Nani anayechochea vurugu Zanzibar?

Nani anayechochea vurugu Zanzibar?

Mimi nnapendelea kila nchi iwe na himaya yake kamili, kila mmoja afahamu mipaka yake, utaifa wake, uzalendo wake, haki zake, mapato yake, tamaduni zake. Si kulazimishana.

Ningependela Serikali mbili zenye mkataba wa Muungano.
Ok shukrani lakini sasa hapo huoni unakiuka msimamo wa chamachako? Na huo msimamo wako si ndio ule wa ‘mkataba' wa Maalim.?
 
Ok vizuri sana ukhti sasa hapo si utakuwa kinyume na chama chako? Kwa hiyo hoja yako ni muungano wa mkataba kama wa Maalim au sio?

Chama changu kila mmoja ana mawazo yake na ndiyo maana saa hizi wengine wako bungeni wanalumbana kwa hoja. Wengine tunalumbana humu JF.

Warioba ni CCM asili na maoni yake zamani yalikuwa Serikali mbili, sasa tatu. Yuko huru, au Warioba siku hizi si CCM?
 
Ok shukrani lakini sasa hapo huoni unakiuka msimamo wa chamachako? Na huo msimamo wako si ndio ule wa ‘mkataba' wa Maalim.?

Ahali yangu kumbuka maneno haya ya Mh Ismail Jussa. '' NCHI NI KAMA NYUMBA na CHAMA NI KAMA DUKA. Unaweza badili biashara yoyote pale dukani na hata kuliamisha duka. LAKIN huwezi amisha Nyumba. Na mwenye akili timamu hawezi weka rehani nyumba kwa kukopa kilo mbili za sukari.

Nafikiri umenifahamu.

 
Kitu ambacho huwa sikielewi kwa CCM ni Dr. Shein/Seif Idd kutetea na ku-kampenia serikali 2 wao ni HAKI. Lakini Maalim Seif kutetea na kukampenia serikali 3 ni kuchochea vurugu na ni UHAINI. Kinana kutetea na kukampenia serikali 2 ni HAKI. Lakini UKAWA kutetea na kukampenia serikali 3 ni upotezaji na rasilimali bure na ni kukwamisha rasimu ya Katiba mpya. Hivi hawa CCM ni MUNGU. Mawazo ya CCM ndiyo sahihi 100% na hayahitaji kuhojiwa au kupingwa na kiumbe chochote kile? Naombeni wana JF mnisaidie maana huenda Tanzania tunatawaliwali na MUNGU CCM. No wonder ndio maana CCM wanasema kwamba UFALME WAO HAUNA MWISHO! (read CCM itatawala MILELE)
 
Chama changu kila mmoja ana mawazo yake na ndiyo maana saa hizi wengine wako bungeni wanalumbana kwa hoja. Wengine tunalumbana humu JF.

Warioba ni CCM asili na maoni yake zamani yalikuwa Serikali mbili, sasa tatu. Yuko huru, au Warioba siku hizi si CCM?
Warioba ni ccm lakini hajawahikusema yeye msimamo wake ni wa serikali 3, alichowakilisha ni maoni ya wananchilakini pia akasema siku ile bungeni kuwa kila mjumbe wa tume alibaki na itikadina imani yake kuhusu muungano kuwa kuna wanaoamini ktk S1, S2, S3 na hataMkataba. Na kama kila mtu ndani ya ccm ana mawazo yanayoheshimiwa mbona kakayangu Mh. Mansoor alisimamia ‘mkataba' mkamuadabisha?
 
Cuf na mbinu zao chafu hawataweza kuichafua zanzibar kwa namna yoyote ile.

Hata Tanganyika na mbinu zao chafu za kughushi signature hazita wazuia Wazanzibar kudai mamlaka kamili....
 
Unajua Zanzibar waandishi wa habari wakongwe wote ni PRO wa vyama vya siasa.
Ahmed Rajab, Hassan Khamis, Ali Saleh , pia akiambatana na huyu wa sasa wa Gazeti la Mwananchi Salma Said hao wote ni mfano wao!
So sio jambo la kushangaza kusikia akitoa tafsiri kama vile Kiswahili ni Lugha ya Family yake tu.
Ni sawa na huku Bara watu wanavolalamika waandishi wa habari wa magazet ya CCM.
Nimeshangaa pia kwamba analinganisha matusi Vs na kutishiwa mtu usalama wa maisha yake!

mada imekushinda sasa unaanza kuwajadili waandishi kama kwamba hayo maneno hayaja tamkwa....?
Kiongozi hoyote dunia hii anayezingatia misingi ya haki za binadamu na utawala bora hawezi kutamka kauli tata zenye kuleta tafsi tofauti kwa RAIA wake...
 
Ngoja nikajiridhishe kama haya aliyoyaandika huyu Ahmed ni sahihi kabla sijaandika mengi..

Ahmed anasema “Kuwashughulikia” maana yake ni kuwachukulia hatua zisizopendeza kama vile kuwatia ndani, kuwatesa au kuwafanyia mambo mengine ya kukirihisha.......

hii tafsiri sijui kaitoa wapi? kwa nini hakudhania kuwa kuwashughuikia maana yake kuhakikisha anawafikisha kwenye vyombo vya sheria?

Wewe itafsiri kama unavyopenda na iwe kushughulikiwa ni kuvalishwa nguo mpya, sasa kwa sababu gani iwapo kila mmoja ana uhuru wa kuchaguwa?
 
Hivi Makamu wa kwanza wa Raisi nchini Zanzibar, Maalim Seif, naye akisimama jukwaani na kuagiza kwamba wanaotetea muundo wa mbili nao washughulikiwe, hali itakuwaje? Je ikitokea kwamba Wazanzibari wengi hawapendelei huo muundo wa serikali mbili, huyo Balozi Idi atafanya nini...ataagiza washughulikiwe? Tuseme ukweli jamani, kwa misimamo kama hii CCM haiitakii mema nchi hii, how sad!
 
Faiza, kauli ya karibu na "Kumshughulikia" ni kama kusema "kukabiliana nae au nao" au kwa lugha za wenzetu "Deal with"... kauli hii haina maana hizo tu ambazo ahmed anataka watu waamini kama kutesa, kutia ndani n.k.......

Kauli kama hii inapotolewa na watu walio na mamlaka za kidola huwa inatafsifiwa mara nyingi kama jitihada za kuhakikisha sheria inafuata mkondo wake na kutimiza wajibu wa kisheria kutokana na watu kukiuka au kwenda kinyume na sheria.......

Kwa bahati mbaya kauli ya Balozi Seif hakuwa na maana ya njia ya sheria. Uliona wapi mtu kuchukuliwa sheria kwa kutofautiana kimtazamo?
 
Cuf na mbinu zao chafu hawataweza kuichafua zanzibar kwa namna yoyote ile.

Pengine Wazanzibari wengi wangetofautiana nawe na kutaka kuondowa CUF na kuweka CCM kwenye kauli yako!
 
Nawaomba waelewa wa protokali za zanzibar hasa kuhusu vyeo na madaraka (siniority) kati ya Maalim Shariff Hamad na Balozi Seif Idd. Nashindwa kuamini kama makamu wa pili anauwezo wa kimamlaka ya kumkemea makamu wa kwanza wa rais hadharani.

Kwani unafikiri CCM ilikubali Serikali ya Kitaifa, ni Wazanzibari walioamuwa hivyo unashangaa Makamo wa Pili, Haji Shaka (UVCCM) anaweza kufanya hivyo.
 
Unajua Zanzibar waandishi wa habari wakongwe wote ni PRO wa vyama vya siasa.
Ahmed Rajab, Hassan Khamis, Ali Saleh , pia akiambatana na huyu wa sasa wa Gazeti la Mwananchi Salma Said hao wote ni mfano wao!
So sio jambo la kushangaza kusikia akitoa tafsiri kama vile Kiswahili ni Lugha ya Family yake tu.
Ni sawa na huku Bara watu wanavolalamika waandishi wa habari wa magazet ya CCM.
Nimeshangaa pia kwamba analinganisha matusi Vs na kutishiwa mtu usalama wa maisha yake!

Kwani alietishiwa usalama wake nani? Mnatakiwa mfatilie mambo ili mjuwe nini kinachoendelea?
Bango linasema kuwa wasaliti wa wananchi , sasa msaliti ni nani iwapo kila mmoja anasema kuwa anasemea matakwa ya Wazanzibari?
 
wazungu na masheikh wakitiwa Tindikali wazenji wanasema ni wabara ndio wanachafua utalii ila hapo leo kumeshaonesha mwanga kama wazenji wenyewe ndio hushiriki haya matendo.

Ni kwelikabisa ni sisi wenyewe ingawa tunaweza tukawatuma watu watufanyie maovu yetu!
 
Faizy nenda Kibanda maiti uungane na Seif, na siju kama wazijui siasa za Zanzibar. We huoni Makamu wa 2 kumchukulia hatua Makamu wa Kwanza ni ajabu? Kwa siasa za Zenj si ajabu. Funguka
 
Back
Top Bottom