Nakutibia wewe na mume wako msigombane tena

Nakutibia wewe na mume wako msigombane tena

mgt software

JF-Expert Member
Joined
Nov 1, 2010
Posts
13,793
Reaction score
7,165
Wana JF wasalaam,

Kama kawaida leo nimeona niwaletee tiba mbadala kwa wale waliodhurika na magonjwa mbali mbali ambayo mme mke hayapendi kuyaona. Leo katika safu ya tiba, kuna tiba tatu ambazo kwa ushirikiano kama mtazizingatia zinaweza kuleta mwamko wa mapenzi yaliyofifia.

1. Kwa wale wenye kinywa kinachotoa harufu kali: zuia hii harufu nyote kwa pamoja, kama wewe unahisi una meno yametoboka toboka, jua kwamba kuna mabaki ya chakula ambayo mswaki hauwezi kufika, basi nenda hospitali wakayazibe au uyang'oe, pia ujaribu kusugua sana ulimi hadi uwe na rangi nyekundu.

2. Dawa ya wanayonukisha soksi mke ndio unapewa jukumu la kumkumbusha baba kuwa na pea kumi za soksi, hakikisha soksi zote ni kotoni na ni nyeupe, hakikisha mume ana pea angalau mbili za ngozi, akivua chukua manukato kidogo tia ndani.

3. Mtonyo mzima ni kwa wale wanaosumbuliwa na fangasi za ukeni na mababa wanausumbuliwa za katikati ya mapaja, chukua dawa inayitwa kibiriti kutoka kiwanda cha dawa kilichopo mwenge, gramm tatu hivi, changanya mafuta ya Baby care ya gramm 100, tafuta pafyumu uipendayo, pulizia nyingi ili kuondoa harufu ya mafuta ya baby care na kibiriti muwasho.

Kisha nyoa nywele zote zinazozunguka mwili wako na kubadilisha majina tofauti tofauti, paka mwili mzima kwa wiki hivi, kwa akina mama, kabla ya kufanya tendo kama una fangas, mwambie mwenzio apake sehemu ya nyeti full ndio muanze mchezo , itakusaidia kupekecha sehemu usizoweza kufika kwa kidole na dawa itaingia sawa sawa fanya hivyo siku tatu.

Baada ya hapo nunua dazen ya vyupi vya kotoni, wewe na mumeo acheni ubahili nunueni vyupi vya kotoni sio mpira, nawe mama unayependelea kuvaa skin taiti za mchina achana nazo sio urembo piga kavukavu ya kotoni kama yakiumeni au nunua boxer ya kiume hakuna neno siku hizi tunavaliana, kama mzigo haunei kwenye vyupi usiwe na aibu kwenda kwa fundi hakushonee vyupi vya kotoni.

Hii ndio tiba dhabiti ambayo inanusuru ndoa kwa kutuhumiana kureta magonjwa ya fangasi kumbe mnatembea na mitambo ya kutengenezea.
 
Apo kwenye acheni ubahili ndo nimechoka kabisa.....
Ila ni mawazo mazuri
 
Mmmmh mara ya mwisho fangasi nilipata mwaka gani vilee.... hata sikumbuki ila hizo cotton hata ubadlisha x3 kama huko kunako unakuosha na sabuni sijui kuingiza kidole kuchokono, umchafuu ukishaduu unajifuta tuu unaendelea na safari,chupi unaanika kwenye tendegu la kitanda,dirishani nk na sio nje ipigwe na jua na kukauka vzr, unnatumia vyoo vya kila pahali wee popote pale unaingia, kujitawaza kwa maji na makopo usiyoyajua,kujiacha mbichimbichi humoo nk wee u.t.i na fangasi hazkuachi ng'ooo utaugua kuutwaaa!
 
Back
Top Bottom