Najali Afya Nutrition Clinic

Najali Afya Nutrition Clinic

Kwedinguzu

Member
Joined
May 16, 2020
Posts
40
Reaction score
26
Habari Wakuu? Bila shaka ni wazima Afya, poleni sana na changamoto za kutafuta ugali.

Mwaka 2023 ndo huo unaisha, Wasaka ajira wenzangu, huu mwaka umeishaje? Unajionaje kwenye harakati za kusaka ajira, mwaka 2024 tutatoboa? Tuzidi sana kumuomba Mungu, naamini ipo siku tutafika nchi ya ahadi.

Niende kwenye mada mojamoja, Mimi kitaaluma ni Afisa lishe, mwaka 2024 ninao mpango wa kufungua Nutrition clinic, naamini umefika wakati sasa wa kila mtu awe na mtaalamu wa Lishe ambae atafuatilia hali ya Lishe ya mtu husika na ku kumshauri nini chakufanya ili aweze kua na hali ya lishe iliyo bora.

Watu walio wengi wanao madaktari wao binafsi wa kuwatibia wanapo kua na mtatizo, lakini tukumbuke ya kua matatizo yaliyo mengi tunaweza kuyazuia kwa kiwango kikubwa kupitia Lishe (Chakula) Kwahiyo kwanini usiwe na mtaalamu wa lishe mwenye kufuatilia chakula unachokula na vinywaji unavyo kunywa kabla ya kua na daktari wa kukutibia?

Clinic ninayofikilia kuianzisha itahusika na makundi yote ya watu

• Watoto umri wa miaka 0-5
• Vijana lika balehe
• Wajawazito na Wanao nyonyesha
• Watu wote ambao sikuwataja kwenye makundi hapo juu (me&ke)

Kwa wazoefu wa masuala ya Clinic, naomba mnifahaimishe, taratibu za kufanya ili niweze kuanzisha hiki kituo.

Asanteni sana.
 
Fika ofisi ya idara ya afya mahali ulipo utapewe muongozo,kila jema.
 
Back
Top Bottom