naninibaraka
JF-Expert Member
- Oct 13, 2011
- 910
- 669
Zikiwa zimebaki siku chache kabla ya watanzania hawajapiga kura. Dalili zote zinaonyesha anguko kubwa la CCM iliyodumu madarakani kwa zaidi ya nusu karne. Tofauti na chaguzi zingine zilizopita, CCM hawana uhakika wa kushinda, hakuna mkoa wanaoweza kujihakikishia ushindi kama ilivyokua awali.
Swala la kukimbiwa na makada wake maarufu mfano Kingunge na wengine limezidi kuiweka CCM kwenye wakati mgumu. Kauli za baadhi ya makada ndani ya CCM mfano mzee Mkapa, Bulembo, Nape na wengine kimezidi kuleta mgawanyo ndani ya hiki chama kikongwe.
Ugumu mwingine na swala la mgombea John Pombe kutosikiliza mawazo ya team ya kampeni ambapo baadhi ya vyombo vya habari vimekua vikiriport kuwa ni mtu asjiyeshaurika. Kauli ya mgombea Magufuli kuwa kuna watu mchana wapo na yeye na usiku wako UKAWA siyo ya kubezwa, kuna uwezekano mkubwa kuwa CCM haijui ukubwa wa tatizo hili, mfano kila wanapokuja na mikakati taarifa zinavuja mapema hata kabla ya utekelezaji ukweli ni kuwa kuna watu ndani ya CCM wameamua kubaki kama strategy ya kukiua chama,.
Information is power, ndio mana kwa strategies hizi UKAWA imeendelea kuimarika licha ya changamoto mbalimbali. CCM kwa sasa wanafanya damage control, team ya zaidi ya watu 30 iliyoundwa kumsaidia Magufuli haijaweza kumnadi Magufuli kama ilivyotegemewa.
Swala la CCM kumtukana Lowassa ilihali kabaki kimya na kuendelea na kunadi sera kwa wananchi nalo ni pigo kwa CCM. Katika maisha ya kawaida kabisa unamtukana matusi mtu asiyekutukana, nani anaonekana mwendawazimu mbele ya wapiga kura? S
Siasa za CCM zisizoendana na mahitaji ya sasa ndizo zilizomfanya Lowassa kuendelea kukubalika kila anakokwenda, dalili au ishara za CCM kuanguka ni kubwa kuliko chaguzi zilizopita!
Mabadiliko yanakuja, siamini hata kidogo kama CCM kwa sasa wanategemea bao la mkono kama kete yao ya mwisho ya ushindi!
Tafakari na chukua hatua..
Swala la kukimbiwa na makada wake maarufu mfano Kingunge na wengine limezidi kuiweka CCM kwenye wakati mgumu. Kauli za baadhi ya makada ndani ya CCM mfano mzee Mkapa, Bulembo, Nape na wengine kimezidi kuleta mgawanyo ndani ya hiki chama kikongwe.
Ugumu mwingine na swala la mgombea John Pombe kutosikiliza mawazo ya team ya kampeni ambapo baadhi ya vyombo vya habari vimekua vikiriport kuwa ni mtu asjiyeshaurika. Kauli ya mgombea Magufuli kuwa kuna watu mchana wapo na yeye na usiku wako UKAWA siyo ya kubezwa, kuna uwezekano mkubwa kuwa CCM haijui ukubwa wa tatizo hili, mfano kila wanapokuja na mikakati taarifa zinavuja mapema hata kabla ya utekelezaji ukweli ni kuwa kuna watu ndani ya CCM wameamua kubaki kama strategy ya kukiua chama,.
Information is power, ndio mana kwa strategies hizi UKAWA imeendelea kuimarika licha ya changamoto mbalimbali. CCM kwa sasa wanafanya damage control, team ya zaidi ya watu 30 iliyoundwa kumsaidia Magufuli haijaweza kumnadi Magufuli kama ilivyotegemewa.
Swala la CCM kumtukana Lowassa ilihali kabaki kimya na kuendelea na kunadi sera kwa wananchi nalo ni pigo kwa CCM. Katika maisha ya kawaida kabisa unamtukana matusi mtu asiyekutukana, nani anaonekana mwendawazimu mbele ya wapiga kura? S
Siasa za CCM zisizoendana na mahitaji ya sasa ndizo zilizomfanya Lowassa kuendelea kukubalika kila anakokwenda, dalili au ishara za CCM kuanguka ni kubwa kuliko chaguzi zilizopita!
Mabadiliko yanakuja, siamini hata kidogo kama CCM kwa sasa wanategemea bao la mkono kama kete yao ya mwisho ya ushindi!
Tafakari na chukua hatua..