nani atafuata kutekwa nyara?

mpemba mbishi

JF-Expert Member
Nov 27, 2011
1,132
185
sasa hivi wimbi la kutekwa nyara kwa wanaharakati mbali mbali nchini likiwa linaendelea, ambapo alianzia kutekwa nyara dr steven ulomboka kwa kudai haki za madaktari, pia ametekwa sheikh farid. My take.... Je nani atafuata kutekwa nyara? Je sasa ni zamu ya wanasiasa? Na nini kifanyike kuzuia unyama huu ambao unaweza kumtokea mtu yoyote. Kama leo watu wanafurahi kutekwa nyara kwa dr ulimboka na sheikh farid, je wanasahau kuwa zoezi hili linaweza kugeuziwa wanasiasa? Je waliofanya vitendo hivyo watakuja pongezwa na kufurahiwa? Je hamjui kuwa munawapa nguvu watekaji? Nimesema haya kwa sababu wakati alipotekwa nyara dr ulimboka baadhi ya watu walipongeza na kufurahia, sasa alitekwa sheikh farid baadhi ya watu wapongeza na kufurahi. kama wewe ni mfuasi wa cuf au chadema unayafurahia haya, je watakapotekwa nyara viongozi wa vyama hivyo mutakuja furahi? Fahamuni kuwa siku adui huwa hana rafiki wa kudumu, bali wana maslahi ya kudumu. Tafakari chukuahatua. Jadili kwa hoja tukomeshe hili lisiendelee kutokea kwa wengine.
 
Fareed alijiteka mwenyewe.
Haihitaji degree kujua hili.

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
Mkuu watu wanapenda zaidi kujadli matukio na si wazo kama hili.Siku akitekwa mwanasiasa ndio utaona mjadala wake utakavyokuwa ila kwa sasa wengi wa watu hawaoni umuhimu mpaka litokee tatizo hilo.
 
Back
Top Bottom