Chadema hakika sikipendi kutokana na
1. Kuweka mbele maslahi ya chama kuliko UTAIFA
2. Kupinga umoja wa vyama vya kisiasa kupitia TCD
3. Wabunge wake kutowawakilisha wananchi ipasavyo wawapo bungeni
4. Madiwani wake kutohamasisha wananchi kufanya shughuli za maendeleo
5. Kuratibu maandamano yanayohatarisha amani nchini
HIVI MASLAHI ya Taifa ni yepi? Maana hili ni suala pana lenye tafsiri nyingi na tata. Kila chama kinachoanzishwa huwa na DIRA na MALENGO yake, suala la kuuangana vyama si baya lakini si lazima.CUF wakiungana na TLP suala la kujiuliza ni je, wanaungana ili iweje? Katika muungano huu ni kipi kitaenda kutekelezwa maana hivi ni vyama vyenye itikadi tofauti.
Ni vyema kujiuliza AMANI ya nchi maana yake ni nini?
Je, shughuli za maendeleo ni zipi? Wananchi wanaolipa kodi(direct or indirect) kwa kulipa kwao kodi wanakuwa bado hawajashiriki shughuli za maendeleo?