mpemba mbishi
JF-Expert Member
- Nov 27, 2011
- 1,132
- 185
sasa hivi wimbi la kutekwa nyara kwa wanaharakati mbali mbali nchini likiwa linaendelea, ambapo alianzia kutekwa nyara dr steven ulomboka kwa kudai haki za madaktari, pia ametekwa sheikh farid. My take.... Je nani atafuata kutekwa nyara? Je sasa ni zamu ya wanasiasa? Na nini kifanyike kuzuia unyama huu ambao unaweza kumtokea mtu yoyote. Kama leo watu wanafurahi kutekwa nyara kwa dr ulimboka na sheikh farid, je wanasahau kuwa zoezi hili linaweza kugeuziwa wanasiasa? Je waliofanya vitendo hivyo watakuja pongezwa na kufurahiwa? Je hamjui kuwa munawapa nguvu watekaji? Nimesema haya kwa sababu wakati alipotekwa nyara dr ulimboka baadhi ya watu walipongeza na kufurahia, sasa alitekwa sheikh farid baadhi ya watu wapongeza na kufurahi. kama wewe ni mfuasi wa cuf au chadema unayafurahia haya, je watakapotekwa nyara viongozi wa vyama hivyo mutakuja furahi? Fahamuni kuwa siku adui huwa hana rafiki wa kudumu, bali wana maslahi ya kudumu. Tafakari chukuahatua. Jadili kwa hoja tukomeshe hili lisiendelee kutokea kwa wengine.