Nailaani serikali inayoongozwa na CCM

Nailaani serikali inayoongozwa na CCM

IKWETE

JF-Expert Member
Joined
Dec 26, 2012
Posts
4,057
Reaction score
696
Baba yangu mzazi baada ya kufika hospitali ya Mhimbili yapata miezi mitatu iliyopita aliambiwa kupata huduma aliyoihitaji alipaswa kutoa kiasi cha shilingi laki tisa na ishirini na saba elf(927,000/-. Wahudumu na manesi wakamtoa wodini na kutuamuru tuondoke turudi baada ya kulipa hicho kiwango. Wakati huo hakuwa na fahamu.

Tukachangishana ikafika laki 6, wakakataa hadi tulipe yote. Baada ya siku mbili pesa ilitimia. Ndipo alipopokelewa na kuanza kupata huduma.

Upuuzi huu umekuwa ukishamirishwa na serikali ya CCM. Watanzania wamekuwa watumwa ndani ya nchi yao wenyewe. Wafanyakazi wamekuwa viburi na hawana wasiwasi kwakuwa mfumo uliopo chini ya CCM unawabeba.

CCM imetufikisha mahali kuwaona wagonjwa masikini wasio,na pesa hawana maana.

Kwa CCM ukiwa mteule na unanufaika na mfumio, huduma za hata kutibiWa mafua utazipata india au marekani
 
Makabwela tuna kazi kweli mkuu,viongozi wote wa nchi hii hufia nje ya nchi,sisi hufia kwenye vizahanati mitaani.
 
...ruzuku ya kugharamia matibabu yetu imepelekwa kwenye kampeni. Mbaya zaidi vitengo vya muhimbili vikikarabatiwa na bei ya matibabu inakarabatiwa utafikiri sio kodi no,hela zetu ndo zimetumika kukarabati....
 
Ndio katiba mpya hiyo inayowajali wananchi wake kwa hali na mali! Wananchi amkeni!
 
Wamekarabati MOCHOARI kwa sababu inapokea wote bila kujali itikadi ya chama
 
Back
Top Bottom