nimetokea kumpenda sana kijana mmoja hivi kiasi cha kutamani awe mume wangu! ana qualities zote ninazozitaka na ameshika dini pia. tatizo ni kwamba nimekuwa nikimpenda muda mrefu sana lakini kutokana na tamaduni nikashindwa kumweleza. nikapata tetesi kwamba ana mpenzi tayari lakini sikuamini maana alikua ana dalili za kunipenda pia. nilipomuuliza akaniambia ndio anaye mpenzi japokuwa ananipenda lakini hawezi kumuacha maana sio playboy.naumia sana kumpenda huyu kiumbe ambae sina uhakika kama atakuja awe wangu. sitamani mwanaume yeyote ila yeye tu. na yeye ananipenda pia lakini ndio hivyo ameshaingia kwenye relationship. nina mtu mwingine ananipenda sana lakini sina feelings zozote juu yake japokua ana nia ya kunioa. nifanyeje jamani??? naogopa kuolewa na nisiyempenda na pia naogopa kuendelea kumsubiri huyo ninaempenda maana sina uhakika kama atakuja kuwa wangu.