NAHITAJI MSAADA WA KARIBU

NAHITAJI MSAADA WA KARIBU

amaniluhuha

Member
Joined
Sep 12, 2016
Posts
20
Reaction score
13
Wana jf mi ni mwanafunzi Wa Kampala university nachukua degree ya pharmacy BUT ninapoingia bord ya mkopo kuangalia kama nimepata mkopo nimekuta hivi YOU'RE NOT ALLOCATED A HIGHER EDUCATION LOAN FOR ANY 2016/2017 IN THE FIRST BATCH.

Sasa wadau haya maneno yana maana sijapata mkopo kabisa au nisubiri batch ya pili maana mimi nilichaguliwa na TCU Kwenye second selection. Mnisaidie kwa hilo
 
Subilia batch ya pili Mkuu usipanic
 
Ndio umekosa sema wametumia maneno yakukufariji.
 
Wakikwambia ukweli utapanic, hayo ni MANENO ya hekima ili kukufanya usije kujinyonga
 
.....unakufa tartiibu huku unajiona. Jaribu ongea na ndugu na jamaa wakuchangie ada laasivyo....utaniambia. Wameagizwa watumie busara siku zisogee..wasiseme hakuna mkopo ila wasubiri awamu ya pili...utatupa mrejesho...Ni mawazo tu...
 
Pole kwa changamoto... Ila sijaelewa... Ndo umejiunga chuo au unaendelea??? Coz Kama ni wa mwaka wa kwanza subiri batch ya pili.... Ila Kama ni mwanafunzi wa muendelezo nenda bodi mkayajenge.
 
Mkopo umekuwa shida sana khaaa na umasikini wetu, sijui vijana watafanyaje. Mungu awapiganie tu
 
Sio unachukua degree,
Sema unasoma degree!
Unachuka unaifaham kwani?
Ni ya kwako hadi uichukue?
Unachukua unajua ulipoiweka?

Pole kwa kukosa mkopo ndio serikali yetu hii tumeipenda wenyewe! Wacha waisome namba eeeeee
 
ndio fanya kusubiri batches zingne lakini huku ukiendlea kujipanga kutafuta pesa ya ada au kwa lolote.ila usiumie pambana na tafta plan b mapema mkuu
 
Back
Top Bottom