Naomba niongee kuhusu vijana wanaomaliza kidato cha sita na kupangiwa kwenda mafunzo ya JKT kwa mujibu wa sheria, sikatai ni kweli wanaenda kufundishwa mafunzo ya awali ya ulinzi na usalama pamoja, uzalendo na uzalishaji mali lakini tija ya maarifa wanayoyapata vijana hawa imeshindwa kabisa kutatua tatizo la ajira Tanzania.
USHAURI WANGU
Ningependa kuishauri serikali kuwa pindi vijana wale wanapomaliza kidato cha sita wakiwa wanasubiri matokeo, ingekua na matokeo chanya sana kama wakati wachache wamepangwa kwenda JKT bhasi wengine wengi wangepelekwa VETA na kwenye taasisi nyingine za UFUNDI, USUSI, UVUVI, UFUGAJI NA KILIMO pamoja na tassisi zingine nyingi kwa kufanya hivi tungejikuta tunatengeneza taifa lenye vijana wenye maarifa tofauti tofauti na mwisho wa siku wanapohitimu vyuo vikuu wakaweze kujiajiri wao na kuajiri wenzao kutokana na maarifa walioyapata kipindi wapo VETA na kwenye taasisi nyingine nyingi walizokua wamepangiwa kuliko kupanga kwenda JKT tu ambapo kwa miaka miki toka kuanzishwa kwa mfumo huu pameshindwa kikubwa kuwapa vijana maarifa ya kutosha ili kutatua tatizo la ajira.
Nawasilisha
View attachment 1857743