Nani kaimba huu wimbo wadau....?

Nani kaimba huu wimbo wadau....?

orangutan

JF-Expert Member
Joined
Mar 21, 2014
Posts
756
Reaction score
775
Kuna wimbo mmoja wa zamani kidogo najaribu kuvuta kumbukumbu ya jina lake bila mafanikio. Ila bahati nzuri ninakumbuka baadhi ya mashairi yake (nadhani unamuhusu kinyonga ama chura-not sure);
"Mbona yeye hana mbawa,
anakula kwa ulimi wakeeeee, sembuse mimi mwanadamuuuu....."

Tafadhali wadau wa miziki mizuri naombeni sana jina la kibao hiki na kimepigwa na mwanamuziki gani. (tukiweza ku-upload hapa jukwaani itakuwa ni vyema sana). Waiting to hear from you!!!!!!!
 
Huo wimbo unaitwa MAZOEA YANANIKONDESHA, bendi iliyopiga wimbo huo inaitwa MZINGA TROUPE (kama sijakosea) ila mwanamuziki aliyeimba wimbo huo jina lake limenitoka kidogo na pia tayari ameshatangulia mbele ya haki.
 
Kuna wimbo mmoja wa zamani kidogo najaribu kuvuta kumbukumbu ya jina lake bila mafanikio. Ila bahati nzuri ninakumbuka baadhi ya mashairi yake (nadhani unamuhusu kinyonga ama chura-not sure);
"Mbona yeye hana mbawa,
anakula kwa ulimi wakeeeee, sembuse mimi mwanadamuuuu....."

Tafadhali wadau wa miziki mizuri naombeni sana jina la kibao hiki na kimepigwa na mwanamuziki gani. (tukiweza ku-upload hapa jukwaani itakuwa ni vyema sana). Waiting to hear from you!!!!!!!

Huo wimbo unaitwa MAZOEA YANANIKONDESHA, bendi iliyopiga wimbo huo inaitwa MZINGA TROUPE (kama sijakosea) ila mwanamuziki aliyeimba wimbo huo jina lake limenitoka kidogo na pia tayari ameshatangulia mbele ya haki.


Yeah uliimbwa na Mzinga Troupe. Wimbo mkali sana, aisee hadi leo ukiusikia utadhani ndio umetoka hivi sasa. Hii ndio raha ya nyimbo za kibongo enzi zile huwezi fananisha na Bongo flava zinazochuja very upesi.
 
Huo wimbo unaitwa MAZOEA YANANIKONDESHA, bendi iliyopiga wimbo huo inaitwa MZINGA TROUPE (kama sijakosea) ila mwanamuziki aliyeimba wimbo huo jina lake limenitoka kidogo na pia tayari ameshatangulia mbele ya haki.

mkuu thanks sana. nishaipata hiyo ngoma na naburudika si mchezo! kama unalipata jina la bendi iliyoimba ngoma nyingine ya kitambo nadhani inaitwa 'wema hawana maisha' . msaada plizz
 
Huo wimbo wa wema hawana maisha umeimbwa na Afro 70 band chini ya uongozi wake patrick balisidya.
 
Huo wimbo wa wema hawana maisha umeimbwa na Afro 70 band chini ya uongozi wake patrick balisidya.

thanks mkuu nimeshaupata. na hicho kibao kumbe kinaitwa 'mashaka na hangaiko'.
 
Kinachofanya nimuwazeeeee sio Sifa ya upole wake,walimwengu walitaka nitetelekeee,ona mjusi na kinyonga wanapata ridhiki yake tena ula vijidudu hai hashiki panga wala bunduki anakula kwa ulimi wake sembuseee Mimi mwanadamuuu mazoea yananikondesha.
 
Kuna wimbo mmoja wa zamani kidogo najaribu kuvuta kumbukumbu ya jina lake bila mafanikio. Ila bahati nzuri ninakumbuka baadhi ya mashairi yake (nadhani unamuhusu kinyonga ama chura-not sure);
"Mbona yeye hana mbawa,
anakula kwa ulimi wakeeeee, sembuse mimi mwanadamuuuu....."


Tafadhali wadau wa miziki mizuri naombeni sana jina la kibao hiki na kimepigwa na mwanamuziki gani. (tukiweza ku-upload hapa jukwaani itakuwa ni vyema sana). Waiting to hear from you!!!!!!!

 
MAZOEA YANANIKONDESHA EEE NIMPENDAE KACHUKULIWA EE MAMA AAA WALA SINA LA KUTAMKA WENYE NGUVU WAMENIRUDIA EEE WALA SINA VYA KUSHITAKI WENYE NGUVU WAMENIRUDIA EEE TULIISHI BILA MATATIZO OO NYUMBANI VITU TELETELE EEE WALLAHI OO KAMA MIMI NINA KASORO WANGU YEYE ANIJURISHE HOOO KWANI MMEZOEA KUNICHUKULIA NIMPENDAE DAIMA HAKUTENDA OVU WALA MM SIKUTENDA OVU LINI NAACHA MAKOVU KUTOKUSAHAU MILELEEE AAA SIKUTENDA OVU LA KUWEZA KULIPWA KISASI WALA HAKUTENDA OVU LA KUTOKUSAHAU MELELE OHOOO TULIISHI KWA MAPENDO MAMAA AAA.......KINACHOFANYA NISEMEEE SIO SIFA YA UZURI WAKE NO AMA SITOPATA ZAIDI YAKE A A A
Ama nimeshakula mizizi labda lakini siamini alijua matatizo ooo kweli nasema mtoto kalelewa kinachofanya nimuwazeeee sio sifa ya upole wake tuu ama sifa zake nyinginezo a a hapana alijua matatizooo kwa haki nasema mungu amjaalieee walimwengu mama dede walitaka nitetelekeeee
,ona mjusi na kinyonga wanapata ridhiki yake tena ula vijidudu hai hata vyenye kurukaruka mbona yeye hana mbawaaa hana makucha wala vifundo unamtosha ulimi wakeeee hashiki panga wala bunduki anakula kwa ulimi wake sembuseee Mimi mwanadamuuuuuu.... mazoea yananikondeshaaaaaaaeeeeee jamani.nifanye nini walimwengu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom