni kuwa waangalifu katika kuyashughulikia maswala hayo mawili.
 
Back
Top Bottom