mdukuzi
JF-Expert Member
- Jan 4, 2014
- 16,039
- 35,922
Ndivyo navyoweza kusema, nilioa miaka mitano iliyopita ila huyu mwanamke ni kiboko niliwahi kutupiwa begi la nguo nje kama Dk Slaa kisa nimerudi saa nne usiku nilichelewa baada ya kutoka kwenye kiako cha harusi ya mshkaji, nami kwa hasira nikaenda kulala kwa wazazi wangu.
Visa vilizidi ikabidi nichukue hamsini zangu,nikiwa na upweke ndio nikakutana na mdada mwenye sifa zote za mke, mrembo sana, msomi, ana adabu na kila sifa nzuri ya mwanamke ikabidi nimfiche kuhusu ndoa yangu, japo nilimwambia kuwa nina mtoto alikuwa tayari.
Ila wiki iliyopita ikabidi nimwambie ukweli kuwa nina ndoa, japo kila mtu anaishi kivyake, dada wa watu kanuna, hataki hata kuniongelesha, najuta kuwahi kuoa huyu ndio alikuwa mke wangu, kwani tulipendana sana na tulimatch vitu vingi sana.
Natamani Yesu arudi afanyie mabadiliko sheria ya ndoa kwa sisi wakristo ili niuoe huyu dada
Visa vilizidi ikabidi nichukue hamsini zangu,nikiwa na upweke ndio nikakutana na mdada mwenye sifa zote za mke, mrembo sana, msomi, ana adabu na kila sifa nzuri ya mwanamke ikabidi nimfiche kuhusu ndoa yangu, japo nilimwambia kuwa nina mtoto alikuwa tayari.
Ila wiki iliyopita ikabidi nimwambie ukweli kuwa nina ndoa, japo kila mtu anaishi kivyake, dada wa watu kanuna, hataki hata kuniongelesha, najuta kuwahi kuoa huyu ndio alikuwa mke wangu, kwani tulipendana sana na tulimatch vitu vingi sana.
Natamani Yesu arudi afanyie mabadiliko sheria ya ndoa kwa sisi wakristo ili niuoe huyu dada