Nakufa naombeni msaada

Nakufa naombeni msaada

sassy girl

Senior Member
Joined
Sep 19, 2020
Posts
112
Reaction score
174
Habari wanajukwaa hili la JF,

Mimi ni mjamzito na ni ujauzito wangu wa kwanza, wakati ipo changa nilikua nasumbuliwa sana na morning stickiness hata maji nilikua sinywi, natema mate tu na kutapika harufu mbaya mbaya yani nilikonda sana kiasi nilikua naumwa Hadi mwanaume wangu akawa anaogopa akawa ananiambia kama haitaweza kuhandle situation tuitoe hakusema Kwa nia mbaya kwakua wote tulimuomba na kumdhamiria hichi kiumbe nafikiri ni kwakua umri wetu na wote hatujawahi kuwa na mtoto, mtoto wetu wa kwanza kwetu sote.

Nisiwachoshe kilichonifanya niandike ni hiki 2nd semester nikawa na ahueni angalau nakula matunda na chakula kiasi nadokoa dokoa hv hv Ila mate yalikua bado nilikua na kopo kabisa special ghafla nikaanza kupata hamu ya Udongo nikamwambia mwenzangu akaenda nitafutia (sipo nyumbani Tanzania ilibidi nigoogle akautafute masokoni lol) akaupata Ila mweupe na nikaridhika nao.

Tatizo likaanza nikishakula chakula udongo ndy kama tunda langu naushushia yani hata dk 5aimalizi toka nile nataka udongo na nnaula hasa hadi najihirumia nikawa Hadi nauficha na kujaribu kujiwekea limit lakin nafail nakumbuka Kuna siku uliisha nikasema nitajikaza na sitakula tena chakula Hadi kesho mana nikila lazima nile udongo else najitskia hovyo hamuwezi amin nilipata shida nilizunguka nyumba mzima usiku wa manane Hadi nilipopiga jicho jikoni kulikua na viazi vitamu vibichi yale maganda yake yanaudongo nikawa nabandua udongo nakula.

Mwezi ujao M/Mungu akijaalia ntajifungua InshaAllah Ila tangu juzi kiukweli najskia hovyo na nahisi kabisa na akili yangu inaniambia ni udongo nikila au nisipokula hali Sawa Ila nashindwa kuacha mwili unakosa nguvu na najua fika nimeula mwingi sana naombeni kujua kama ndy sababu ya kuhisi hovyo na je madhara ya Udongo ingawaje kesho InshaAllah nimepanga kama hali itakua hii niende hospital.

Asante I naombeni kujua madoctor

Sent from my Nokia 7.2 using JamiiForums mobile app
 
Unaupungufu wa vitamin fulani ngoja waje madaktari watakueleza..
 
Pole Sana Dada! Mwenyezi akujaalie ujifungue salama.

Kila mimba ina changamoto zake na wewe una changamoto hizo katika mimba hiyo.

Ulaji wa udongo kwa mjamzito mara nyingi huchangiwa na upungufu wa baadhi ya Madini muhimu mwilini.

Unahitaji doctor kutoka wapi...
Tanzania, huko ughaibuni ulipo, au hapa Jf!
 
Hongera kwa ujauzito...

Pia pole kwa mateso unayopitia

Sio mtaalamu ila watakuja wataalamu ninachojua mimi mateso ni kawaida kwa mama mjamzito kikubwa ni uvumilivu tu uzuri umebakiza mda mdogo uendele kuvumilia.. tuliambiwa mwanamke atabeba mimba na kujifungua kwa mateso na uchungu ndio mateso yenyewe hayo jikaze

Swala udongo sioni kama linamadhara tena kuna wanawake wanakula udongo all of their life... Nimewaona tunaishi nao nawanadunda tu mjini.

Pole sana.. Mungu aendelee kukupa nguvu na uvumilifu zaidi.
 
Kula ule udongo unaouzwa sokoni ni sahihi kabisa na unatakiwa kula mwingi kadri unavyojisikia.Kwa sasa hivi kiasi cha madini unachohitaji ni kikubwa sana kwa kuwa mpo wawili,yaani wewe pamoja na mtoto wako.

Ule udongo ni madini ya calcium,iron,e.t.c wala siyo udongo kama unavyoita wewe.Kula udongo kwa wingi kadri unavyojisikia ila hakikisha kuwa unakula ule unaouzwa masokoni.Usile udongo ila mradi udongo kwa kuwa utaishia kupata magonjwa mengine.
 
Clinic huend nin.....kwan sikuna vidonge vya iron mnapewaga...inamana huvitumii kabisa ama...mwil wa binadam ni machine...uhitaj wako wa udongo kias hko inamana huna madin chuma...na kama hupat supliments za hayo madini kuna uwezekano ikaja mwathiri mtoto..akizaliwa ana tatzo ndio utaelewa....kama unahudhuria clinic wenzio huwa wanaelezwa hayo mambo
 
kula udongo wakat wa ujauzito mana yake ni kua unakosa madini ya chuma, mamii utapungukiwa damu jikaze kula sana mboga za majani dagaa samaki samaki udongo sio mzuri
 
hio inaitwa craving...ni disorder ya mjamzito kutamani vitu visivyo vyakula....fuatilia zaidi kuhusu minor disorders za pregnancy utaikuta hii na zingine nyingi
 
Kwa ninavyofahamu kula udongo utaishia kupata minyoo ambayo itakuathiri wewe na mwanao,

Suluhisho hapo ni wewe kutumia vidonge vya FeFo ili kuongeza madini chuma, pia kula sana mboga za majani, dagaa, samaki, nyama na matunda,

Kuhusu udongo sio mzuri utakuletea shida itakayokutesa na kumtesa mwanao pia, ukisoma athari za minyoo wakati wa ujauzito utaelewa vizuri

Na hakuna udongo mzuri, whether unauzwa sokoni ama unauandaa mwenyewe
 
Pole sana, jitahidi uwe unakula walau punje 5 za tende au zaidi kwa siku. Tende itakusaidia kuongeza uzito,zina baadhi ya madini kukupa nguvu na tende humsaidia mama mjamzito kutotoka damu nyingi wakati wa kujifungua.

Ukiwa na muda pitia hii kitu mtandaoni "Eating dates during pregnancy" au link hiyo hapo chini usiogope tende haina madhara yoyote kwa mjamzito.
Eating Dates During Pregnancy - Safe or Unsafe ?

"Seafarers and children are friends like fish and water".
 
Wala usijali. Fanya mwili wako unavyotaka usijinyime.

Mke wangu ujauzito wa kwanza alipata shida sana mpaka nikajuta kwa nini nilipiga bao ndani si ningemwaga nje. Alikondaaaaa. By nature yeye mwemba. Halafu kakonda sasa. Kama skeleton. Nimeogopa sana. Semister ya tatu mambo ndio yakawa afadhali.
So usijali kabsa.
 
Pole sana dada hongera kwa kuwa mama kijacho

Ngoja nieleze kidogo kuhusu hali yako,mwanamke anapopata ujauzito kuna mabadiliko ambayo yanatokea ndani ya mwili wake wanaita 'physiological changes' kwa sababu ya pregnancy hormones effect.

Hiyo hali ya kula udongo kitaalamu inaitwa 'pica' means desire to eat non nutritious substance hiyo ni dalili ya upungufu wa iron,Tumia hemovit syrup huo ni upungufu wa damu.

Kuhusu kuwa na mate mdomoni nafikiri ni kwa sababu ya reflux ya acid inasababisha hypersalivation mdomoni tumia Omeprazole

Ni hayo tyu mama kijacho,kila la kheri
 
Kama ni mimba yak0 ya kwanza inawezekan ni Hali ya kawaida si0 wew uhisi unatatzo kubwa kumbe ni kwakuw huna uzoefu

Pengine zaidi nenda Hospital kwakuw hata sisi ujatupa indication ambazo tunawez tambua its normal situation or bady condition

NB:-kitanzania sijackia mama mjamzto amezurka kwa kula udongo ila kula udongo ni ukosefu wa madn fulan na HAKUNA MADHARA DHAHIRI NILIYOWAH SIKIA.
 
Asanteni Kwa ushauri ,sijambo na Mimi na mtoto pia tunaendelea vizur nilienda hospital nimepewa hyo hemovica na vidonge Mungu awabariki nyote
 
Wewe una kichaa sio bure.

Unatuandikiaje uzi kwamba unakufa? Au ndo attention seeker

Tunakuja kusoma kumbe ni ishu ya kupenda kula udongo

Ushanikwaza [emoji35][emoji35][emoji35][emoji35][emoji35][emoji35]
Asante kama ukihitaji ushaur wa haraka na wewe tafuta attention kama mie ili watu waukimbilie Uzi wako[emoji3]bila kichwa cha habari usingesoma ,hongera Kwa kukwazika panapo makaaliwa nikishusha mzigo ntakuPM utume permpers
 
Back
Top Bottom