St. Paka Mweusi
JF-Expert Member
- Sep 3, 2010
- 7,638
- 4,522
Kama mada inavyojieleza. Sote huwa tunaumia tunaposalitiwa na wapenzi wetu. Utakuta nimemgharimia kumsomesha, kumsubiri amalize masomo na kuhakikisha anaishi bila ya matatizo. Anapomaliza bila aibu ananiambia wewe sio type yangu wala hukuwa chaguo langu .Kama gharama sema ni kiasi gani nikurudishie. Ukija upande wa pili nao utakuta msichana amemvumilia mwanaume toka hana kitu akampa upendo wa kweli na kumfariji mpaka mwanaume anafanikiwa kimaisha. Inapofikia wakati wa kuoa utasikia wewe hukua chaguo langu au wazazi wangu wamenitafutia mke kijijini. Hapa wote wawili mwanaume na mwanamke tunaumizwa. Sasa swali langu ni nani kati ya mwanaume na mwanamke anayeumia zaidi pale anapotendwa kwenye mahusiano? Na ni jinsia ipi inayoongoza kwa kuumizwa na wenzi wao? Binafsi niliumizwa na mrembo mmoja nikaapa kutopenda tena na nikaamua maisha yangu yatakuwa ya ulevi tu.