Sungurampole
JF-Expert Member
- Nov 17, 2007
- 984
- 205
Nani anaisimamia elimu ya Tanzania?
Kila kukicha nasikia mambo yanayonifanya niamini kuwa hatuna budi kujiuliza "Hivi ni nani haswa anayesimamia mwenendo mzima wa Elimu ya Tanzania, na kazi hii anaifanyaje?"
Miaka ya karibuni tumesikia kwa uchache(kumbukumbu zangu) haya:
Kufutwa masomo ya kilimo na biashara katika mitaala ya sekondari
Kufutwa kwa michezo shuleni
Kufutwa kwa mitihani ya kitaifa ya darasa la nne
Kufutwa kwa mitihani ya kitaifa kidato cha Pili
Kurudishwa kwa masomo ya kilimo na biashara katika mitaala ya sekondari
Kurudishwa kwa michezo shuleni
Kurudishwa kwa mitihani ya kitaifa kidato cha Pili
Hapa inaonekana wazi hatuna dira wala dhima inayotupa mwelekeo wa elimu ya watoto wetu na taifa tunalolitaka.
Swali-Hivi inawezekanaje haya kupita?
Hivi mchango wa wadau kama waalimu na wasomi wetu ulikuwa nini katika maamuzi haya?
Tufanye nini ili tuache kufanya elimu ya watoto yetu maabara ya majaribio?
Nawasilisha
Kila kukicha nasikia mambo yanayonifanya niamini kuwa hatuna budi kujiuliza "Hivi ni nani haswa anayesimamia mwenendo mzima wa Elimu ya Tanzania, na kazi hii anaifanyaje?"
Miaka ya karibuni tumesikia kwa uchache(kumbukumbu zangu) haya:
Kufutwa masomo ya kilimo na biashara katika mitaala ya sekondari
Kufutwa kwa michezo shuleni
Kufutwa kwa mitihani ya kitaifa ya darasa la nne
Kufutwa kwa mitihani ya kitaifa kidato cha Pili
Kurudishwa kwa masomo ya kilimo na biashara katika mitaala ya sekondari
Kurudishwa kwa michezo shuleni
Kurudishwa kwa mitihani ya kitaifa kidato cha Pili
Hapa inaonekana wazi hatuna dira wala dhima inayotupa mwelekeo wa elimu ya watoto wetu na taifa tunalolitaka.
Swali-Hivi inawezekanaje haya kupita?
Hivi mchango wa wadau kama waalimu na wasomi wetu ulikuwa nini katika maamuzi haya?
Tufanye nini ili tuache kufanya elimu ya watoto yetu maabara ya majaribio?
Nawasilisha