Nahitaji ushauri katika kuibadili hii tabia

Nahitaji ushauri katika kuibadili hii tabia

Pendelea kufanya ibada, mshirikishe Mungu akusaidie kukurekebisha.
Pia andika ukutani kwako kijikaratasi cha kuikataa hiyo tabia na kila mara sema nafsini mwako, Mimi Ni mtu mpya
Asante nitaanza kufanyia kazi ushauri wako
 
Jiunge kwenye Network marketing company yoyote ,fanya kwa mwaka mmoja. Aisee hutojuta for the rest of your life.
Ni moja kati ya vitu ninavyochukia kufanya
 
Kuna baadhi ya tabia hapo ambazo nilikuwa nazo kama wewe ila ukifikia umri fulani haihitaji ushauriwe ni namna tu ya kujiongoza mwenyewe


Mimi ni miongoni mwa watu waliokuwa hawaongei maneno ma3 kwa mtu yeyote hata mzazi nikikutana naye ni salamu na ishu nyingine basi, wakija wageni nasalimiana nao nikimaliza naondoka nakaa mwenyewe

Kilichonibadili ni chuo baada ya kupewa assignment ya kundi, nakumbuka nilikuwa mwenyekiti kundini, tukapanga muda wa kukutana kama saa kumi na mbili jioni, hakuna aliyetokea nikaondoka.... Imefika saa Tatu usiku wadau ndio wanakuja tukafanye kazi nikanyamaza kama kawaida yangu ila walipozidi kuzungumza nikawa mkali kwa kuwaropokea kuwa hawajali muda......

Asante Dr. Joseph popote ulipo, kuanzia hapo akawa ni mtu ambaye anakuja kunipigisha stori ili apotezee tukio lilotokea lakini nilipata matokeo chanya, yakuanza kujichanganya, stori za JF nazipeleka za uongo na ukweli ili mradi wa furahi nikajikuta napata chain ya marafiki ndugu na watu wengi kunikubali........

Kuna msemo amewahi kuniambia moja ya mashangazi zangu; MAISHA NI KUPANGA NA KUCHAGUA, HUKU WEWE UKIWA MPANGAJI AU MPANGUAJI YOTE UTAKAVYOONA WEWE

Katika hayo yote na umri ulio nao ilikubidi uanze kujiongeza kwa kubadilika mwenyewe, lakini ukiendelea kushupaza shingo, unaweza kukuta hata msiba umetokea au tatizo fulani au sherehe au kazi au chochote kile wataacha kukwambia kwasababu ya jeuri uliyo nayo



Yangu ni hayo kwa leo

Mr. Ben
 
Aisee mimi hi tabia naipenda sana hata...kwenye simu...nina namba za watu muhimu tu pamoja na marafiki wachache sana....Lakini mimi kuna kitu kilisababisha hadi niwe kwenye tabia kama hiyo..
 
Dah.....rahisi sana....chukua karatasi na kalamu.....
Andika listi ya watu 15 waliofanikiwa kifedha katika mji uliopo.....
Andika listi ya watu 10 wenye pisi kali katika mji huohuo uliopo....
Andika listi ya watu 5 wenye mamlaka hapo mjini kwako....
Kama haumo hata kwenye list moja wapo... my friend basi wewe ni mtu wa kawaida kabisa....achana na hayo mawazo mabovu
 
Mtoto anapozaliwa hua na id, ego na super ego.

Id inadeal sexual drives na aggressiveness, super ego inadeal na moral conscience na ego ina kazi ya kucheki reality kati ya id na super ego.

Yaani id inakuambia unachohitaji, ego inakuonyesha reality ya unachohitaji na super ego inadeal na morality ya unachohitaji.

Hakitakiwi chochote kuzidi katika hivyo vitatu.

Ikitokea kimezidi ndiyo unakua unajiona wewe ni zaidi ya sisi, wewe ni wewe katika mahusiano. It is a matter of time before uhusiano wako na wazazi ukaenda na maji pia.

Sasa fika ofisini kwangu Mtaa wa Congo Round about ya msimbazi ili nikupe huduma ya therapy juu ya hili swala. Unaweza nicheki kwa namba yangu pia ili nikupe huduma kwa njia ya simu.

Gharama ni nafuu.
Unaweza u-sympathy mkuu🤣🤣🤣 sema umenikumbusha mbali sana haya masuala ya
Id
Ego
Super ego
💯💯💯💯💯
 
Haaaaa mkuu hizo ni tabia za introvent so unatakiwa kujua hali yako hiyo na namna ya kuishi kwa amani na hiyo hali ,ukiweza hili hutopata shida,hata mimi niko hivyo sina mawasiliano wala mazoea na watu bila sababu za msingi na wala sipati shida yoyote labda kidogo kwenye mahusiano.
Ila kama huendeshwi na hisia za wanawake sio shida ila kama unatawaliwa na hizo hisia utapata tabu saaana upande huo
 
Aisee mimi hi tabia naipenda sana hata...kwenye simu...nina namba za watu muhimu tu pamoja na marafiki wachache sana....Lakini mimi kuna kitu kilisababisha hadi niwe kwenye tabia kama hiyo..
Binafsi hata mimi naipenda ila wengine sasa ndio wanapata shida sasa shida zao mimi hazinihusu maana huwezi nilazimisha niongee na wewe iwe unataka au hutaki,kama una jambo la msingi njoo ila kama huna wala siwezi kupoteza mda wangu
Hata mimi ni salamu afu miendo,nina marafiki wachache sana na vijiwe vichache saaana na bahati nzuri huwa napenda mpira tena kuangalia pekeyangu makelele na mabishano ya kwenye vibanda umiza naona kero sana.Uzuri wa hii tabia ni kwamba hutokuja kugombana na mtu popote pale si ofisini au nyumbani ila sasa uwe tayari kupitwa na fursa au matukio lakini pia jitahidi kujenga finanancial stability na kama ni shle uwe na uwezo hasa bila kutegemea wengine
 
Back
Top Bottom