Naiona Simba ikishuka daraja

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
47,034
144,387
Kipigo cha bao 5 kutoka kwa Yanga, kina dalili zote za kuivuruga Simba kuanzia kwenye uongizi mpaka kwa wachezaji na bench zima la ufundi.

Hivyo; busara ikikosekana, kuna hatari ya hii club kusambaratika na kufanya vibaya katika ligi na wasipokuwa makini, club itashika nafasi za chini kwenye ligi na hata kushuka daraja wasipojiangalia labda wabebwe.

Simba wanapaswa kukubali matokeo kwani udhaifu wa timu yao lilikuwa ni jambo la wazi na limekuwa likisemwa ila walikuwa wanashinda kibahati.

Nawashauri Simba wajitoe kwenye ligi ya mabingwa, vinginevyo watavuna aibu kuliko ile walioipata kutoka kwa Yanga.
 
Yanga juzi haikuwa kwenye muunganiko mzuri. Timu ilicheza mchezo wa hovyo usiovutia. Nadhani kwenye mzunguko wa pili timu ya Wananchi itakuwa imeshapata muunganiko mzuri kitimu na kutoa adhabu kali zaidi kwa hawa vijana wa Msimbazi. Mwakani Simba watakula 8 sifuri.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom