Nani aliidangaya CHADEMA?


Huyu Mbwambo kama wengi mlivyosoma uzi wake mrefu mtamwelewa ni wazi anakishabikia chama gani na ni kati ya wale wanaosemekana kulipwa kwa kueleweka udhaifu wao. Hawezi kudanganya popote kuwa mgombea wa chadema kwa maana ya ukawa hanadi sera za chama chake kila afanyapo mikutano ya kujinadi. Wote tunaona,kusikia na kusoma pia.Hivyo hivyo hawezi kusema chadema wameachana na kukemea ufisadi na wizi wa hela na rasmali za taifa na lipo pia katika ilani yao aisome na kuacha kuwaaminisha wananchi uongo. Hawezi pia kudai chadema inashabikia ukanda vinginevyo yeye ndie anaefanya hivyo kwani mgombea anaemshabikia wa chama chake wanatoka kanda moja pia. Hatuelezi ni kwa nini mgombea wake anakwepa kujinadi kwa jina la chama chake huku akijua yeye kama yeye hamiliki nchi na ametumwa na chama chenye usajili wa kudumu. Awaeleze watanzania mgombea wao atakavyotekeleza anayowaahidi watanzania ndani ya chama chake kwa mfumo walio nao ambao hana ubavu wa kubadilisha lolote na akabaki salama. Yote anayoeleza majukwaani yanaweza kutekelezwa na chama kilicho nje ya mfumo wao waite wapinzani au kama tungekuwa na mgombea binafsi na sio chama kinachoongoza nchi na serikali kwa sasa yaani ccm. Labda atuambie ccm yake kwa sasa imejiandaaje kulipa IPTL fedha zao kwani toka May mwaka huu wameshaleta barua ya kutaka kulipwa hela za tegeta escrow acc walizogawana eti sio za serikali. Tumeisoma wote humu humu Jf jukwaa hili hili. Naomba wananchi wenye uelewa na wanaotaka maendeleo ya nchi na mwananchi mmoja mmoja wampuuze huyu bwana na ushawishi wake usio na mwelekeo. MABADILIKO UKAWA UKAWA MABADILIKO.
 

Tena waambie mwenye kampuni yake ya IPTL ameshaitwanga serikali barua toka mwezi wa tano mwaka huu kutaka hela zake na faida zilizokuwa escrow account au awafikishe mahakamani.Zile fedha walimlipa Sigh kwa kuamini documents za kufodge na kisha kuzigawana mafisadi wote wakidai hazina mwenyewe. Kesi hii IPTL wanashinda asubu na mapema na walipwe gharama za kuendesha kesi.Watanzania fumbueni macho mkidanganyika na hadaa za Magufuli majukwaani mtataabika kwa miaka yote kumi atakayoongoza kwani kwa mfumo wa ccm hana ubavu wa kubadili lolote wala kutekeleza anayowaaminisha majukwaani kwa sasa.
 
Ujinga ni mwingi na Mara nyingi mjinga huona karibu nakubali kweli wana ukawa wengi ni watu wenye ufinyo wa mishipa ya kufikiri
 
Kamwe hukuwahi kuipenda na kuiunga CHADEMA ilipokuwa ikiibua hoja za ufisadi; iweje uipende na kuionea huruma ghafla leo inapopambana kuleta mabadiliko tuyatakayo nje ya ccm..??
Kwani CHADEMA ya zamani haikuwa inapambana kuleta mabadiliko?
 
Kura yangu kwa magufuli...wana ukawa lazima wajue kuwa lowassa hakuondoka ccm kwa kuwa ni mbaya. Ni kwa kuwa walimkata tu. Tatizo akili za nyumbu
 
Kinachokupa jeuri ya kuandika hivi ni hizo tafiti uchwara. Ila usisahau goodluck jonathan tafiti zilimpa 70%
Hiyo ni Nigeria brother, siyo tz ,- Tanzania na watanzania wanafahamu nani kiongozi na nani mpiga deal. Tarehe 25 ipo Karibu kura yangu kwa Magufuli mzee wa push up
 
Naiunga Mkono Makala Kwa 100%.Mimi Natamka Wazi Kuwa Lowassa Ni Fisadi Na Hafai Kwenda Ikulu.Mimi Binafsi Yangu Nimeshaamua Kura Yangu Kwa Magufuli.Tunataka Raisi Mchapakazi Sio Mchezadili
#hapakazitu
Plain and simple Lowassa hafai kuwa Rais wa Tanzania.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…