Nampenda Mume Wangu Lakini ananitenda

Nampenda Mume Wangu Lakini ananitenda

Mume Anitaki Tena Baada Yakupata Hawara Nifanyeje, Tumeoana miaka 4 Sasa,tuna Mtoto Mmoja Nanina Mimba Tena Hanijali, Hanipi Haki Yandoa Miez Miwili Sasa, Ananidharirisha Wamarafikize, Nakunisemea Uongo Kwawazaz Wake Ili Apate Sababu Japo Wakwe Wananijua Vizuri Kitabia, Nawanampinga Maana Wanamjua Tabia Yake

Pole sana dada,
Naelewa ni kiasi gani unavyopata shida kulea mwenyewe mzigo mlioutafuta pamoja huku mwenzio akikusaliti. Jipe moyo na kufanya kilicho sahihi. Mungu atakusikia na atakupa faraja kwa unayoyapitia. Pia msamehe mumeo inawezekana ni tatizo la kisaikolojia ndio maana hawezi kushiriki na wewe na kupeleka kwa wengine (Sina maana kwamba ni kawaida ama ni sawa ila ukimuelewa itasaidia afya yako na ya mwana ajaye). Jaribu tu kuelewa kisichoeleweka kwa ajili ya afya bora ya mama na mtoto wake, It is tough to be a mother. Ni kitu ambacho wanaume wengi hatukielewi lakini ni kazi kuwa mama (Blessings to all mothers!)

Kiukweli ingekuwa bora kama ungemuomba mama mkwe ukaishi kwao walau nyote mshirikiane kumlea ajaye, au kama inawezekana umualike mkweo hapo kwenu... Inawezekana mwanaye akatulia kwa kumuogopa mamaye.
 
Ndoa tamu jamani hasa ikiwa na mikiki mikiki na furaha kidogo,lazima mpimwe imani bila kupimwa imani mtajuana vipi kama mnamapenzi ya kweli na mko ngangali..hayo ni mapito tu bidada yataisha na utasahau na utajiona bora kuliko wote.
 
Mawahara ni tatzo sugu ktk ndoa nyingi.muombe Mungu tu ndio muweza wa yote.
 
hivi huko kwenye ndoa kunanini mbona kila anaeenda anarudi na kitambaa kimeloa machozi tena vyote vya rangi moja?
 
ushauri we mpe ngumu.... maana kama wewe anakutesa na ww bado unanyenyekea ndo mwenzako anazidi kkfanyia maana anaona huna la kufanya..... ila ukimpa ngumu kama ukaenda kwenu kwa muda, haumtafuti kwenye simu wala wapi yani unakata mawasiliano nae... yeye mwenyewe baada ya muda utamuona na wewe hapo ndo unakuwa kichwa juu yake.. ila fanya kwa kumrekebisha sio kumkomoa na kumtesa kama unapenda
 
haya manaume haya basi tu mungu ayasaidie......>
.......Don't generalize lady in action!.

Mpe ushauri nini afanye katika hali aliyokuwa nayo na sio kuzidi kulalamika sehemu ambapo unaweza kumpa mwenzio A,B,C,D akapata pa kuanzia kutatua tatizo linalomkabili.

Wanaume ndo baba zetu na wanawake ndo Mama zetu, unapoweka general comments kwa wanaume wote maana yake unareflect pia kwa baba ako au baba zetu the same kwa wanawake.

Nachoweza kusema kwa sasa ni kumpa pole muathirika wa tukio, aangalie constructive advices wadau watakazotoa na ajue hilo tukio sio mwisho wa ndoa au maisha yake maana tatizo halitatuliwi kwa kulikimbia bali kutafuta njia sahihi ya kukabiliana nalo bila ya kusababisha madhara kwa pande zote.

Mungu ampe ujasiri na naamini atamsaidia kufikia suluhisho jema katika kuokoa ndoa yake.

.......Ni mtazamo tu! na neno langu sio sheria.
 
Sikia nikwambie Ndugu yangu kurud kwenu sio solution but nikujiongezea matatizo ,tafuta watu wa karibu uwashirikishe then uone itakavyo Kuwa, ila zidisha maombi
 
hivi huko kwenye ndoa kunanini mbona kila anaeenda anarudi na kitambaa kimeloa machozi tena vyote vya rangi moja?

asilimia kubwa tuliolewa
wanatoka kwao wanene wazuri
wakiingia baada ya mda unakua english figure
baadae unanenepa unakua ushazoes shida then unaanza kua mteja wa dawa za sukari na presha
au la uwe na roho ngumu
 
Pole sana kwa unayoyapitia,hiyo ni mitihani tu jipe moyo utashinda, kwasasa jali hali uliyonayo,jiepushe na stress wala usishindane naye kwa lolote mwache afanye yake ila yupo ambaye ni rafiki kwetu na msaada tunaposhindwa mueleze yeye mshitaki kwa baba yako wa mbinguni,muombee akutane naye hakika ni mwaminifu atambadilisha.

Kama ukishindwa kabisa kuendelea kukaa naye basi nenda kwao,kama ni wakarimu endelea kukaa mpka utakapojifungua,kama hakieleweki nenda kwenu ila uachane nao kwa wema.
 
asilimia kubwa tuliolewa
wanatoka kwao wanene wazuri
wakiingia baada ya mda unakua english figure
baadae unanenepa unakua ushazoes shida then unaanza kua mteja wa dawa za sukari na presha
au la uwe na roho ngumu

Umesema kwwli ukifaulu lazm uugue kisukar madonda ya tumbo ni htr sana
 
Mume Anitaki Tena Baada Yakupata Hawara Nifanyeje, Tumeoana miaka 4 Sasa,tuna Mtoto Mmoja Nanina Mimba Tena Hanijali, Hanipi Haki Yandoa Miez Miwili Sasa, Ananidharirisha Wamarafikize, Nakunisemea Uongo Kwawazaz Wake Ili Apate Sababu Japo Wakwe Wananijua Vizuri Kitabia, Nawanampinga Maana Wanamjua Tabia Yake

Ana hawara nawewe unajua?

Nafsi ishabebwa hiyo sasa wewe kaa unalia hapo instead of kufanya toba na maombi ya kurudisha nafsi
 
Mume Anitaki Tena Baada Yakupata Hawara Nifanyeje, Tumeoana miaka 4 Sasa,tuna Mtoto Mmoja Nanina Mimba Tena Hanijali, Hanipi Haki Yandoa Miez Miwili Sasa, Ananidharirisha Wamarafikize, Nakunisemea Uongo Kwawazaz Wake Ili Apate Sababu Japo Wakwe Wananijua Vizuri Kitabia, Nawanampinga Maana Wanamjua Tabia Yake

we vumilia tu usilalamike sana ulikubali mwenyew utakubali kuishi kwenye shida na raha au umesahau
 
asilimia kubwa tuliolewa
wanatoka kwao wanene wazuri
wakiingia baada ya mda unakua english figure
baadae unanenepa unakua ushazoes shida then unaanza kua mteja wa dawa za sukari na presha
au la uwe na roho ngumu

Mhh! Wengine hatujitangazi tu lakini .......... tumepitia shida ngumu ngumu zisizo na mfano. Likikukuta ni kukaza moyo tu, mradi maisha yaendelee. Hakuna shortcut juu suala hili.
 
Yakiwashinda ndo mwaleta hapa, kabla ya hapo ni fb tu
 
hivi huko kwenye ndoa kunanini mbona kila anaeenda anarudi na kitambaa kimeloa machozi tena vyote vya rangi moja?
Yaache tu ndugu ingia ukutane nayo na ukikutana nayo pamban kweli kweli yaani had ukifikia kikomo ukasema bas mikono juu hakuna anayekulaumu ila ndoani kuna mengi san ikiwa hujaingia huwezi jua hata moja utaona kila ndoa ina furaha na kwa nini wew umechelewa kuipata hiyo furaha kikubwa ni kuomba mungu tu ukutane na changamoto utakazoweza kuzitatua nikisema uombe mungu usikutane nazo nitakuwa nadanganya kiukweli ndoa zina mengi wajameni kikubwa ni kupambana omba mungu dad mumeo abadilike amani iwepo ndoani kwenu naishia hapo tu
 
Back
Top Bottom