mafioso
Member
- Jan 17, 2008
- 34
- 28
Wadau, salama?
Nakuja mbele zenu leo kuomba msaada wa mawazo juu ya mambo ya biashara. Mm sina uzoefu wa biashara, nimesomea IT, nimeajiriwa mwaka wa tano sasa, lakini nimekuja kugundua kipato changu kiko hali mbaya sababu ya mshahara finyu wa ajira, pesa nayopata ni ya kula na kodi tu ya nyumba, kdg na ada za watoto. Nina familia na nimeshtuka kuwa nisipofanya maarifa mapema maisha yatakuwa magumu huko mbeleni. Umri wangu ni miaka ipatayo thalatha.
Nina kila imani kuwa sasa ni wakati muafaka kutafuta kipato zaidi nje ya ajira yangu, ikibidi nikiweza kuestablish kitu changu basi niache ajira na nikisimamie kikamilifu ili kifanikiwe. Ninaishi Dar, nina budget ya 30M ambazo niko tayari kuziingiza kwenye shughuli nitakayoweza kuidentify ambayo niko tayari kuisimamia kwa nguvu zote.
Huko nyuma nimeshajaribu ufugaji wa kuku wa kizungu haukuwa na mafanikio sana pamoja na kusimamia kwa karibu sana, nikahamia kuku wa kienyeji ambao nafuga mpk sasa lkn kama mnavyojua, wale ukuaji wao ni wa muda mrefu sana, so sijaanza kufanya biashara. Nimeshajaribu kilimo, matunda, mahindi, viazi, maharagwe, lkn haikuwa na matokeo mazuri, nilipata hasara lkn sijakata tamaa katika kuhangaika.
Leo nakuja mbele yenu kuomba mchango wa mawazo maana naona nimestuck, ningependa kupata wazo la biashara, au shughuli ninayoweza kuifanya ikanizalishia kipato cha ziada. Kama nilivyosema, mm si mbobezi/mzoefu sana wa biashara lkn niko tayari kujifunza na kupambana na changamoto nitakazo kutana nazo.
Ni imani yangu nitapata michango chanya toka kwenu wadau, najua waosha vinywa hawatakosekana kwenye uzi huu lkn ndiyo changamoto zenyewe hizo kwenye mkusanyiko wa watu wengi.
Nawasilisha.
Nakuja mbele zenu leo kuomba msaada wa mawazo juu ya mambo ya biashara. Mm sina uzoefu wa biashara, nimesomea IT, nimeajiriwa mwaka wa tano sasa, lakini nimekuja kugundua kipato changu kiko hali mbaya sababu ya mshahara finyu wa ajira, pesa nayopata ni ya kula na kodi tu ya nyumba, kdg na ada za watoto. Nina familia na nimeshtuka kuwa nisipofanya maarifa mapema maisha yatakuwa magumu huko mbeleni. Umri wangu ni miaka ipatayo thalatha.
Nina kila imani kuwa sasa ni wakati muafaka kutafuta kipato zaidi nje ya ajira yangu, ikibidi nikiweza kuestablish kitu changu basi niache ajira na nikisimamie kikamilifu ili kifanikiwe. Ninaishi Dar, nina budget ya 30M ambazo niko tayari kuziingiza kwenye shughuli nitakayoweza kuidentify ambayo niko tayari kuisimamia kwa nguvu zote.
Huko nyuma nimeshajaribu ufugaji wa kuku wa kizungu haukuwa na mafanikio sana pamoja na kusimamia kwa karibu sana, nikahamia kuku wa kienyeji ambao nafuga mpk sasa lkn kama mnavyojua, wale ukuaji wao ni wa muda mrefu sana, so sijaanza kufanya biashara. Nimeshajaribu kilimo, matunda, mahindi, viazi, maharagwe, lkn haikuwa na matokeo mazuri, nilipata hasara lkn sijakata tamaa katika kuhangaika.
Leo nakuja mbele yenu kuomba mchango wa mawazo maana naona nimestuck, ningependa kupata wazo la biashara, au shughuli ninayoweza kuifanya ikanizalishia kipato cha ziada. Kama nilivyosema, mm si mbobezi/mzoefu sana wa biashara lkn niko tayari kujifunza na kupambana na changamoto nitakazo kutana nazo.
Ni imani yangu nitapata michango chanya toka kwenu wadau, najua waosha vinywa hawatakosekana kwenye uzi huu lkn ndiyo changamoto zenyewe hizo kwenye mkusanyiko wa watu wengi.
Nawasilisha.