Namna Mkoa wa Kilimanjaro unavyokua kwa kasi

NEW NOEL

JF-Expert Member
May 21, 2011
863
407
Picha hizi ni maeneo ya Machame katika wilaya ya Hai ambayo mbunge wake ni Freeman Mbowe.

Kwa kweli inatia moyo kuona namna watu wa mkoa huu hususani wachagga wanapofanya uwekezaji katika maeneo yao. Na wanafuata ila falsafa inayosema 'Charity begins at Home'.

Na kwa sasa badala ya kujenga tu nyumba za kuishi,utaweza kuona namna hata Hotel na Lodge za kisasa zikijengwa.

Nafikiri ni wakati sasa na watu wa maeneo mengine nao wakafanya uwekezaji.

Kwani sio tu watachangia pato la taifa bali watatoa na ajira kwa watu wa maeneo hayo.
 

Attachments

  • 1456919998753.jpg
    1456919998753.jpg
    55.8 KB · Views: 187
  • 1456920046140.jpg
    1456920046140.jpg
    45.6 KB · Views: 188
  • 1456920069131.jpg
    1456920069131.jpg
    47.8 KB · Views: 207
  • 1456920088011.jpg
    1456920088011.jpg
    50.6 KB · Views: 150
Aisse kuna watu mawe kweli.

Uwekezajiwa Lodges na Hotels kwa Moshi ni wa muda mrefu saaana tena wazawa kibao wamewekeza.Eti wewe ndio unaona leo.Sie tuliopo kwenye Utalii tunalijua hilo

Halafu nani kakuambia kwamba Kilimanjaro ni Wachaga tuu ndio wamewekeza.Au Kabla ni moja tu

Kama kuna chama kina mwanachama kama wewe,basi kinahasara kweli,maana uelewa wako negative zero
 
Wabunge na madiwani wa Dodoma, Singida,Katavi Nk wangekuwa na utaratibu wa kutembelea Kilimanjaro na kufanya study tour kujua wanafanyaje ili kupata maendeleo pamoja na uhaba mku wa wa ardhi walionao? Nini mwelekeo wao wa kisiasa ili ujuzi watakaopata waupeleke kwao.
Sio jambo zuri nchi moja wengine wanaishi vizuri na wengine wanaoonea viwavi na kula magunzi ya mahindi
 
Ndio sababu Chadema hawaitishi Maandamano huko ili Mazingira ya kwao yasiharibike! lissu ajifunze maana yeye huwazuia wananchi wake wasichangie maendeleo wakati wenzie wanachanja mbuga na wote ni Chadema
 
Aisse kuna watu mawe kweli.

Uwekezajiwa Lodges na Hotels kwa Moshi ni wa muda mrefu saaana tena wazawa kibao wamewekeza.Eti wewe ndio unaona leo.Sie tuliopo kwenye Utalii tunalijua hilo

Halafu nani kakuambia kwamba Kilimanjaro ni Wachaga tuu ndio wamewekeza.Au Kabla ni moja tu

Kama kuna chama kina mwanachama kama wewe,basi kinahasara kweli,maana uelewa wako negative zero
Waache walie lie tu wenzao ma porter wanapanda mlima,ma guide wanapandisha na kupata kipato,watoto wanasoma na kupata ajira nzuri huku wengine wakijamba jamba tu
 
Picha hizi ni maeneo ya Machame katika wilaya ya Hai ambayo mbunge wake ni Freeman Mbowe.
Kwa kweli inatia moyo kuona namna watu wa mkoa huu hususani wachagga wanapofanya uwekezaji katika maeneo yao. Na wanafuata ila falsafa inayosema 'Charity begins at Home'. Na kwa sasa badala ya kujenga tu nyumba za kuishi,utaweza kuona namna hata Hotel na Lodge za kisasa zikijengwa.
Nafikiri ni wakati sasa na watu wa maeneo mengine nao wakafanya uwekezaji.
Kwani sio tu watachangia pato la taifa bali watatoa na ajira kwa watu wa maeneo hayo.


Wewe kweli akili zako zinakutosha wewe mwenyewe! Nilifikiri unaleta Viwanda amabvyo vimezalisha ajira na Miundombinu mipya na bora kumbe unaleta mavila ya akina Mengi na wafanyakzi wa UN waliojenga kwao!

Sasa wewe Mavila ya mtu binafsi yanakusaidia nini? Siajabu akikuona hapo jirani na geti lake atakuitia askari wewe unajivunia!
 
Sawa, Mi nina wivu wa kike!.Wazee wa sifa!. Kamkoa kadogooo sawa na wilaya ya Gairo , Mnakasifu kwa maendeleo!, Poleni, maendeleo sio Nyumba, bali ni uchumi jumuishi, ingekua Kilimanjaro ina Maendeleo vijana wote wasio na kazi wangekimbilia Kilimanjaro, Si mnaona Uingereza?(British isle) kadogooo lakin watu kila siku wanataka kwenda.Hakuna mkoa ulioendelea Tanzania, Mikoa yote ni 'hari mbaya' na Mingine ni 'Mahututi'.
 
Sawa, Mi nina wivu wa kike!.Wazee wa sifa!. Kamkoa kadogooo sawa na wilaya ya Gairo , Mnakasifu kwa maendeleo!, Poleni, maendeleo sio Nyumba, bali ni uchumi jumuishi, ingekua Kilimanjaro ina Maendeleo vijana wote wasio na kazi wangekimbilia Kilimanjaro, Si mnaona Uingereza?(British isle) kadogooo lakin watu kila siku wanataka kwenda.Hakuna mkoa ulioendelea Tanzania, Mikoa yote ni 'hari mbaya' na Mingine ni 'Mahututi'.
Kadogo na reachable every corner.
Of course kumiliki nyumba bora ni maendeleo, siyo sawa na kumiliki nyumba ya tembe/nyasi. Hotel hutoa ajira halafu hapo ni kijijini.
 
Wewe kweli akili zako zinakutosha wewe mwenyewe! Nilifikiri unaleta Viwanda amabvyo vimezalisha ajira na Miundombinu mipya na bora kumbe unaleta mavila ya akina Mengi na wafanyakzi wa UN waliojenga kwao!

Sasa wewe Mavila ya mtu binafsi yanakusaidia nini? Siajabu akikuona hapo jirani na geti lake atakuitia askari wewe unajivunia!
Sasa mimi nazungumzia uwekezaji wa hotel na lodge wewe unazungumzia nyumba za watu. Usikurupuke,soma na fikiri kabla haujaja na hoja.
 
Aisse kuna watu mawe kweli.

Uwekezajiwa Lodges na Hotels kwa Moshi ni wa muda mrefu saaana tena wazawa kibao wamewekeza.Eti wewe ndio unaona leo.Sie tuliopo kwenye Utalii tunalijua hilo

Halafu nani kakuambia kwamba Kilimanjaro ni Wachaga tuu ndio wamewekeza.Au Kabla ni moja tu

Kama kuna chama kina mwanachama kama wewe,basi kinahasara kweli,maana uelewa wako negative zero
Unaposema uwekezaji wa lodge na hotel ni wa muda mrefu unapaswa kuwa na data kamili. Usikurupuke,wala kusukumwa kujibu hoja kwa wivu usio wa kimaendeleo. Palipo na stahiki ya kupewa sifa ni vyema ukatoa sifa. Nimezungumzia Machame ambapo ni maeneo ya vijijini na watu wengi wanaendelea kuwekeza na wengi wao ni wachaga. Hivyo ni vyema na wakazi wa maeneo mengine tukaiga mazuri na kuyapeleka kwetu.
 
mahali pakiongozwa na mpinzani.....
tegemeeni uongoz bora+maendfeleo2 yakutosha.....
upinzani ndo nguzo na chachu ya maendelea TZ....CCM yamewashinda tangu tupate uhuru
ni maajabu2 yanendeleaga
 
Mkoa wa Kilimanjaro hauna uwekezaji wowote.Hata hiyo picha haipo Machame.Kilimanjaro ni mkoa masikini sana kimapato.ndio sababu tumesambaa kila kona ya nchi kujitafutia riziki..hakuna ardhi ya kulima,Zao la kahawa limekufa siku nyingi.Utawekeza nini?Biashara ya hapa ni kwenda Taveta ulete bidhaa na ukwepe kodi. Mji wa Moshi umechakaa mno.Wenyeji wataendelea kukimbia huku kwani kiuchumi ni mbaya sana.
 
Back
Top Bottom