Namna ya kuisaidia tanzania

George Kahangwa

JF-Expert Member
Oct 18, 2007
547
147
Wakuu,
Mara kadhaa nimekuwa nikiwaza ni kwa namna gani taifa letu la Tanzania tunaweza sisi wenyewe watanzania tukalikwamua katika hali duni ya kiuchumi, pengine hata kijamii na kisiasa. Yamkini wenzangu nanyi mmekuwa mkiwaza juu ya jambo hili. Ni wakati mzuri basi tukashirikishana mawazo juu ya kile tunachoona yafaa kifanyike ili Tanzania 'ipone'

Binafsi nadhani mojawapo ya yanayohitajika ni kuwepo 'mhamo luwaza' kuhusu siasa.
Tanzania, ni moja kati ya nchi ambazo zimeweka raslimali zake nyingi na muhimu katika siasa. (hili kwa mtazamo wangu, ni kosa). Tunatumia fedha nyingi sana katika mambo ya bla bla za kisiasa, na mifano ya hilo si haba; angalia maslahi ya wanasiasa ukilinganisha na maslahi ya wataalam, angalia gharama za kampeni za kisiasa ukilinganisha na gharama za kampeni kama za vita dhidi ya ukimwi na nyinginezo, angalia ruzuku ya vyama ukilinganisha na ruzuku za taasisi za utafiti au sekta nyeti, etc.

Mbaya zaidi, kila uchao viongozi wetu wanawaza namna ya kuongeza gharama za kisiasa (mf.hivi karibuni zimekuwepo habari kuwa tume ya uchaguzi-NEC, itaongeza majimbo mengine 10 ya uchaguzi!)

Nadhani namna mojawapo ya kuisaidia nchi yetu, ni kuondoa sehemu kubwa ya keki ya taifa iliyoelekezwa katika siasa, badala yake ipelekwe katika sekta za kiutaalam. Kwa kufanya hivi, tutasaidia taifa kwa namna nyingi, ikiwa ni pamoja na kukomesha wimbi la wataalam, wasomi na watu wa kada mbali mbali kukimbilia siasa badala ya kutumia utaalam wao mahali panapostahili na wanakohitajika zaidi.

Watanzania wamefika mahali wanafanya kila linalowezekana (hongo,ushirikina,etc) ili wapate nafasi katika siasa, hii si kwa sababu nyingine bali mnofu mnene ulioko huko. Ni wakati wa kuhamisha mnofu huo.
 
Kahangwa

Hakika umefikiri zaidi, ni kweli kuwa serikali yetu imejielekeza katika hayo uliyosema, na ndiyo mtizamo wa serikali iliyoko madarakani, mimi kwa mtizamo wangu nadhani itakuwa vigumu kuishauri serikali iliyoko madarakani kuachana kile inachookiamini kwa sasa.
Kahangwa nadhani ingekuwa busara tufikiri kupata serikali mpya jambo ambalo ni gumu mno, lakini kama watanzania tukiazimia wote hakika tunaweza, tupate serikali itakayowasikiliza wananchi wake na kuwajali.

Kahangwa itakuwa vigumu sana kutoa ushauri kwa serikali inayodhani kuwa iko sawa,
 
Namna kuisaidia Tanzania kikwelikweli!
1. Futa bunge kwa miaka ishirini...utakuwa ume-save pesa nyingi sana kama malipo ya wabunge, posho, uchaguzi hizo pesa zote ambazo zingetumika huko ...jenga vyuo vikuu kila mkoa (full walimu, majengo nk)...
2. Futa vyeo DC, Manaibu Waziri, Waziri (Katibu mkuu tu anatosha wizarani), wizara 11 zinazoongozwa na makatibu wakuu...pesa utazo kuwa ume-save hapo boresha mafao ya wafanyakazi watanzania hasa wa serikalini kuongeze morally kazini
3. Wizara ya Barabara ianzishwe ndani ya miaka ishirini nchi iwe na barabara zinazounganisha mikoa, wilaya, na kata zote kwa lami (kwa kutumia hela za ndani (TRA)
4. Hakuna uchaguzi wa Rais kwa miaka 20 isipokuwa uchaguzi wa serikali za mitaa basi ...anzisha kitengo cha monotoring (say PCCB) kuangalia pesa ziendazo mikoa, wilaya na kata zinawafikia walengwa ...My thought.
 
Namna kuisaidia Tanzania kikwelikweli!
1. Futa bunge kwa miaka ishirini...utakuwa ume-save pesa nyingi sana kama malipo ya wabunge, posho, uchaguzi hizo pesa zote ambazo zingetumika huko ...jenga vyuo vikuu kila mkoa (full walimu, majengo nk)...
2. Futa vyeo DC, Manaibu Waziri, Waziri (Katibu mkuu tu anatosha wizarani), wizara 11 zinazoongozwa na makatibu wakuu...pesa utazo kuwa ume-save hapo boresha mafao ya wafanyakazi watanzania hasa wa serikalini kuongeze morally kazini
3. Wizara ya Barabara ianzishwe ndani ya miaka ishirini nchi iwe na barabara zinazounganisha mikoa, wilaya, na kata zote kwa lami (kwa kutumia hela za ndani (TRA)
4. Hakuna uchaguzi wa Rais kwa miaka 20 isipokuwa uchaguzi wa serikali za mitaa basi ...anzisha kitengo cha monotoring (say PCCB) kuangalia pesa ziendazo mikoa, wilaya na kata zinawafikia walengwa ...My thought.

Utajibu vipi maswali ya wanademokrasia, kwa kuendesha nchi bila bunge kabisa na kwa kutokuwa na chaguzi?
 
Mliambiwa mfunge mikanda na hakuna siku mmeambiwa mfungue mikanda hiyo.mbona wengine wameshaifungua? Au walidhani nyerere alisahau kuwaambia wafungue?
 
Utajibu vipi maswali ya wanademokrasia, kwa kuendesha nchi bila bunge kabisa na kwa kutokuwa na chaguzi?
China hakuna chaguzi je hakuna demokrasia? hakuna maendeleo na maisha mazuri?Demokrasia ni dhana tu.Tumefaidika nini na demokrasia umaskini? Bila wabunge serikali haiwezi kufahamu wapi hakuna barabara, maji, umeme, hospital nk?. wabunge wanakula bure fedha za wananchi. Mimi hadi leo sijawahi kupata huduma za mbuge. Wenyeviti wa mitaa na vijiji tosha kabisa. Nakuunga mkono siasa ni kupoteza tu rasilimali ya nchi.
 
Utajibu vipi maswali ya wanademokrasia, kwa kuendesha nchi bila bunge kabisa na kwa kutokuwa na chaguzi?
Wanademokrasia watusubiri mpaka baada ya miaka 20, wakati kuna resources za kuwalipa na watu walioosoma ili wasiwadanganye...ntawaambia please wait I have a mission.
 
Wanademokrasia watusubiri mpaka baada ya miaka 20, wakati kuna resources za kuwalipa na watu walioosoma ili wasiwadanganye...ntawaambia please wait I have a mission.

wanaoitwa wadau wa maendeleo (nchi za nje, hususan mataifa tajiri) watakutangazia vikwazo vya kiuchumi kukushinikiza urejeshe demokrasia, hapo utafanyaje?
 
Namna kuisaidia Tanzania kikwelikweli!
1. Futa bunge kwa miaka ishirini...utakuwa ume-save pesa nyingi sana kama malipo ya wabunge, posho, uchaguzi hizo pesa zote ambazo zingetumika huko ...jenga vyuo vikuu kila mkoa (full walimu, majengo nk)...
2. Futa vyeo DC, Manaibu Waziri, Waziri (Katibu mkuu tu anatosha wizarani), wizara 11 zinazoongozwa na makatibu wakuu...pesa utazo kuwa ume-save hapo boresha mafao ya wafanyakazi watanzania hasa wa serikalini kuongeze morally kazini
3. Wizara ya Barabara ianzishwe ndani ya miaka ishirini nchi iwe na barabara zinazounganisha mikoa, wilaya, na kata zote kwa lami (kwa kutumia hela za ndani (TRA)
4. Hakuna uchaguzi wa Rais kwa miaka 20 isipokuwa uchaguzi wa serikali za mitaa basi ...anzisha kitengo cha monotoring (say PCCB) kuangalia pesa ziendazo mikoa, wilaya na kata zinawafikia walengwa ...My thought.
Mh kweli its your thoughts!
 
Mawazo yangu binafsi: kabla hatujaanza kuangalia wanao tutawala labda ni vyema tukaangalia sisi wenyewe tufanye nini.
1. Niwe mfuata sheria.
2. Lipa kodi ambazo ninatakiwa kulipa
3. Tuache tabia zakutafuta njia za mkato (k.m. vyeti feki, lesseni za biashara feki, ...)
4. Tuwe na fikra za uzalendo na sio by default kufikiria deals....
5. Tuwe na akili za kujituma na sio kalalamika juu ya matatizo
6. tuwe wachapa kazi

Hayo tuu yataweza leta mabadiliko tunayoyahitaji... then labda tunaweza hold viongozi wetu accountable...

Nawasilisha....
 
Mawazo yangu binafsi: kabla hatujaanza kuangalia wanao tutawala labda ni vyema tukaangalia sisi wenyewe tufanye nini.
1. Niwe mfuata sheria.
2. Lipa kodi ambazo ninatakiwa kulipa
3. Tuache tabia zakutafuta njia za mkato (k.m. vyeti feki, lesseni za biashara feki, ...)
4. Tuwe na fikra za uzalendo na sio by default kufikiria deals....
5. Tuwe na akili za kujituma na sio kalalamika juu ya matatizo
6. tuwe wachapa kazi

Hayo tuu yataweza leta mabadiliko tunayoyahitaji... then labda tunaweza hold viongozi wetu accountable...

Nawasilisha....

Mkuu Skasuku,
Kama ningeambiwa niipe hoja yako heading, ningesema UADILIFU. Basi kumbe namna nyingine ya kuisaidia Tanzania ni kujenga uadilifu miongoni mwa raia, raia wapi lakini.. hiki kizazi kilichokwisha kubuhu katika kutenda kinyume na uliyoyataja, au tuelekeze ukunjaji katika samaki wabichi (mashuleni)?
 
Mkuu Skasuku,
Kama ningeambiwa niipe hoja yako heading, ningesema UADILIFU. Basi kumbe namna nyingine ya kuisaidia Tanzania ni kujenga uadilifu miongoni mwa raia, raia wapi lakini.. hiki kizazi kilichokwisha kubuhu katika kutenda kinyume na uliyoyataja, au tuelekeze ukunjaji katika samaki wabichi (mashuleni)?

Naam! Mashuleni, misikitini, makanisani, katika jamii... Ukiangalia Tanzania ya sasa kweli kuna mambo mengi sana yakuweka sawa. Huu ni mtihani mkubwa... na hauna feki.. sijui tutalitatua vipi...
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom